-
“Nina Tumaini kwa Mungu”Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Desemba
-
-
15. Kwa nini Yesu anaitwa “matunda ya kwanza”?
15 Yesu ndiye wa kwanza kufufuliwa akiwa kiumbe wa roho, na bila shaka ufufuo wake ndio muhimu zaidi. (Mdo. 26:23) Lakini si yeye tu aliyeahidiwa kufufuliwa na kwenda mbinguni akiwa kiumbe wa roho. Yesu aliwahakikishia mitume wake waaminifu kwamba wangetawala pamoja naye mbinguni. (Luka 22:28-30) Ili wapokee thawabu hiyo, ni lazima wangekufa kwanza. Baadaye, kama Kristo, wangefufuliwa wakiwa na miili ya roho. Paulo aliandika kwamba “Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, matunda ya kwanza ya wale ambao wamelala usingizi katika kifo.” Paulo alionyesha kwamba wengine pia wangefufuliwa na kwenda kuishi mbinguni aliposema hivi: “Lakini kila mmoja katika daraja lake mwenyewe: Kristo aliye matunda ya kwanza, baadaye wale walio wa Kristo wakati wa kuwapo kwake.”—1 Kor. 15:20, 23.
16. Ni nini kinachoweza kutusaidia kujua wakati ambapo ufufuo wa mbinguni ungetukia?
16 Kwa ujumla, maneno hayo ya Paulo yanatusaidia kujua wakati ambapo ufufuo wa mbinguni ungetukia. Ungetukia “wakati wa kuwapo kwake.” Kwa muda mrefu, Mashahidi wa Yehova wamethibitisha kupitia Maandiko kwamba tangu mwaka wa 1914 tumekuwa tukiishi wakati wa “kuwapo” kwa Yesu kulikoahidiwa. Tungali tunaishi katika kipindi hicho, na sasa mwisho wa mfumo huu mwovu wa mambo umekaribia sana.
17, 18. Ni nini kitakachowapata baadhi ya watiwa mafuta wakati wa kuwapo kwa Kristo?
17 Biblia inatupatia habari zaidi kuhusu ufufuo wa mbinguni: “Hatutaki mkose kujua kuhusu wale walalao usingizi katika kifo . . . Kwa maana ikiwa imani yetu ni kwamba Yesu alikufa na kufufuliwa tena, vivyo hivyo pia, wale ambao wamelala usingizi katika kifo kupitia Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye . . . Sisi tulio hai ambao tutabaki mpaka kuwapo kwa Bwana hatutawatangulia kwa vyovyote wale ambao wamelala usingizi katika kifo; kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni akiwa na mwito wenye amri, . . . na wale walio wafu katika muungano na Kristo watafufuliwa kwanza. Baadaye sisi tulio hai tuliobaki tutanyakuliwa, pamoja nao, katika mawingu ili kukutana na Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana sikuzote.”—1 The. 4:13-17.
18 Ufufuo wa kwanza ungetukia wakati fulani baada ya kuanza kwa “kuwapo” kwa Kristo. Watiwa mafuta watakaokuwa hai wakati wa dhiki kuu ‘watanyakuliwa katika mawingu.’ (Mt. 24:31) Wale ‘watakaonyakuliwa hawatalala usingizi katika kifo,’ katika maana ya kwamba hawatalala katika usingizi wa kifo kwa muda mrefu. ‘Wote watabadilishwa, kwa muda mfupi, kufumba na kufumbua jicho, wakati wa tarumbeta ya mwisho.’—1 Kor. 15:51, 52.
-
-
“Nina Tumaini kwa Mungu”Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Desemba
-
-
20. Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba ufufuo utatukia kwa mpangilio?
20 Biblia inaposema kuhusu wale watakaofufuliwa ili wakaishi mbinguni, inasema kwamba watafufuliwa “kila mmoja katika daraja lake mwenyewe.” (1 Kor. 15:23) Vivyo hivyo, tunaweza kuwa na uhakika kwamba wale watakaofufuliwa ili waishi duniani watafufuliwa kwa mpangilio unaofaa. Hilo ni tumaini linalosisimua sana. Je, wale waliokufa karibuni watafufuliwa mwanzoni mwa Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo na kukaribishwa na wapendwa wao wanaowafahamu? Je, wanaume waaminifu wa zamani na wenye uwezo wa kuongoza mambo watafufuliwa mapema ili wasaidie kusimamia watu wa Mungu katika ulimwengu mpya? Vipi kuhusu watu ambao hawakumtumikia Yehova? Watafufuliwa lini, na wapi? Tunaweza kujiuliza maswali mengi. Lakini je, kweli mambo hayo yanapaswa kutuhangaisha kwa sasa? Je, haingefaa kusubiri na kuona mambo yatakavyokuwa? Tuna uhakika kwamba tutafurahi kushuhudia jinsi Yehova atakavyoshughulikia mambo hayo.
-