Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi ya Kufanya Maamuzi Mazuri
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 5. Heshimu dhamiri za watu wengine

      Maamuzi yetu hutofautiana na maamuzi ya watu wengine. Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunaheshimu dhamiri za watu wengine? Fikiria hali mbili zinazofuata:

      Hali ya 1: Dada anayependa kujipamba anahamia kutaniko ambalo dada wengi wanakwazika wanapoona watu wakijipamba.

      Soma Waroma 15:1 na 1 Wakorintho 10:23, 24, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Kulingana na maandiko haya, dada huyo anaweza kuamua kufanya nini? Utafanya nini unaposhughulika na mtu ambaye dhamiri yake inamkataza kufanya jambo ambalo dhamiri yako inakubali?

      Hali ya 2: Ndugu ambaye anajua kwamba Biblia haikatazi kunywa kileo kwa kiasi, lakini anaamua kutokunywa kileo. Anakaribishwa kwenye tafrija ambapo anaona akina ndugu wakinywa kileo.

      Soma Mhubiri 7:16 na Waroma 14:1, 10, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Kulingana na maandiko haya, ndugu huyo anaweza kuamua kufanya nini? Utafanya nini ukimwona mtu anafanya jambo ambalo dhamiri yako inakuzuia kufanya?

      Hatua zinazotusaidia kufanya maamuzi mazuri.

      Mwanamke akisali.

      1. Mwombe Yehova akusaidie kuamua jambo la kufanya.​—Yakobo 1:5.

      Mwanamke huyo akifanya utafiti kwa kutumia Biblia, machapisho yanayotegemea Biblia, na kompyuta.

      2. Fanya utafiti katika Biblia na machapisho yanayotegemea Biblia ili upate kanuni zinazohusika. Unaweza pia kuzungumza na Wakristo wenye uzoefu.

      Mwanamke huyo akifikiria.

      3. Fikiria matokeo ya uamuzi utakaofanya, yaani, jinsi utakavyoathiri dhamiri yako na dhamiri za watu wengine.

  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha—Sehemu ya 1
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 6. Mnaweza kushinda matatizo katika ndoa

      Hakuna ndoa iliyo kamilifu. Kwa hiyo, mume na mke wanapaswa kushirikiana ili kushinda matatizo. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

      VIDEO: Jinsi ya Kuimarisha Kifungo cha Ndoa (5:44)

      • Katika video hiyo, ni mambo gani yanayoonyesha kwamba uhusiano kati ya mume na mke ulianza kudhoofika?

      • Walifanya nini ili kuimarisha ndoa yao?

      Soma 1 Wakorintho 10:24 na Wakolosai 3:13. Baada ya kusoma kila andiko, zungumzieni swali hili:

      • Kufuata ushauri huo kunawezaje kuimarisha ndoa?

      Biblia inasema kwamba tunapaswa kuheshimiana. Kumheshimu mtu kunatia ndani kumtendea kwa njia ya fadhili na staha. Soma Waroma 12:10, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Je, mume au mke anapaswa kutarajia kwamba mwenzi wake ndiye anayepaswa kuwa wa kwanza kuonyesha heshima? Kwa nini?

  • Kwa Nini Mavazi na Mwonekano Wetu Ni Muhimu?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • Sisi sote tunapenda kuchagua mavazi tutakayovaa na jinsi tutakavyojipamba. Kuna kanuni za Biblia zinazoweza kutusaidia kuchagua mavazi na mapambo tunayopenda, na pia yatakayomfurahisha Yehova. Tutazungumzia baadhi ya kanuni hizo katika somo hili.

      1. Tunapaswa kuongozwa na kanuni gani tunapochagua mavazi na mapambo?

      Tunapaswa kuchagua “mavazi yanayofaa, kwa kiasi na utimamu wa akili,” na kudumisha mwonekano safi ambao unaonyesha kwamba ‘tunamtumikia Mungu.’ (1 Timotheo 2:9, 10) Fikiria kanuni hizi nne: (1) Tunapaswa kuvaa “mavazi yanayofaa.” Kama vile ambavyo umejionea katika mikutano ya kutaniko, watu wa Yehova wana mapendezi mbalimbali, lakini mavazi na mitindo yetu ya nywele huonyesha kwamba tunamheshimu Mungu tunayemwabudu. (2) Kuvalia “kwa kiasi” humaanisha kwamba mwonekano wetu haupaswi kuchochea hisia za ngono, wala hatupaswi kujielekezea fikira sana. (3) Tunaonyesha kwamba tuna “utimamu wa akili” kwa kuepuka kufuata kila mtindo wa mavazi au mapambo yanayopendwa na wengi. (4) Sikuzote mwonekano wetu unapaswa kuonyesha kwamba ‘tunamtumikia Mungu,’ ili iwe rahisi kwa wengine kuona kwamba tunamwabudu Mungu wa kweli.​—1 Wakorintho 10:31.

      2. Kwa nini tunapaswa kuwafikiria waabudu wenzetu tunapochagua mavazi?

      Ingawa tuna uhuru wa kuchagua mavazi tutakayovaa, tunapaswa kufikiria jinsi mwonekano wetu utakavyowaathiri wengine. Tunajitahidi sana kuepuka kumkwaza mtu yeyote. Badala yake, ‘tunampendeza jirani yetu kwa mema ili kumjenga.’​—Soma Waroma 15:1, 2.

