-
Vijana, Chagueni Kumtumikia YehovaMnara wa Mlinzi—2006 | Julai 1
-
-
Leo, Tunajiweka Wakfu kwa Hiari
3, 4. Ni nini kinachoweza kuwasaidia watoto ambao wazazi wao wamejiweka wakfu, wajiweke wakfu kwa hiari?
3 Biblia inaonyesha kwamba Mungu huwaona watoto wadogo kuwa watakatifu hata ikiwa mzazi mmoja tu ndiye Mkristo mwaminifu. (1 Wakorintho 7:14) Je, hilo hufanya watoto hao wawe watumishi wa Yehova waliojiweka wakfu? Hapana. Hata hivyo, watoto wanaolelewa na wazazi ambao wamejiweka wakfu kwa Yehova hupewa mazoezi ambayo yanaweza kuwasaidia wajiweke wakfu kwa Yehova kwa hiari. Mfalme mwenye hekima Sulemani aliandika hivi: “Ee mwanangu, shika amri ya baba yako, wala usiiache sheria ya mama yako. . . . Unapotembea huku na huku, itakuongoza; unapolala, itakulinda; na unapokuwa umeamka, hiyo yenyewe itakuhangaikia. Kwa maana amri hiyo ni taa, na sheria ni nuru, nayo makaripio ya nidhamu ndiyo njia ya uzima.”—Methali 6:20-23.
-
-
Vijana, Chagueni Kumtumikia YehovaMnara wa Mlinzi—2006 | Julai 1
-
-
Kukubali Daraka Lako
12. (a) Ingawa wazazi wanaweza kuwazoeza watoto wao, ni jambo gani ambalo hawawezi kuwafanyia? (b) Ni wakati gani ambapo kijana anakuwa na daraka mbele za Yehova kuhusiana na maamuzi anayofanya?
12 Kuna wakati ambapo vijana hawalindwi tena na uaminifu wa wazazi wao. (1 Wakorintho 7:14) Mwanafunzi Yakobo aliandika hivi: “Ikiwa mtu anajua jinsi ya kufanya yaliyo sawa na bado hayafanyi, hiyo ni dhambi kwake.” (Yakobo 4:17) Wazazi hawawezi kumtumikia Mungu kwa ajili ya watoto wao wala watoto hawawezi kumtumikia Mungu kwa ajili ya wazazi wao. (Ezekieli 18:20) Je, umejifunza kumhusu Yehova na makusudi yake? Je, una umri wa kutosha kuelewa mambo ambayo umejifunza na kuwa na uhusiano pamoja naye? Ikiwa ndivyo, je, si jambo linalopatana na akili kufikiri kwamba Mungu anaona kuwa unaweza kuamua kumtumikia?
-