-
DhamiriUfahamu wa Kina wa Maandiko
-
-
Kujali Dhamiri za Wengine. Kwa vile dhamiri inahitaji kuzoezwa kikamili na kwa usahihi kupitia Neno la Mungu ili iweze kufanya maamuzi yanayofaa, dhamiri ambayo haijazoezwa inaweza kuwa dhaifu. Yaani, bila kutumia hekima mtu anaweza kuinyamazisha kwa urahisi, au anaweza kukasirishwa na matendo au maneno ya wengine, hata wakati ambapo wengine hawajakosea. Paulo alitoa mfano wa jambo hilo kuhusu kula, kunywa, na kuhukumu siku fulani kuwa muhimu kuliko nyingine. (Ro 14:1-23; 1Ko 8:1-13) Mkristo aliye na ujuzi na ambaye dhamiri yake imezoezwa anaamriwa amfikirie na kumjali yule aliye na dhamiri dhaifu, asitumie uhuru wake wote au kusisitiza kupata “haki” zake zote au sikuzote kufanya anachopenda. (Ro 15:1) Anayeiumiza dhamiri dhaifu ya Mkristo mwenzake ‘anamtendea dhambi Kristo.’ (1Ko 8:12) Kwa upande mwingine, Paulo anadokeza kwamba ingawa hangetaka kufanya jambo ambalo litamkasirisha ndugu aliye dhaifu, na hivyo kusababisha ndugu huyo amhukumu, huyo aliye dhaifu anapaswa vilevile kumfikiria ndugu yake, ajitahidi kufikia ukomavu kwa kupata ujuzi zaidi na kuizoeza dhamiri yake ili asikasirishwe kwa urahisi na kuwa na maoni mabaya kuwahusu wengine.—1Ko 10:29, 30; Ro 14:10.
-
-
“Kweli Itawaweka Ninyi Huru”Mnara wa Mlinzi—2004 | Machi 1
-
-
Mtume Paulo alifurahia uhuru aliopata kupitia Kristo lakini hakutumia uhuru wake kujipendeza au kuwaumiza wengine. Katika barua yake kwa kutaniko la Korintho, alionyesha kwamba hangeumiza dhamiri ya mtu mwingine kwa kufanya jambo ambalo alikuwa na uhuru wa Kimaandiko kulifanya lakini ambalo lingemsumbua mtu asiye na ujuzi wa kutosha, ambaye labda dhamiri yake ingeumizwa na tendo la Paulo. Anataja mfano wa kula nyama iliyotolewa kwa sanamu kabla haijapelekwa sokoni kuuzwa. Kula nyama hiyo kungemfanya mtu aliye na dhamiri dhaifu achambue uhuru wa Paulo wa kuila na hivyo mtu huyo angekuwa kama hakimu wa Paulo, jambo ambalo halingefaa. Kwa hiyo, Paulo alisema: “Kwa nini iwe kwamba uhuru wangu unahukumiwa na dhamiri ya mtu mwingine? Ikiwa nakula nikiwa na shukrani, kwa nini nitukanwe juu ya kile ninachotolea shukrani?” Hata hivyo, mtume huyo aliazimia kutumia uhuru wake kwa njia inayojenga na isiyodhuru.—1 Wakorintho 10:23-33.
-