-
Kusali Mbele ya Wengine Kwa Moyo MnyenyekevuMnara wa Mlinzi—1986 | Mei 15
-
-
Paulo aligusia kanuni nyingine ya maana alipoandika hivi: “Nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda. . . . Wewe ukibariki [ukisifu, NW ] kwa roho, yeye aketiye katika mahali pa mjinga ataitikiaje, Amina, baada ya kushukuru kwako, akiwa hayajui usemayo? ” (1 Wakorintho 14:14-16) Katika siku za Paulo Wakristo fulani walipokea kipawa cha kimuujiza cha kusema lugha mbalimbali, na kwa wazi wengine kati yao walisali kwa kutumia lugha hizo mbele ya kundi. Lakini kama vile Paulo alivyoonyesha, wale wengine kundini hawakuwaelewa.
Leo, sisi hatuna kipawa hicho cha kimuujiza. Lakini Wakristo wanaosali kwa ajili ya wengine wanapaswa kusali kwa njia itakayoeleweka. Kwa mfano, mwanzoni mwa hotuba ya watu wote, tunakaribisha watu wa kutoka nje wajiunge nasi katika sala. Katika sala ya namna hiyo, hakika lingekuwa jambo la akili kuepuka maneno au habari ambayo ingekuwa ngumu kueleweka na wageni.
-
-
Kusali Mbele ya Wengine Kwa Moyo MnyenyekevuMnara wa Mlinzi—1986 | Mei 15
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 22]
Je, inafaa wasikilizaji waseme “Amin” kwa sauti yenye kusikika mwishoni mwa sala inayotolewa mbele ya watu?
Ndiyo, ikiwa wanataka au wanajisikia wakisukumwa na moyo kufanya hivyo. Paulo aliitaja “Amina” inayosemwa na wale wanosikiliza sala, ingawa hakusema wazi kama waliitoa kwa sauti yenye kusikika, au kwa unyamavu katika mioyo yao. (1 Wakorintho 14:16) Lakini, chini ya Torati ya Musa, kulikuwa na pindi moja ambapo Waisraeli waliagizwa waziwazi waseme “Amina” kwa sauti kubwa. (Kumbukumbu la Torati 27:14-26) Kwa hiyo, wakati mtu mwenye kusali anapoonyesha sala yake imefikia mwisho kwa kusema “Amina,” inafaa wasikilizaji waseme “Amina” katika mioyo yao au kwa sauti ya chini yenye kusikika. Inawapasa wazazi wazoeze watoto wao kuonyesha uthamini unaofaa katika njia ambayo wanaitamka “Amina” yo yote ya sauti ya chini.
-