Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Kufahamu Sisi Ni Nini Wakati wa Ukumbusho’
    Mnara wa Mlinzi—1990 | Februari 15
    • ‘Kufahamu Sisi Ni Nini Wakati wa Ukumbusho’

      “Kama sisi tungefahamu sisi wenyewe ni nini, hatungehukumiwa . . . ili kwamba tusipate kuwa wenye kulaaniwa vikali.”—1 WAKORINTHO 11:31, 32, NW.

      1. Wakristo wa kweli wataka kuepuka nini kwa uhakika, na kwa nini?

      MKRISTO hataki kamwe kamwe kuhukumiwa vibaya na Yehova. Kutopendeza “Hakimu wa dunia yote” kungeweza kuongoza kwenye ‘kulaaniwa vikali pamoja na ulimwengu’ na kupoteza wokovu. Ndivyo ilivyo tuwe twatumainia uhai mbinguni pamoja na Yesu au uhai usio na mwisho katika paradiso ya kidunia.—Mwanzo 18:25; 1 Wakorintho 11:32, NW.

      2, 3. Tungeweza kuhukumiwa vibaya katika jambo gani, na Paulo alisema nini juu ya hili?

      2 Katika 1 Wakorintho sura ya 11, mtume Paulo alinena juu ya eneo moja ambamo tungeweza kuja hukumuni. Ingawa alielekeza maelezo yake kwa Wakristo wapakwa-mafuta, shauri lake ni la maana kwa wote, hasa katika majira haya. Kufahamu sisi wenyewe ni nani kwaweza kutusaidia tupate kibali cha Mungu tusihukumiwe. Katika kuzungumza juu ya mwadhimisho wa kila mwaka wa Mlo wa Jioni wa Bwana, Paulo aliandika hivi:

  • ‘Kufahamu Sisi Ni Nini Wakati wa Ukumbusho’
    Mnara wa Mlinzi—1990 | Februari 15
    • 17, 18. (a) Wakristo fulani katika Korintho walitumbukia katika zoea gani? (b) Kwa nini ulaji na unywaji wa kupindukia ulikuwa jambo zito sana? (Waebrania 10:28-31)

      17 Paulo alitokeza jambo hili katika barua yake kwa Wakorintho wakati ambapo mitume fulani walikuwa wangali hai na wakati Mungu alipokuwa akiita Wakristo “ili wawe watakatifu.” Paulo alisema kwamba zoea baya lilikuwa limesitawi miongoni mwa wale waliowajibika kushiriki mifano. Baadhi yao walikula milo yao mapema na hapo wakala au wakanywa kupita kiasi, hiyo ikiwafanya wasinzie, waduwazwe katika hisi zao. Tokeo ni kwamba, hawakuweza “kufahamu mwili,” mwili wa Yesu wa kiasili wenye kuwakilishwa na mkate. Je! hilo lilikuwa jambo zito sana? Ndiyo! Kwa kushiriki bila ustahiki, wakawa “wenye hatia mintarafu ya mwili na damu ya Bwana.” Kama wangekuwa chonjo kiakili na kiroho, ‘wangeweza kufahamu walikuwa nini na hawangehukumiwa.’—1 Wakorintho 1:2; 11:20-22, 27-31, NW.

      18 Wakristo hao walihitaji kufahamu nini na jinsi gani? Kwanza hasa, iliwalazimu kuthamini katika moyo na akili wito wao wa kuwa miongoni mwa warithi 144,000 wa uhai wa kimbingu. Walifahamuje hivyo, na je! yapasa wengi leo waitikadi kwamba wao ni sehemu ya kikundi kidogo hiki ambacho Mungu amekuwa akikichagua tangu siku ya mitume?

      19. Ni hali gani yenye kufunua iliyoenea sana wakati wa Ukumbusho wa 1989?

      19 Kwa kweli, ni hesabu ndogo sana ya Wakristo wa kweli leo ambao hufahamu hivyo kuhusu wao wenyewe. Kwenye mwadhimisho wa Mlo wa Jioni wa Bwana katika 1989, zaidi ya 9,479,000 walikusanyika katika makundi ya Mashahidi wa Yehova kuzunguka dunia. Wapata 8,700 walidai kuwa na tumaini la ‘kuokolewa kwa ajili ya ufalme wa kimbingu.’ (2 Timotheo 4:18, NW) Walio wengi zaidi—ndiyo, mamilioni ya Wakristo wengine wabarikiwa walio waaminifu-washikamanifu ambao walikusanyika—walifahamu kwamba tumaini lao halali ni kuishi milele duniani.

      20. Wale wa 144,000 hujuaje kwamba wameitwa? (1 Yohana 2:27)

      20 Kwenye Pentekoste 33 W.K., Mungu alianza kuchagua 144,000 kwa ajili ya uhai wa kimbingu. Kwa kuwa tumaini hili lilikuwa jipya, lisiloshikwa na watumishi wa Mungu kabla ya wakati wa Yesu, wale wenye kuchaguliwa wangejuaje au wangehakikishiwaje juu ya tumaini hili? Wao hufahamu hivi kwa kupokea ushahidi wa tumaini hilo ambao hutolewa na roho takatifu ya Mungu. Hiyo haimaanishi kwamba wao huiona kikweli roho hiyo (hiyo si mtu) wala kwamba wao huwa na mwono fulani wa kiakili wa roho ikiwasiliana nao, wala hawasikii sauti zenye kutoka kwenye makao ya roho. Paulo aeleza hivi: “Roho yenyewe hutoa ushahidi pamoja na roho yetu kwamba sisi ni watoto wa Mungu . . . Sisi pia ni warithi: warithi kweli kweli wa Mungu, lakini warithi-shirika pamoja na Kristo, mradi sisi twateseka pamoja ili kwamba sisi pia tupate kutukuzwa pamoja.”—Warumi 8:16, 17, NW.

      21. (a) Wapakwa-mafuta hujuaje kwamba wana tumaini la kimbingu? (1 Wakorintho 10:15-17) (b) Wapakwa-mafuta mmoja mmoja ni watu wa aina gani, nao hushuhudiaje tumaini lao wakiwa na kiasi?

      21 Ushahidi, au ung’amuzi huu, huelekeza upya fikira na tumaini lao. Wangali ni wanadamu, wenye kuonea shangwe vitu vyema vya uumbaji wa kidunia wa Yehova, hata hivyo mwelekezo mkuu wa maisha na mahangaikio yao ni juu ya kuwa warithi-shirika pamoja na Kristo. Hawakufikia kuwa na mtazamio huu kwa mhemko tu. Wao mmoja mmoja ni watu wenye fikira za mtu timamu, wakiwa na usawaziko katika maoni na mwenendo wao. Ingawa hivyo, kwa kutakaswa na roho ya Mungu wana usadikisho kuhusu wito wao, bila kuwa na shaka yenye kung’ang’ania juu ya wito huo. Wao wang’amua kwamba wokovu wao utakuwa wa kwenda mbinguni wakithibitika kuwa wenye imani. (2 Wathesalonike 2:13; 2 Timotheo 2:10-12) Kwa kuelewa dhabihu ya Yesu yamaanisha nini kwao na kufahamu kwamba ni Wakristo wapakwa mafuta kwa roho, wao hushiriki mifano ya Ukumbusho wakiwa na moyo wa kiasi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki