-
“Lieni Pamoja na Watu Wanaolia”Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Julai
-
-
14. Tunaweza kufanya nini ili kuwafariji waliofiwa?
14 Hivyo basi, inaeleweka kwamba nyakati nyingine ni vigumu kujua jambo la kumwambia mtu aliyelemewa na huzuni. Hata hivyo, Biblia inasema kwamba “ulimi wa mwenye hekima huponya.” (Met. 12:18) Watu wengi wamepata mawazo yenye kufariji wanayoweza kuwaeleza wengine katika broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa.c Hata hivyo, mara nyingi jambo linalofariji zaidi ni “[kulia] pamoja na watu wanaolia.” (Rom. 12:15) Gaby, ambaye alifiwa na mume wake, anakiri hivi: “Mimi hulia mara nyingi, na kila ninapolia ninahisi kama ninaeleza hisia zangu. Hiyo ndiyo sababu mimi hufarijika marafiki wanapolia pamoja nami. Wakati huo, sijihisi nikiwa peke yangu ninapohuzunika.”
-
-
“Lieni Pamoja na Watu Wanaolia”Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Julai
-
-
20. Kwa nini ahadi za Yehova zinafariji sana?
20 Inafariji sana kujua kwamba Yehova, Mungu wa faraja yote, ataondoa huzuni yote na kuandaa faraja ya kudumu wakati ambapo “wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti [ya Kristo] na kutoka”! (Yoh. 5:28, 29) Mungu anaahidi kwamba “atameza kifo milele na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova hakika atafuta machozi katika nyuso zote.” (Isa. 25:8) Wakati huo, badala ya “[kulia] pamoja na watu wanaolia,” wakaaji wote wa dunia “[watashangilia] pamoja na watu wanaoshangilia.”—Rom. 12:15.
-