-
Utasimamaje Mbele ya Kiti cha Hukumu?Mnara wa Mlinzi—1995 | Oktoba 15
-
-
12 Basi, kwa Danieli kumwona Mungu ‘akiketi katika kiti cha ufalme’ kulimaanisha kuja Kwake kutoa hukumu. Mapema zaidi Daudi aliimba: “[Wewe Yehova] umenifanyia hukumu na haki; umeketi kitini pa enzi [“ufalme,” NW] ukihukumu kwa haki.” (Zaburi 9:4, 7) Na Yoeli aliandika: “Mataifa na wajihimize, wakapande juu katika bonde la Yehoshafati; maana huko ndiko [mimi Yehova] nitakakoketi niwahukumu mataifa yote.” (Yoeli 3:12; linganisha Isaya 16:5.) Yesu na Paulo vilevile walikuwa katika hali za kihukumu ambamo mwanadamu fulani aliketi ili kusikiza kesi na kutoa hukumu.b—Yohana 19:12-16; Matendo 23:3; 25:6.
-
-
Utasimamaje Mbele ya Kiti cha Hukumu?Mnara wa Mlinzi—1995 | Oktoba 15
-
-
b Kuhusu jambo la Wakristo kupelekana mahakamani, Paulo aliuliza: “Je, ni watu wadharauliwao katika kutaniko ambao mwawaweka kuwa mahakimu [kihalisi “mnafanya waketi”]?”—1 Wakorintho 6:4, NW.
-