-
Inamaanisha Nini Kuwa Mtu wa Kiroho?Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Februari
-
-
MTU WA KIROHO NI NANI?
3. Ufafanuzi wa Biblia kuhusu mtu wa kimwili unatofautianaje na ule wa mtu wa kiroho?
3 Mtume Paulo anatusaidia kuelewa mtu wa kiroho ni nani kwa kuonyesha tofauti kati ya “mtu wa kiroho” na “mtu wa kimwili.” (Soma 1 Wakorintho 2:14-16.) Wanatofautianaje? “Mtu wa kimwili” anaelezwa kuwa mtu asiyekubali “mambo ya roho ya Mungu, kwa maana hayo ni upumbavu kwake; naye hawezi kuyajua.” Kwa upande mwingine, “mtu wa kiroho” ni mtu ambaye “huchunguza mambo yote” na ana “akili ya Kristo.” Paulo anatutia moyo tuwe watu wa kiroho. Watu wa kimwili na wa kiroho wanatofautiana katika njia gani nyingine?
-
-
Inamaanisha Nini Kuwa Mtu wa Kiroho?Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Februari
-
-
6. Ni nini kinachomtambulisha mtu wa kiroho?
6 Hivyo basi, inamaanisha nini kuwa “mtu wa kiroho”? Tofauti kabisa na mtu wa kimwili, mtu wa kiroho ana mwelekeo wa kuhangaikia uhusiano wake pamoja na Mungu. Watu walio na mtazamo wa kiroho hujitahidi kuwa “waigaji wa Mungu.” (Efe. 5:1) Hilo linamaanisha kwamba wanajitahidi kuwa na maoni kama ya Yehova kuhusu mambo, na kuyaona kama Yehova anavyoyaona. Wanamwona Mungu akiwa halisi sana. Tofauti kabisa na watu walio na mtazamo wa kimwili, watu wa kiroho hujitahidi kuhakikisha kwamba kila jambo wanalofanya maishani mwao linapatana na viwango vya Yehova. (Zab. 119:33; 143:10) Badala ya kukazia matendo ya mwili, mtu mwenye mtazamo wa kiroho hujitahidi kuonyesha “tunda la roho.” (Gal. 5:22, 23) Ili kufafanua zaidi maana ya kuwa na “mtazamo wa kiroho,” fikiria mfano huu: Mtu ambaye ni stadi katika mambo ya kibiashara husemwa kuwa ana mtazamo au akili ya biashara. Vivyo hivyo, mtu ambaye huchukua kwa uzito mambo ya kiroho au ya kidini husemwa kuwa ana mtazamo wa kiroho.
7. Biblia inasema nini kuhusu watu walio na mtazamo wa kiroho?
7 Biblia inawasifu watu walio na mtazamo wa kiroho. Andiko la Mathayo 5:3 linasema hivi: “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho, kwa kuwa Ufalme wa mbinguni ni wao.” Andiko la Waroma 8:6 linaonyesha manufaa ya kuwa na mtazamo wa kiroho linaposema hivi: “Kukaza akili kwenye mwili humaanisha kifo, lakini kukaza akili kwenye roho humaanisha uzima na amani.” Tunapokazia mambo ya kiroho, tunakuwa na amani pamoja na Mungu, tunapata amani ya akili, na tumaini la uzima wa milele.
-