-
Mimweko ya Nuru—Mikubwa na Midogo (Sehemu ya Pili)Mnara wa Mlinzi—1995 | Mei 15
-
-
“Mamlaka za Juu Zaidi” Zaeleweshwa Wazi
4, 5. (a) Wanafunzi wa Biblia walionaje Warumi 13:1? (b) Ni nini lililoonwa baadaye kuwa msimamo wa Kimaandiko kuhusu “mamlaka za juu zaidi”?
4 Mmweko mwangavu wa nuru ulionwa katika 1962 kuhusu Warumi 13:1, lisemalo: “Kila nafsi na ijitiishe kwa mamlaka za juu zaidi [“mamlaka zilizo kubwa,” NW].” (King James Version) Wanafunzi wa Biblia wa mapema walielewa kwamba “mamlaka za juu zaidi” zinazotajwa hapo zilirejezea mamlaka za kilimwengu. Wao walielewa kuwa andiko hili lilimaanisha kwamba ikiwa Mkristo angesajiliwa katika vita, angewajibika kuvaa yunifomu, abebe bunduki, na kwenda vitani, katika mitaro. Ilifikiriwa kwamba kwa kuwa Mkristo hangeua mwanadamu mwenzake, yeye angelazimishwa kufyatua bunduki yake hewani hali ikiwa mbaya zaidi.a
5 Mnara wa Mlinzi la Novemba 15 na la Desemba 1, 1962, yaliangaza nuru iliyo wazi kwa habari hiyo yalipozungumzia maneno ya Yesu kwenye Mathayo 22:21: “Mlipeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na Mungu yaliyo ya Mungu.” Yaliyohusika na habari hiyo yalikuwa maneno ya mitume kwenye Matendo 5:29: “Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu.” Wakristo hujitiisha kwa Kaisari—“mamlaka za juu zaidi”—maadamu tu Mkristo hahitajiki kukiuka sheria ya Mungu. Ujitiisho kwa Kaisari ulionwa kuwa wa kadiri, si kamili. Wakristo hulipa Kaisari yale tu ambayo hayapingi matakwa ya Mungu. Iliridhisha kama nini kuwa na nuru iliyo wazi kwa habari hiyo!
-
-
Mimweko ya Nuru—Mikubwa na Midogo (Sehemu ya Pili)Mnara wa Mlinzi—1995 | Mei 15
-
-
a Kwa kuitikia maoni hayo, The Watch Tower la Juni 1 na la Juni 15, 1929, yalifasiri “mamlaka za juu zaidi” kuwa Yehova Mungu na Yesu Kristo. Ni msimamo huo uliorekebishwa hasa katika 1962.
-