-
‘Endeleeni Kuushinda Uovu’ kwa Kuizuia HasiraMnara wa Mlinzi—2010 | Juni 15
-
-
10. Wakristo wanapaswa kuwa na mtazamo gani kuhusu kulipiza kisasi?
10 Kisa cha Simeoni na Lawi na kisa cha Daudi na Abigaili kinaonyesha waziwazi kwamba Yehova anapinga hasira inayopita mipaka na jeuri na kwamba anawabariki wale wanaojitahidi kufanya amani. Mtume Paulo aliandika hivi: “Ikiwezekana, kwa kadiri inavyowategemea ninyi, iweni wenye kufanya amani na watu wote. Wapendwa, msijilipizie kisasi wenyewe bali iachieni nafasi ghadhabu; kwa maana imeandikwa: ‘Kisasi ni changu; mimi nitalipa, asema Yehova.’ Lakini, ‘ikiwa adui yako ana njaa, mlishe; ikiwa ana kiu, mpe kitu anywe; kwa maana kwa kufanya hivyo utakusanya makaa yenye moto juu ya kichwa chake.’ Usiache ushindwe na uovu, bali endelea kuushinda uovu kwa wema.”—Rom. 12:18-21.a
-
-
‘Endeleeni Kuushinda Uovu’ kwa Kuizuia HasiraMnara wa Mlinzi—2010 | Juni 15
-
-
a “Makaa yenye moto” yalitumiwa zamani kuyeyusha mawe yenye madini ya chuma kwa kuchoma mawe hayo kwa moto juu na chini ili kupata chuma. Tunapowaonyesha fadhili watu wanaotenda bila fadhili tunaweza kuwafanya wabadili mtazamo wao na kuonyesha sifa zao nzuri.
-