Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Msimlipe Yeyote Uovu Kwa Uovu”
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Julai 1
    • “Msijilipizie Kisasi Wenyewe”

      15. Andiko la Waroma 12:19 linaonyesha sababu gani ya kutolipiza kisasi?

      15 Paulo anatoa sababu nyingine nzuri ya kutolipiza kisasi; mwenendo huo unaonyesha kwamba tuna sifa ya kiasi. Anasema hivi: “Wapendwa, msijilipizie kisasi wenyewe bali iachieni nafasi ghadhabu; kwa maana imeandikwa: ‘Kisasi ni changu; mimi nitalipa, asema Yehova.’” (Waroma 12:19) Mkristo ambaye anajaribu kulipiza kisasi ana kimbelembele. Anajichukulia daraka ambalo ni la Mungu. (Mathayo 7:1) Kwa kuongezea, anapojichukulia mambo mikononi mwake, anaonyesha kwamba hana imani katika uhakikisho huu wa Yehova: “Mimi nitalipa.” Kinyume cha hilo, Wakristo wa kweli wanasadiki kwamba Yehova “atasababisha haki ifanywe kwa ajili ya watu wake waliochaguliwa.” (Luka 18:7, 8; 2 Wathesalonike 1:6-8) Wanaonyesha sifa ya kiasi kwa kumwachia Mungu daraka la kulipiza uovu.—Yeremia 30:23, 24; Waroma 1:18.

  • “Msimlipe Yeyote Uovu Kwa Uovu”
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Julai 1
    • 18. Kwa nini kutolipiza kisasi ni jambo linalofaa, la upendo, na la kiasi?

      18 Katika mazungumzo haya mafupi ya Waroma sura ya 12, tumeona sababu fulani muhimu zinazofanya ‘tusimlipe yeyote uovu kwa uovu.’ Kwanza, kutolipiza kisasi ni jambo linalofaa. Kwa sababu ya huruma ambazo Mungu ametuonyesha, ni jambo zuri na linalofaa kujitoa wenyewe kwa Yehova na kutii amri zake kwa kupenda, kutia ndani amri ya kuwapenda adui zetu. Pili, kutolipa uovu kwa uovu ni kuonyesha upendo. Tunapofanya amani na kutolipiza kisasi, tunatumaini kwa upendo kwamba tutawasaidia hata wapinzani fulani wakali wawe waabudu wa Yehova. Tatu, tunaonyesha sifa ya kiasi kwa kutolipa uovu kwa uovu. Kujilipizia kisasi ni kuwa na kimbelembele, kwa kuwa Yehova anasema: “Kisasi ni changu.” Neno la Mungu linatuonya hivi pia: “Je, kimbelembele kimekuja? Basi aibu itakuja; lakini wenye kiasi wana hekima.” (Methali 11:2) Tunaonyesha sifa ya kiasi tunapomwachia Mungu daraka la kulipiza uovu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki