-
Ufalme wa Mungu Ni Nini?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
7. Sheria za Ufalme wa Mungu ni bora zaidi
Serikali huweka sheria ambazo zimekusudiwa kuwanufaisha na kuwalinda raia wake. Ufalme wa Mungu pia una sheria ambazo zinapaswa kufuatwa na raia wake. Soma 1 Wakorintho 6:9-11, kisha mzungumzie maswali haya:
Unafikiri ulimwengu utakuwaje kila mtu atakapofuata sheria za Mungu?a
Je, unafikiri Yehova ana haki ya kuwawekea sheria raia wa Ufalme wake? Kwa nini?
Ni nini kinachoonyesha kwamba watu ambao hawafuati sheria hizo wanaweza kubadilika?—Ona mstari wa 11.
Serikali huweka sheria ili kuwalinda na kuwanufaisha raia wake. Ufalme wa Mungu una sheria bora zinazowalinda na kuwanufaisha raia wake
-
-
Biblia Inasema Nini Kuhusu Ngono?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
Yehova anajua mambo yanayotufaa kabisa. Anatufundisha jinsi ya kudumisha maadili safi na manufaa ya kufanya hivyo. Soma Methali 7:7-27 au onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.
Kijana huyo aliingiaje katika kishawishi?—Ona Methali 7:8, 9.
Kulingana na Methali 7:23, 26, uasherati unaweza kuwa na matokeo mabaya sana. Tukidumisha maadili safi tutaepuka matatizo gani?
Kuwa na maadili safi kunawezaje kutusaidia kufurahia maisha milele?
Baadhi ya watu wanafikiri kwamba mambo ambayo Biblia inafundisha kuhusu ngono kati ya watu wa jinsia moja, si jambo la upendo kuwaelekea watu hao. Lakini Yehova ni Mungu mwenye upendo na anataka watu wote wafurahie maisha milele. Ili tustahili kuishi milele, lazima tufuate viwango vyake vya maadili. Soma 1 Wakorintho 6:9-11, kisha mzungumzie swali hili:
Je, Mungu anachukizwa tu na ngono kati ya watu wa jinsia moja au kuna mambo mengine yanayomchukiza?
Ili tumfurahishe Mungu, sisi sote tunahitaji kufanya mabadiliko. Je, tunanufaika tunapofanya mabadiliko hayo? Soma Zaburi 19:8, 11, kisha mzungumzie maswali haya:
Je, unafikiri viwango vya Yehova kuhusu maadili vinafaa? Kwa nini?
Yehova amewasaidia watu wengi watii viwango vyake vya maadili. Anaweza kukusaidia pia
-
-
Wakristo Wanapaswa Kuwa na Maoni Gani Kuhusu Kileo?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
6. Jinsi ya kushinda zoea la kunywa kupita kiasi
Ona jambo lililomsaidia mwanamume fulani ashinde zoea la kunywa kileo kupita kiasi. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.
Katika video hiyo, Dmitry alitendaje baada ya kunywa kileo?
Je, ilikuwa rahisi kwake kuacha mara moja zoea hilo?
Mwishowe, nini kilichomsaidia kushinda uraibu wa kunywa kileo?
Soma 1 Wakorintho 6:10, 11, kisha mzungumzie maswali haya:
Kwa nini ulevi ni kosa zito?
Ni nini kinachoonyesha kwamba mtu aliye na zoea la kunywa kupita kiasi anaweza kubadilika?
Soma Mathayo 5:30, kisha mzungumzie swali hili:
Kukata mkono kunamaanisha kwamba mtu anapaswa kuacha tabia fulani ili amfurahishe Yehova. Unaweza kufanya nini ikiwa unapambana kushinda zoea la kunywa kileo kupita kiasi?a
Soma 1 Wakorintho 15:33, kisha mzungumzie swali hili:
Rafiki zako wanawezaje kufanya unywe kileo kupita kiasi?
-