      3. Mwonekano wetu unawezaje kuwavutia watu kwenye ibada ya kweli?

      Ingawa tunajitahidi kuvalia kwa njia inayofaa pindi zote, tunajitahidi hasa kuvalia vizuri tunapohudhuria mikutano ya kutaniko na tunaposhiriki katika huduma. Hatungependa kuwakengeusha watu wasikazie fikira ujumbe muhimu tunaowapelekea. Badala yake, mwonekano wetu unaweza kuwavutia watu kujifunza kweli na ‘kulipamba fundisho la Mwokozi wetu.’​—Tito 2:10.

      CHIMBA ZAIDI

      Chunguza jinsi tunavyoweza kuhakikisha kwamba mavazi na mwonekano wetu unawasaidia wengine watambue sisi ni Wakristo.

      Wanaume wawili wakiwa wamesimama mbele ya hakimu. Mwanamume mmoja amevalia suti, na mwingine amevaa mavazi yaliyochanika na kofia.

      Mwonekano wetu unaweza kuonyesha kwamba tunawaheshimu watu wenye mamlaka. Ingawa Yehova huona jinsi tulivyo moyoni, mwonekano wetu pia unapaswa kumheshimu

      4. Mwonekano wetu mzuri unamheshimu Yehova

      Ni sababu gani muhimu zaidi inayofanya tufikirie kwa makini mwonekano wetu? Soma Zaburi 47:2, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Kwa kuwa tunamwakilisha Yehova, tunapaswa kuvalia kwa njia gani?

      • Je, unafikiri mwonekano wetu ni muhimu tunapohudhuria mikutano na tunaposhiriki katika huduma? Kwa nini?

      5. Jinsi ya kufanya maamuzi mazuri kuhusu mavazi na mapambo

      Onyesha VIDEO.

      VIDEO: “Fanyeni Mambo Yote kwa Utukufu wa Mungu” (10:18)

      Iwe mavazi yetu ni ya bei ghali au bei rahisi, yanapaswa kuwa safi na yanayofaa hali hususa. Soma 1 Wakorintho 10:24 na 1 Timotheo 2:9, 10. Kisha mzungumzie kwa nini tunapaswa kuepuka kuvaa . . .

      • mavazi yasiyo safi na yasiyo nadhifu.

      • mavazi yanayobana sana, yanayoonyesha sehemu za mwili, au yanayochochea hisia za ngono.

      Ingawa Wakristo hawako chini ya Sheria ya Musa, Sheria hiyo inatusaidia kujua maoni ya Yehova. Soma Kumbukumbu la Torati 22:5, kisha mzungumzie swali hili:

      • Kwa nini tunapaswa kuepuka kuvaa na kujipamba kwa njia inayofanya mwanamume aonekane kama mwanamke au mwanamke kuonekana kama mwanamume?

      Soma 1 Wakorintho 10:32, 33 na 1 Yohana 2:15, 16, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Kwa nini tunapaswa kuepuka mwonekano unaoweza kuwaudhi wengine katika eneo tunaloishi au kutanikoni?

      • Ni mitindo gani ya mavazi na mapambo inayopendwa katika eneo unaloishi?

      • Je, unafikiri baadhi ya mitindo hiyo huenda isimfae Mkristo? Kwa nini?

      Tunaweza kuvaa na kujipamba kwa njia mbalimbali na bado tukamfurahisha Yehova

      Wanaume na wanawake wenye umri mbalimbali kutoka katika jamii na mataifa mbalimbali walio na mavazi na mitindo tofauti-tofauti ya nywele inayowafaa Wakristo.

      WATU FULANI HUSEMA: “Nina haki ya kuvaa kwa njia yoyote ninayotaka.”

      • Je, unakubaliana na maoni hayo? Kwa nini?

      MUHTASARI

      Tunapofanya maamuzi mazuri kuhusu mwonekano wetu, tunaonyesha kwamba tunamheshimu Yehova na watu wengine.

      Ungejibuje?

      • Kwa nini jinsi tunavyovalia na kujipamba ni muhimu kwa Yehova?

      • Ni kanuni gani zinazopaswa kutuongoza tunapofanya maamuzi kuhusu mwonekano wetu?

      • Mwonekano wetu unawezaje kuathiri maoni ya wengine kuhusu ibada ya kweli?

      Lengo

      CHUNGUZA ZAIDI

      Chunguza jinsi mavazi yako yanavyoweza kuathiri maoni ya wengine kukuhusu.

      “Mwonekano Wangu Unanitambulishaje?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

      Jifunze kwa nini ni jambo la hekima kufikiria kwa makini kabla ya kuamua kujichanja chale, yaani, kuchora tattoo mwilini.

      “Biblia Inasema Nini Kuhusu Kujichanja Chale?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

      Chunguza kanuni nyingine zinazopaswa kuongoza maamuzi yetu.

      “Je, Mtindo Wako wa Mavazi Unamtukuza Mungu?” (Mnara wa Mlinzi, Septemba 2016)

      Mwanamke fulani aliyetaka kumfurahisha Mungu alijifunza jinsi gani kuheshimu maoni ya wengine kuhusu mavazi?

      “Mavazi na Mapambo Yalinizuia Kufanya Maendeleo” (Amkeni!, Desemba 22, 2003)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki