-
Jihadhari na Moyo Wenye HilaMungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
-
-
7 Mkristo anaweza kufikiri kimakosa kwamba moyo wake hauwezi kamwe kumdanganya, kama wengi walivyofikiri katika siku za Yeremia. Kwa mfano, huenda mtu akasema, ‘Lazima nifanye kazi ili niruzuku familia yangu,’ jambo ambalo linaeleweka. Lakini namna gani akianza kufikiri, ‘Nahitaji kuongeza elimu ili kupata kazi nzuri zaidi’? Huenda hilo pia likaonekana kuwa wazo linalofaa, ambalo huenda likamfanya awaze: ‘Mambo yamebadilika siku hizi, mtu anahitaji kusoma hadi chuo cha ufundi au chuo kikuu ili asije akapoteza kazi.’ Bila kuwa mwangalifu, mtu anaweza kuanza kupuuza shauri lenye hekima, na lenye usawaziko kutoka kwa jamii ya mtumwa mwaminifu na mwenye busara kuhusu elimu ya ziada, na kuanza kukosa mikutano! Wengine wamefinyangwa na maoni ya ulimwengu kuhusu elimu. (Efe. 2:2, 3) Biblia inaonya hivi: “Msiige tabia na mienendo ya dunia hii.”—Rom. 12:2, Neno—Agano Jipya.a
Je, moyo wako umekudanganya ukose mikutano?
-
-
Jihadhari na Moyo Wenye HilaMungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
-
-
a Tafsiri ya NET Bible (2005) inasema: “Msipatanishwe na ulimwengu wa sasa.” Maelezo ya chini yanaongeza: “Inaonekana kwamba si lazima mtu achukue hatua ili ‘kupatanishwa’ na ulimwengu wa sasa, ni jambo linalotendeka, kwa kiasi fulani, pasipo hata mtu kufikiria. Hata hivyo, . . . huenda kwa kiasi fulani mtu akatambua na kukubali mabadiliko yanayoendelea. Yawezekana kwamba hali zote mbili zinahusika.”
-