-
Ufufuo wa Yesu Humaanisha Uzima!Mnara wa Mlinzi—2013 | Machi 1
-
-
UFUFUO wa Yesu sio tukio la zamani tu, lisilo na umuhimu wowote kwetu leo. Mtume Paulo alionyesha umuhimu wake alipoandika hivi: “Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, matunda ya kwanza ya wale ambao wamelala usingizi katika kifo. Kwa kuwa kifo ni kupitia mwanadamu, ufufuo wa wafu pia ni kupitia mwanadamu. Kwa maana kama vile katika Adamu wote wanakufa, vivyo hivyo pia katika Kristo wote watafanywa kuwa hai.”—1 Wakorintho 15:20-22.
-
-
Ufufuo wa Yesu Humaanisha Uzima!Mnara wa Mlinzi—2013 | Machi 1
-
-
Maneno yanayofuata ya Paulo yanaeleza jambo ambalo limewezekana kwa sababu ya ufufuo wa Yesu. Paulo alisema: “Kwa kuwa kifo ni kupitia mwanadamu ufufuo wa wafu pia ni kupitia mwanadamu.” Sote tunakufa kwa sababu tulirithi dhambi na kutokamilika kutoka kwa Adamu. Hata hivyo, kwa kutoa mwili wake mkamilifu wa kibinadamu kuwa dhabihu, Yesu alifanya iwezekane kwa wanadamu kukombolewa kutoka kwenye utumwa wa dhambi na kifo kupitia ufufuo. Akihitimisha hoja yake vizuri, Paulo aliandika hivi kwenye Waroma 6:23: “Mshahara ambao dhambi hulipa ni kifo, lakini zawadi ambayo Mungu hutoa ni uzima wa milele kupitia Kristo Yesu Bwana wetu.”
-