-
Mlo wa Jioni wa Bwana—Huo Wapaswa Uadhimishwe Mara Nyingi Kadiri Gani?Mnara wa Mlinzi—1994 | Machi 15
-
-
Kumbuka pia kwamba Yesu alianzisha mwadhimisho huu halafu akafa katika tarehe ya kalenda ya Kiyahudi ya Nisani 14.a Hiyo ilikuwa siku ya Sikukuu ya Kupitwa, sherehe iliyokumbusha Wayahudi juu ya ule ukombozi mkubwa waliopata katika Misri katika karne ya 16 K.W.K. Wakati huo, dhabihu ya mwana-kondoo ilitokeza ukombozi wa wazaliwa wa kwanza wa Wayahudi, hali malaika wa Yehova aliwaua wazaliwa wa kwanza wote wa Wamisri.—Kutoka 12:21, 24-27.
Hilo lasaidiaje uelewevu wetu? Mtume Mkristo Paulo aliandika hivi: “Kristo kupitwa kwetu ametolewa dhabihu.” (1 Wakorintho 5:7, NW) Kifo cha Yesu kilikuwa dhabihu ya Sikukuu ya Kupitwa iliyo kuu zaidi, ikitolea ainabinadamu fursa ya ukombozi ulio mtukufu zaidi. Hivyo, kwa Wakristo, Ukumbusho wa kifo cha Kristo umechukua mahali pa Sikukuu ya Kupitwa ya Kiyahudi.—Yohana 3:16.
Sikukuu ya Kupitwa ilikuwa sherehe ya kila mwaka. Hivyo, kwa kusababu kuzuri, Ukumbusho pia hufanywa kila mwaka. Sikukuu ya Kupitwa—ile siku ambayo Yesu alikufa—ilifanywa sikuzote kwenye siku ya 14 ya mwezi wa Kiyahudi wa Nisani. Kwa hiyo, kifo cha Kristo chapaswa kukumbukwa mara moja kwa mwaka kwenye siku ya kalenda inayolingana na Nisani 14. Katika 1994 siku hiyo ni Jumamosi, Machi 26, baada ya jua kushuka. Hata hivyo, kwa nini makanisa ya Jumuiya ya Wakristo hayajaifanya hiyo kuwa siku ya mwadhimisho wa pekee? Kuchunguza historia kifupi kutajibu swali hilo.
-
-
Mlo wa Jioni wa Bwana—Huo Wapaswa Uadhimishwe Mara Nyingi Kadiri Gani?Mnara wa Mlinzi—1994 | Machi 15
-
-
a Nisani, mwezi wa kwanza wa mwaka wa Kiyahudi, ulianza kwa kuonekana kwa mwezi mpya kwa mara ya kwanza. Hivyo sikuzote Nisani 14 ilifika wakati wa mwezi mpevu.
-