-
Sitawisha Upendo Ambao Haushindwi KamweMnara wa Mlinzi—2009 | Desemba 15
-
-
13. (a) Ni andiko gani litakalokuwa andiko la mwaka wa 2010? (b) Upendo haushindwi kamwe katika maana gani?
13 Kisha, Paulo anatueleza kile ambacho upendo unamaanisha na kile ambacho haumaanishi. (Soma 1 Wakorintho 13:4-8.) Sasa, chunguza ikiwa unatimiza yale ambayo upendo unamaanisha. Kazia fikira hasa sentensi ya mwisho ya mstari wa 7 na sentensi ya kwanza ya mstari wa 8: ‘Upendo huvumilia mambo yote. Upendo haushindwi kamwe.’ Hilo ndilo andiko letu la mwaka wa 2010. Ona kwamba katika mstari wa 8, Paulo alisema kwamba zawadi za roho, kutia ndani kutoa unabii na kusema kwa lugha, zawadi ambazo zilitumiwa mwanzoni mwa kutaniko la Kikristo, zingeondolewa mbali. Zingekoma. Lakini upendo utakuwepo sikuzote. Yehova ndiye chanzo cha upendo, naye anaishi milele. Hivyo, upendo hautashindwa kamwe, au kukoma. Utaendelea kuwepo milele ukiwa sifa ya Mungu wetu anayeishi milele.—1 Yoh. 4:8.
-
-
Sitawisha Upendo Ambao Haushindwi KamweMnara wa Mlinzi—2009 | Desemba 15
-
-
Upendo Haushindwi Kamwe
20, 21. (a) Kwa nini upendo ni wenye thamani bora zaidi? (b) Kwa nini umeazimia kufuatia ile njia ya upendo?
20 Watu wa Yehova leo wanaonyesha kwamba ni jambo la hekima kufuatia ile njia iliyo bora zaidi ya upendo. Kwa kweli, njia hiyo inashinda hali yoyote ile. Ona jinsi mtume Paulo alivyokazia ukweli huo. Kwanza, alitaja kwamba zawadi za roho zingepitilia mbali na kwamba kutaniko la Kikristo lingekua na kufikia ukomavu. Kisha, akakata kauli hivi: “Sasa, hata hivyo, inabaki imani, tumaini, upendo, hayo matatu; lakini lililo kubwa zaidi kati ya hayo ni upendo.”—1 Kor. 13:13.
21 Mwishowe, mambo ambayo tunaamini yatakuwa halisi, na hivyo hatutahitaji tena kuonyesha imani katika mambo hayo. Tumaini katika ahadi ambazo tunatamani sana kuona zikitimizwa halitahitajiwa tena baada ya mambo yote kuwa mapya. Lakini namna gani upendo? Upendo hautashindwa kamwe, au kukoma. Utabaki. Huku tukitazamia kuishi milele, bila shaka tutaona na kuelewa zaidi sehemu mbalimbali za upendo wa Mungu. Ukifanya mapenzi ya Mungu kwa kuendelea kufuatia ile njia iliyo bora zaidi ya upendo ambayo haishindwi kamwe, huenda utadumu milele.—1 Yoh. 2:17.
-