Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Pindua Kila Wazo Ambalo Ni Kinyume cha Ujuzi wa Mungu!
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2019 | Juni
    • 1. Mtume Paulo aliwaandikia Wakristo watiwa-mafuta onyo gani?

      “ACHENI,” mtume Paulo akaonya. Acheni nini? “Acheni kufinyangwa na mfumo huu wa mambo.” (Rom. 12:2) Paulo aliwaambia maneno hayo Wakristo wa karne ya kwanza. Kwa nini aliwapa onyo kali hivyo wanaume na wanawake waliokuwa wamejiweka wakfu kwa Mungu na kutiwa mafuta kwa roho takatifu?​—Rom. 1:7.

      2-3. Shetani hujaribu jinsi gani kutufanya tumwache Yehova, lakini tunaweza kung’oa jinsi gani mambo yaliyokita mizizi akilini mwetu?

      2 Paulo alitoa onyo hilo kwa sababu baadhi ya Wakristo walikuwa wakiathiriwa na mawazo yasiyofaa na falsafa zilizoendelezwa na ulimwengu wa Shetani. (Efe. 4:17-19) Yeyote miongoni mwetu anaweza kuathiriwa na mambo hayo. Katika jitihada zake za kufa na kupona za kutufanya tumwache Yehova, Shetani, mungu wa mfumo huu wa mambo, hutumia mbinu mbalimbali. Kwa mfano, anaweza kutumia mwelekeo wowote tulio nao wa kutamani kuwa mashuhuri au kuonekana kuwa watu muhimu. Huenda hata akatumia malezi yetu, utamaduni wetu, au elimu yetu ili kupotosha njia yetu ya kufikiri.

  • Pindua Kila Wazo Ambalo Ni Kinyume cha Ujuzi wa Mungu!
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2019 | Juni
  • Pindua Kila Wazo Ambalo Ni Kinyume cha Ujuzi wa Mungu!
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2019 | Juni
    • ‘KUFANYA UPYA AKILI YAKO’

      4. Ni mabadiliko gani ambayo wengi wetu tulihitaji kufanya tulipokubali kweli?

      4 Fikiria kuhusu mabadiliko uliyohitaji kufanya ulipokubali kweli ya Neno la Mungu na kuamua kumtumikia Yehova. Kwa wengi wetu, hilo lilihusisha kuacha mwenendo fulani usiofaa. (1 Kor. 6:9-11) Tunamshukuru sana Yehova kwa kutusaidia kushinda mazoea hayo mabaya!

      5. Ni mambo gani mawili yanayotajwa kwenye Waroma 12:2?

      5 Hata hivyo, hatupaswi kamwe kuhisi kwamba hatuhitaji kuendelea kufanya mabadiliko. Ingawa tuliacha kufanya dhambi nzito tulizokuwa tukifanya kabla ya kubatizwa, bado tunahitaji kuendelea kujitahidi kuepuka jambo lolote linaloweza kutushawishi kurudia matendo yetu ya awali. Tunawezaje kufanya hivyo? Paulo anaeleza hivi: “Acheni kufinyangwa na mfumo huu wa mambo, bali mgeuzwe kwa kufanya upya akili yenu.” (Rom. 12:2) Hivyo, ni lazima tufanye mambo mawili. Kwanza, tunahitaji ‘kuacha kufinyangwa,’ au kuongozwa na ulimwengu huu. Pili, tunahitaji ‘kugeuzwa’ kwa kufanya upya akili yetu.

      Ni Kugeuzwa au Ni Kujifanya?

      Kijana ambaye hajali mwonekano wake, hajanyoa ndevu wala kuchana nywele, lakini ameshika picha yake akiwa safi na nadhifu na akiwa amevalia shati na tai

      Neno la Kigiriki linalotafsiriwa ‘kugeuzwa’ lililo kwenye Waroma 12:2 linarejelea badiliko la umbo au muundo wa kitu, kama vile kiwavi anavyobadilika na kuwa kipepeo. Kugeuzwa kunamaanisha kubadili jinsi tulivyo kwa ndani, yaani, utu wetu, asili yetu. Kinyume cha hilo, neno la Kigiriki linalotafsiriwa “kujifanya” kwenye 2 Wakorintho 11:13-15 linarejelea badiliko la nje tu, yaani, mwonekano wetu wa nje.

      6. Tunajifunza nini kutokana na wazo linalopatikana katika maneno ya Yesu kwenye Mathayo 12:43-45?

      6 Kugeuzwa ambako Paulo alikuwa akizungumzia kunahusisha mengi zaidi ya kubadili mwonekano wetu wa nje. Kunahusisha kila sehemu ya utu wetu. (Tazama sanduku, “Ni Kugeuzwa au Ni Kujifanya?”) Tunahitaji kufanya upya akili yetu, yaani, mitazamo yetu ya ndani kabisa, hisia zetu, na mielekeo yetu. Hivyo, kila mmoja wetu anahitaji kujiuliza, ‘Je, mabadiliko ninayofanya ili niwe Mkristo ni ya kijuujuu tu, au ninajitahidi kuyafanya yapenye na kufika ndani kabisa ya utu wangu?’ Ni muhimu tujue tofauti kati ya mambo hayo mawili. Maneno ya Yesu kwenye Mathayo 12:43-45, yanaonyesha jambo tunalohitaji kufanya. (Soma.) Wazo tunalopata kutokana na maneno hayo linakazia ukweli huu muhimu: Haitoshi tu kuondoa mawazo yasiyofaa akilini mwetu; tunahitaji pia kujaza pengo hilo mawazo yanayompendeza Mungu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki