Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwigeni Yehova, Mungu Wetu Asiye na Ubaguzi
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Juni 15
    • 11. Kutendea watu bila ubaguzi kulionyeshwaje katika kutaniko la kwanza la Kikristo?

      11 Katika kutaniko la kwanza la Kikristo, Wayahudi na watu wa mataifa walikuwa sawasawa. Paulo alieleza hivi: “Utukufu na heshima na amani kwa kila mtu afanyaye lililo jema, kwa Myahudi kwanza na pia kwa Mgiriki. Kwa maana hakuna ubaguzi kwa Mungu.”b (Waroma 2:10, 11) Kile kilichoamua kama wangenufaika na fadhili zisizostahiliwa za Yehova, si asili yao, bali ni jinsi walivyotenda baada ya kujifunza kumhusu Yehova na matarajio yaliyotolewa na fidia ya Mwana wake Yesu. (Yohana 3:16, 36) Paulo aliandika: “Kwa maana yeye si Myahudi aliye hivyo kwa nje, wala tohara si ile ambayo ni ya nje juu ya mwili. Bali yeye ni Myahudi aliye hivyo kwa ndani, na tohara yake ni ile ya moyo kwa roho, wala si kwa mfumo fulani wa sheria iliyoandikwa.” Kisha kwa kubadili maneno yanayohusu jina “Myahudi” (linalomaanisha “wa Yuda,” yaani, aliyesifiwa), Paulo aliongeza kusema hivi: “Sifa ya huyo huja, si kutoka kwa wanadamu, bali kutoka kwa Mungu.” (Waroma 2:28, 29) Yehova huwasifu watu bila ubaguzi. Je, sisi nasi hufanya hivyo?

  • Mwigeni Yehova, Mungu Wetu Asiye na Ubaguzi
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Juni 15
    • b Hapa, neno “Wagiriki” linamaanisha watu wa Mataifa kwa ujumla.—Insight on the Scriptures, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova, Buku la Kwanza, ukurasa wa 1004.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki