-
“Kifo Kitafanywa Kuwa Si Kitu”Mnara wa Mlinzi—1998 | Julai 1
-
-
10 “Mwisho” ni mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo, wakati Yesu amkabidhipo Ufalme Mungu wake aliye Baba, kwa unyenyekevu na kwa uaminifu-mshikamanifu. (Ufunuo 20:4) Kusudi la Mungu “kukusanya tena pamoja vitu vyote katika Kristo” litakuwa limetimizwa. (Waefeso 1:9, 10) Ingawa hivyo, kwanza Kristo atakuwa ameharibu “serikali yote na mamlaka yote” yenye kupinga mapenzi ya Enzi Kuu ya Mungu. Hilo lahusisha mengi zaidi ya uharibifu utakaotekelezwa kwenye Har–Magedoni. (Ufunuo 16:16; 19:11-21) Paulo asema hivi: “Ni lazima [Kristo] atawale akiwa mfalme mpaka Mungu awe ameweka maadui wote chini ya miguu yake. Kikiwa ni adui wa mwisho, kifo kitafanywa kuwa si kitu.” (1 Wakorintho 15:25, 26) Naam, alama zote za dhambi na kifo cha Kiadamu zitakuwa zimeondolewa. Basi, kwa sababu ya uhitaji, Mungu atakuwa ameyaacha “makaburi ya ukumbusho” yakiwa tupu kwa kuwafufua wafu.—Yohana 5:28.
-
-
“Kifo Kitafanywa Kuwa Si Kitu”Mnara wa Mlinzi—1998 | Julai 1
-
-
15. Yamaanisha nini kusema kwamba wanaofufuliwa “[watahukumiwa] kutokana na mambo yale yaliyoandikwa katika hizo hati-kunjo”?
15 Wenye kufufuliwa “[watahukumiwaje] kutokana na mambo yale yaliyoandikwa katika hizo hati-kunjo kulingana na vitendo vyao”? Hati-kunjo hizo si rekodi ya vitendo vyao vya wakati uliopita; walipokufa, waliondolewa hatia ya dhambi walizofanya maishani mwao. (Waroma 6:7, 23) Hata hivyo, wanadamu wenye kufufuliwa bado watakuwa chini ya dhambi ya Kiadamu. Basi, ni lazima iwe kwamba hati-kunjo hizo zitaeleza kikamili maagizo ya kimungu ambayo wote lazima wafuate ili wanufaike kikamili na dhabihu ya Yesu Kristo. Alama ya mwisho ya dhambi ya Kiadamu inapofutwa, “kifo kitafanywa kuwa si kitu” katika maana kamili. Kufikia mwisho wa miaka elfu, Mungu “[ata]kuwa vitu vyote kwa kila mtu.” (1 Wakorintho 15:28) Mwanadamu hatahitaji tena uingiliaji-kati wa Kuhani wa Cheo cha Juu au Mfidi. Wanadamu wote watarudishwa kwenye hali ya ukamilifu ambayo Adamu alifurahia hapo awali.
-