Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wazee Wakristo Ni ‘Wafanyakazi Wenzi Kwa Shangwe Yetu’
    Mnara wa Mlinzi—2013 | Januari 15
    • 6, 7. (a) Ni kwa njia gani moja wazee wanaweza kumwiga Yesu, Paulo, na watumishi wengine wa Mungu? (b) Kwa nini kukumbuka majina ya ndugu zetu kunaongeza shangwe yao?

      6 Ndugu na dada zetu wengi wanasema kwamba shangwe yao inaongezeka wazee wanapopendezwa nao kibinafsi. Njia moja ya msingi ambayo wazee wanafanya hivyo ni kwa kuiga mfano wa Daudi, Elihu, na Yesu mwenyewe. (Soma 2 Samweli 9:6; Ayubu. 33:1; Luka 19:5.) Kila mmoja wa watumishi hao wa Yehova alipendezwa kikweli na mtu fulani kwa kumwita kwa jina lake. Paulo pia alithamini umuhimu wa kukumbuka na kutumia majina ya waamini wenzake. Alimalizia moja ya barua zake kwa kuwasalimu ndugu na dada zaidi ya 25 kwa majina, kutia ndani Persisi, dada Mkristo ambaye Paulo alisema hivi kumhusu: “Salimuni Persisi mpendwa wetu.”—Rom. 16:3-15.

  • Wazee Wakristo Ni ‘Wafanyakazi Wenzi Kwa Shangwe Yetu’
    Mnara wa Mlinzi—2013 | Januari 15
    • 8. Paulo aliwaiga Yehova na Yesu kwa njia gani moja muhimu?

      8 Paulo pia alipendezwa na wengine kwa kuwapongeza kwa unyoofu, na hiyo ni njia nyingine ya msingi ya kuongeza shangwe ya waamini wenzetu. Hivyo, baada ya Paulo kusema kwamba alitamani kufanya kazi kwa shangwe ya ndugu zake, aliandika hivi katika barua hiyohiyo: “Ninajisifu kwa njia kubwa kuhusiana nanyi.” (2 Kor. 7:4) Bila shaka, maneno hayo ya pongezi yaliichangamsha mioyo ya ndugu huko Korintho. Paulo aliyasifu makutaniko mengine kwa njia hiyohiyo. (Rom. 1:8; Flp. 1:3-5; 1 The. 1:8) Baada ya kumtaja Persisi katika barua yake kwa kutaniko la Roma, Paulo aliongezea hivi: “Alifanya kazi nyingi katika Bwana.” (Rom. 16:12) Dada huyo mwaminifu alitiwa moyo kama nini na pongezi hiyo! Paulo aliwaiga Yehova na Yesu katika kuwapongeza wengine.—Soma Marko 1:9-11; Yohana 1:47; Ufu. 2:2, 13, 19.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki