Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Iweni Wenye Kufanya Amani na Watu Wote”
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Oktoba 15
    • Kuushinda Uovu kwa Wema

      13, 14. (a) Kwa nini hatushangai tunapopata upinzani? (b) Tunaweza kuwabariki jinsi gani wale wanaotutesa?

      13 Soma Waroma 12:14, 21. Tukiwa na uhakika kabisa kwamba Yehova atatimiza ahadi zake, tunaweza bila wasiwasi kutumia nguvu zetu zote katika kazi ambayo ametupatia, kazi ya kuhubiri ‘habari njema ya ufalme katika dunia yote inayokaliwa.’ (Mt. 24:14) Tunajua kwamba utendaji huo wa Kikristo utaamsha hasira ya maadui wetu, kwa kuwa Yesu alituonya hivi: “Mtachukiwa na mataifa yote kwa sababu ya jina langu.” (Mt. 24:9) Kwa hiyo, hatushangai wala kuvunjika moyo tunapopata upinzani. Mtume Petro aliandika hivi: “Wapendwa, msishangazwe juu ya moto unaowaka katikati yenu, unaowapata ninyi ili kuwa jaribu, kana kwamba jambo geni linawapata. Kinyume chake, endeleeni kushangilia kwa maana ninyi ni washiriki katika mateso ya Kristo.”—1 Pet. 4:12, 13.

  • “Iweni Wenye Kufanya Amani na Watu Wote”
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Oktoba 15
    • 15. Ni njia gani bora ya kuushinda uovu kwa wema?

      15 Hivyo basi, Mkristo wa kweli anatii maneno ya mstari wa mwisho wa Waroma sura ya 12: “Usiache ushindwe na uovu, bali endelea kuushinda uovu kwa wema.” Chanzo cha uovu wote ni Shetani Ibilisi. (Yoh. 8:44; 1 Yoh. 5:19) Katika ufunuo ambao mtume Yohana alipewa, Yesu alifunua kwamba ndugu zake watiwa-mafuta ‘wamemshinda [Shetani] kwa sababu ya damu ya Mwana-Kondoo na kwa sababu ya neno la kutoa kwao ushahidi.’ (Ufu. 12:11) Hilo linaonyesha kwamba njia bora ya kumshinda Shetani na uvutano wake mwovu juu ya mfumo wa sasa wa mambo ni kwa kufanya mema kupitia kazi yetu ya kutoa ushahidi na kuhubiri habari njema ya Ufalme.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki