-
Sehemu ya Mamlaka za Juu ZaidiMnara wa Mlinzi—1990 | Novemba 1
-
-
Wakristo wa Kweli
‘Hawapingi Mamlaka’
3, 4. (a) Ni kanuni gani zavunjwa na waitwao eti Wakristo ambao huunga mkono mapinduzi? (b) Mtu mmoja aligundua nini juu ya Mashahidi wa Yehova?
3 Katika karne ya kwanza, Yesu alisema juu ya wafuasi wake hivi: “Wao si sehemu ya ulimwengu, kama vile mimi nisivyo sehemu ya ulimwengu.” (Yohana 17:14, NW) Yeyote aitwaye eti Mkristo ambaye huunga mkono mapinduzi yuko sana sehemu ya ulimwengu. Yeye si mfuasi wa Yesu; wala ‘hatii mamlaka za juu zaidi.’ (Warumi 13:1, NW) Ingekuwa vema atii onyo la mtume Paulo kwamba “yeye ambaye hupinga mamlaka amechukua msimamo dhidi ya mpango wa Mungu; wale ambao wamechukua msimamo dhidi yayo watapokea hukumu kwao wenyewe.”—Warumi 13:2, NW.
4 Kwa utofautisho na wengi katika Jumuiya ya Wakristo, Mashahidi wa Yehova hawashughuliki na jeuri ya kutumia silaha. Mwanamume mmoja katika Ulaya aligundua hilo. Aandika hivi: “Kwa kuona matokeo ya dini na siasa, nilijitoa kuupindua utaratibu wa kijamii uliothibitika. Nilijiunga na kikundi cha wavamizi-haramu nikapokea mazoezi katika kushughulika na namna zote za silaha; nilishiriki katika visa vingi vya unyang’anyi wa kutumia silaha. Maisha yangu yalikuwa katika hatari daima. Kadiri wakati ulivyopita, ilionekana wazi kwamba tulikuwa tukipigana bure tu. Mimi nilikuwa mwanamume aliyevurugika fikira, aliye hoi kabisa kwa kukosa tumaini katika maisha. Ndipo Shahidi mmoja wa kike akabisha mlango wetu. Aliniambia juu ya Ufalme wa Mungu. Kwa kusisitiza kwamba kulikuwa ni kupoteza wakati wangu, nikadokeza kwamba mke wangu asikilize. Alifanya hivyo, na funzo la nyumbani la Biblia likaanzwa. Mwishowe, niliafiki kuhudhuria funzo hilo. Nashindwa kupata maneno ya kueleza kitulizo nilichohisi kwa kuielewa kani yenye kushurutisha ainabinadamu kuelekea uovu. Ahadi nzuri sana ya Ufalme imenipa tumaini lenye utegemezo na kusudi katika maisha.”
-
-
Sehemu ya Mamlaka za Juu ZaidiMnara wa Mlinzi—1990 | Novemba 1
-
-
6. Kwa nini sheria nyingi za kibinadamu ni njema hata ingawa “ulimwengu wote unatawaliwa na yule Mwovu”?
6 Serikali za kitaifa huweka mifumo ya sheria, na zilizo nyingi za sheria hizi ni njema. Je! hilo litushangaze, kwa sababu ya uhakika wa kwamba “ulimwengu wote unatawaliwa na yule Mwovu”? (1 Yohana 5:19, HNWW) Sivyo. Yehova alimpa baba yetu wa awali, Adamu, dhamiri, na hisi hii ya kindani ya yafaayo na yenye makosa huonyeshwa kwa njia nyingi katika sheria za kibinadamu. (Warumi 2:13-16) Hammurabi, mpaji-sheria wa kale Mbabulonia, alitoa dibaji ya fungu la sheria zake kama ifuatavyo: “Wakati huo [wao wali-]nitaja mimi ili nisaidie kukuza hali njema ya watu, mimi, Hammurabi, yule mwana-mfalme mwenye ujitoaji, mwenye kuhofu mungu, ili kusababisha haki idumu katika bara, ili kuharibu waovu na uovu, kwamba walio imara wasiweze kuonea walio dhaifu.”
-