-
Njia ya Upendo Haishindwi KamweMnara wa Mlinzi—1999 | Februari 15
-
-
4. Biblia huandaa ufahamu gani wenye kina kuhusu wivu?
4 Baada ya maelezo yake ya kwanza kuhusu upendo, Paulo aliwaandikia Wakorintho hivi: “Upendo hauna wivu.” (1 Wakorintho 13:4) Wivu waweza kujidhihirisha kwa kutoridhika na ufanisi au utimizo mbalimbali wa wengine kwa kuwa mwenye husuda. Wivu huo ni wenye kuharibu—kimwili, kihisia-moyo, na kiroho.—Mithali 14:30; Waroma 13:13; Yakobo 3:14-16.
5. Upendo waweza kutusaidiaje kushinda wivu inapoonekana kuwa tu umepuuzwa kwa kutopewa pendeleo fulani la kitheokrasi?
5 Kwa kuzingatia hilo, jiulize, ‘Je, mimi ninakuwa mwenye husuda inapoonekana kuwa nimepuuzwa kwa kutopewa pendeleo fulani la kitheokrasi?’ Ikiwa jibu ni ndiyo, usikate tamaa. Mwandikaji wa Biblia Yakobo atukumbusha kwamba wanadamu wote wasio wakamilifu wana “mwelekeo wa kuhusudu.” (Yakobo 4:5) Kumpenda ndugu yako kwaweza kukusaidia kupata tena usawaziko wako. Kwaweza kukusaidia ushangilie na wale wanaoshangilia na kutoona kana kwamba umefedheheshwa mtu fulani anapopata kibali au sifa.—Linganisha 1 Samweli 18:7-9.
6. Ni hali gani mbaya iliyotokea katika kutaniko la Korintho la karne ya kwanza?
6 Paulo aongeza kusema kwamba upendo “haujigambi, haujitutumui.” (1 Wakorintho 13:4) Ikiwa tuna kipawa au uwezo fulani, hakuna haja ya kuuonyesha kwa majivuno. Kwa wazi, hili lilikuwa tatizo la wanaume fulani waliotamani makuu, ambao walipenyeza ndani ya kutaniko la Korintho la kale. Huenda ikawa kwamba walikuwa na uwezo mbalimbali uliopita wa wengine katika kueleza mawazo, au walifanya mambo kwa ustadi zaidi. Kuvuta uangalifu kwao wenyewe huenda kukawa kulichangia kugawanyika kwa kutaniko katika vikundi kadhaa. (1 Wakorintho 3:3, 4; 2 Wakorintho 12:20) Hali hiyo ikawa mbaya sana hivi kwamba baadaye ilimbidi Paulo awatie Wakorintho adabu kwa sababu ya ‘kuchukuliana na watu wenye kukosa akili,’ ambao Paulo aliwafafanua kwa kuwachambua kuwa ‘mitume walio bora sana.’—2 Wakorintho 11:5, 19, 20.
7, 8. Onyesha kutoka katika Biblia jinsi tuwezavyo kutumia vipawa vya kiasili tulivyo navyo kuendeleza muungano.
7 Hali sawa na hiyo yaweza kutokea leo. Kwa kielelezo, watu wengine wanaweza kuwa na mwelekeo wa kujisifia matimizo yao katika huduma au mapendeleo yao katika tengenezo la Mungu. Hata ikiwa tuna ustadi au uwezo fulani wa pekee ambao wengine katika kutaniko hawana, je, hilo lingekuwa sababu ya kutufanya tujitutumue? Kwa vyovyote, yatupasa kutumia vipawa vya kiasili tulivyo navyo ili kuendeleza muungano—bali si kujiendeleza wenyewe.—Mathayo 23:12; 1 Petro 5:6.
8 Paulo aliandika kwamba ingawa kutaniko lina viungo vingi, “Mungu aliuungamanisha mwili.” (1 Wakorintho 12:19-26) Neno la Kigiriki linalotafsiriwa ‘kuungamanisha’ lamaanisha kuchanganya kwa upatanifu kama vile kuchanganya rangi mbalimbali. Kwa hiyo, hakuna mtu yeyote katika kutaniko anayepaswa kujitutumua kuhusu uwezo wake mbalimbali na kujaribu kutawala wengine. Kiburi na kutaka makuu haziruhusiwi katika tengenezo la Mungu.—Mithali 16:19; 1 Wakorintho 14:12; 1 Petro 5:2, 3.
-
-
Njia ya Upendo Haishindwi KamweMnara wa Mlinzi—1999 | Februari 15
-
-
11. (a) Twaweza kuonyesha upendo wenye fadhili na wenye adabu kwa njia zipi? (b) Twaweza kuonyeshaje kwamba hatushangilii ukosefu wa uadilifu?
11 Paulo pia aliandika kwamba upendo ni “wenye fadhili” na kwamba “haujiendeshi bila adabu.” (1 Wakorintho 13:4, 5) Naam, upendo hautaturuhusu tutende kwa njia ya ufidhuli, isiyo na adabu, au isiyo na staha. Badala yake, tutafikiria hisia za wengine. Kwa kielelezo, mtu mwenye upendo ataepuka kufanya mambo ambayo yangesumbua dhamiri za wengine. (Linganisha 1 Wakorintho 8:13.) Upendo “haushangilii ukosefu wa uadilifu, bali hushangilia pamoja na kweli.” (1 Wakorintho 13:6) Ikiwa tunapenda sheria ya Yehova, hatutauchukua kivivi hivi ukosefu wa adili au kupendezwa na mambo ambayo Mungu huchukia. (Zaburi 119:97) Upendo utatusaidia kupata shangwe katika mambo yajengayo badala ya kubomoa.—Waroma 15:2; 1 Wakorintho 10:23, 24; 14:26.
-
-
Njia ya Upendo Haishindwi KamweMnara wa Mlinzi—1999 | Februari 15
-
-
16. Ni katika hali zipi upendo waweza kutusaidia tuwe wenye kustahimili?
16 Kisha Paulo atuambia kwamba “upendo ni wenye ustahimilivu.” (1 Wakorintho 13:4) Hutuwezesha kustahimili hali zenye majaribu, labda zenye kuendelea kwa muda mrefu. Kwa kielelezo, Wakristo wengi wameishi kwa miaka mingi katika nyumba iliyogawanyika kidini. Wengine ni waseja, si kwa kuchagua kuwa hivyo, bali kwa sababu wameshindwa kupata mwenzi anayefaa “katika Bwana.” (1 Wakorintho 7:39; 2 Wakorintho 6:14) Kisha kuna wale wanaopambana na matatizo ya kiafya yenye kudhoofisha. (Wagalatia 4:13, 14; Wafilipi 2:25-30) Kwa kweli, katika mfumo huu usio mkamilifu, hakuna yeyote anayeishi maisha yasiyohitaji uvumilivu wa aina fulani.—Mathayo 10:22; Yakobo 1:12.
-