Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi ya Kufanya Maamuzi Mazuri
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 5. Heshimu dhamiri za watu wengine

      Maamuzi yetu hutofautiana na maamuzi ya watu wengine. Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunaheshimu dhamiri za watu wengine? Fikiria hali mbili zinazofuata:

      Hali ya 1: Dada anayependa kujipamba anahamia kutaniko ambalo dada wengi wanakwazika wanapoona watu wakijipamba.

      Soma Waroma 15:1 na 1 Wakorintho 10:23, 24, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Kulingana na maandiko haya, dada huyo anaweza kuamua kufanya nini? Utafanya nini unaposhughulika na mtu ambaye dhamiri yake inamkataza kufanya jambo ambalo dhamiri yako inakubali?

      Hali ya 2: Ndugu ambaye anajua kwamba Biblia haikatazi kunywa kileo kwa kiasi, lakini anaamua kutokunywa kileo. Anakaribishwa kwenye tafrija ambapo anaona akina ndugu wakinywa kileo.

      Soma Mhubiri 7:16 na Waroma 14:1, 10, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Kulingana na maandiko haya, ndugu huyo anaweza kuamua kufanya nini? Utafanya nini ukimwona mtu anafanya jambo ambalo dhamiri yako inakuzuia kufanya?

      Hatua zinazotusaidia kufanya maamuzi mazuri.

      Mwanamke akisali.

      1. Mwombe Yehova akusaidie kuamua jambo la kufanya.​—Yakobo 1:5.

      Mwanamke huyo akifanya utafiti kwa kutumia Biblia, machapisho yanayotegemea Biblia, na kompyuta.

      2. Fanya utafiti katika Biblia na machapisho yanayotegemea Biblia ili upate kanuni zinazohusika. Unaweza pia kuzungumza na Wakristo wenye uzoefu.

      Mwanamke huyo akifikiria.

      3. Fikiria matokeo ya uamuzi utakaofanya, yaani, jinsi utakavyoathiri dhamiri yako na dhamiri za watu wengine.

  • Kwa Nini Mavazi na Mwonekano Wetu Ni Muhimu?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 2. Kwa nini tunapaswa kuwafikiria waabudu wenzetu tunapochagua mavazi?

      Ingawa tuna uhuru wa kuchagua mavazi tutakayovaa, tunapaswa kufikiria jinsi mwonekano wetu utakavyowaathiri wengine. Tunajitahidi sana kuepuka kumkwaza mtu yeyote. Badala yake, ‘tunampendeza jirani yetu kwa mema ili kumjenga.’​—Soma Waroma 15:1, 2.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki