-
‘Mtihani wa Unyofu wa Upendo Wako’Mnara wa Mlinzi—1989 | Desemba 1
-
-
Je! Wakorintho vilevile wangesukumwa na moyo ‘wawe na wingi katika kutoa kwa fadhili’? Alipokuwa akizuru Korintho mara ya kwanza, Paulo alikuwa amelazimika kujiruzuku mwenyewe akiwa mfanyiza mahema. (Matendo 18:1-3) Aliendelea na mwongozo huu wa kujiruzuku hata kundi lilipokuwa likisitawi huko, akijiepusha kutumia “mamlaka” yake ya kupokea msaada wa kifedha akiwa mweneza-evanjeli wa wakati wote.—1 Wakorintho 9:3-12.
Thomas Scott mwelezaji wa Biblia asema hivi: “Labda yeye alikuwa ameshuhudia mambo fulani katika nia ya Wakristo Wakorintho, ambalo kwanza lilimfanya akatae kupokea riziki yoyote kutoka kwao.” Labda kwa kuongozwa na hali iliyowazunguka ya kufuatia vitu vya kimwili kwa ubinafsi, huenda ikawa Wakorintho hao walikuwa hawana tu nia ya kuwa wakarimu. Huenda pia ikawa Paulo alihofu kwamba Wakorintho hao wenye fikira ya kufuatia ubiashara wangetia shaka juu ya kusudio lake kama angekubali msaada wao wa kifedha. Huenda hata kukawa na wale ambao, kama watu fulani katika Thesalonike, walikuwa wavivu na walitaka kupata udhuru wa kuishi kwa kuwategemea Wakristo wenzao.—2 Wathesalonike 3:7-12.
Vyovyote ilivyokuwa, Paulo na waandamani wake walichagua, kujiruzuku wenyewe, “ili sisi tusizitolee kizuizi chochote zile habari njema ambazo zahusu yule Kristo.” (1 Wakorintho 9:12, NW) Ingawa hivyo, baada ya muda Paulo aliingia katika matatizo makubwa ya kifedha, na habari hizo zikafikia ndugu wale maskini wenye kuishi katika Filipi. Paulo aliwaambia Wakorintho hivi: “Naliwanyang’anya makanisa mengine mali yao, nikitwaa posho langu ili niwahudumia ninyi. Nami nilipokuwa pamoja nanyi na kuhitaji sikumlemea mtu. Maana hao ndugu waliokuja kutoka Makedonia walinipa kadiri ya mahitaji yangu; nami katika mambo yote nalijilinda nafsi yangu nisiwalemee hata kidogo; tena nitajilinda.”—2 Wakorintho 11:8, 9; linganisha Wafilipi 4:15, 16.
-
-
‘Mtihani wa Unyofu wa Upendo Wako’Mnara wa Mlinzi—1989 | Desemba 1
-
-
Lakini hatuhitaji kungojea msiba utukie ndipo tuthibitishe upendo wetu wa kidugu. Mkristo mwenzetu akipatwa na ugumu wa kifedha, twaweza kuwa na wepesi wa hisia ya kujali mahitaji yake, tukifanya mengi kuliko kusema, “Mkaote moto na kushiba.” (Yakobo 2:15, 16) Na namna gani wale walio katika utumishi wa wakati wote ambao ‘hupata riziki kwa ile Injili.’ Kama Paulo, wao hawadai wala hawatarajii usaidizi wa kifedha kutoka kwa wale ambao wao huwatumikia. Hata hivyo, wengi wamesukumwa kuonyesha ukarimu kuelekea wale ambao hufanya kazi ya jasho ili ‘wapande vitu vya kiroho’ kwa ajili yao.—1 Wakorintho 9:11, 14.
-