-
“Wakeni Roho”Mnara wa Mlinzi—2009 | Oktoba 15
-
-
9. Kwa nini Paulo anawalinganisha Wakristo waliozaliwa kwa roho na viungo vya mwili?
9 Soma Waroma 12:4, 5, 9, 10. Paulo anawalinganisha Wakristo watiwa-mafuta na viungo vya mwili, wanapotumikia kwa umoja chini ya Kichwa chao, Kristo. (Kol. 1:18) Anawakumbusha Wakristo waliozaliwa kwa roho kwamba mwili una viungo vingi, lakini vina kazi tofauti na kwamba ‘ingawa ni wengi, wao ni mwili mmoja katika muungano na Kristo.’ Vivyo hivyo, Paulo aliwahimiza hivi Wakristo watiwa-mafuta huko Efeso: “Na tukue kwa upendo katika mambo yote ndani yake yeye aliye kichwa, Kristo. Kutoka katika yeye mwili wote, kwa kuunganishwa pamoja kwa upatano na kufanywa ushirikiane kupitia kila kiungo ambacho hutoa kile kinachohitajiwa, kulingana na utendaji wa kila kiungo kimoja-kimoja katika kipimo kinachofaa, hutokeza ukuzi wa mwili ili huo ujijenge wenyewe katika upendo.”—Efe. 4:15, 16.
-
-
“Wakeni Roho”Mnara wa Mlinzi—2009 | Oktoba 15
-
-
11. Umoja wetu unategemea nini, na Paulo alitoa shauri gani lingine?
11 Umoja huo unategemea upendo, ambao ni “kifungo kikamilifu cha muungano.” (Kol. 3:14) Kwenye Waroma sura ya 12, Paulo anakazia hilo anaposema kwamba upendo wetu unapaswa kuwa “bila unafiki” na kwamba “katika upendo wa kindugu” tunapaswa kuwa na “upendo mwororo kwa mtu na mwenzake.” Hilo linatufanya tuheshimiane. Mtume Paulo anasema hivi: “Katika kuonyeshana heshima iweni wa kwanza.” Bila shaka, hatupaswi kufikiri kwamba upendo ni hisia tu ya moyoni. Tunapaswa kufanya yote tunayoweza ili kudumisha usafi wa kutaniko. Anapotoa shauri lake kuhusu upendo, Paulo anaongezea hivi: “Chukieni maovu, shikamaneni na mema.”
-