-
Jihadhari na “Waepikurea”Mnara wa Mlinzi—1997 | Novemba 1
-
-
Epikurasi pia alifundisha kwamba hakuwezi kuwa na uhai baada ya kifo. Bila shaka, hilo lilikuwa kinyume cha fundisho la Biblia la ufufuo. Kwa kweli, mtume Paulo alipozungumza kwenye Areopago, yaelekea Waepikurea walikuwa miongoni mwa waliotofautiana na Paulo juu ya fundisho la ufufuo.—Matendo 17:18, 31, 32; 1 Wakorintho 15:12-14.
Huenda ikawa kwamba sehemu iliyokuwa hatari zaidi katika falsafa ya Epikurasi ilikuwa pia ndiyo yenye hila zaidi. Kule kukana kwake kuwako kwa uhai baada ya kifo kulimwongoza kwenye mkataa wa kwamba mwanadamu apaswa aishi maisha yenye furaha kadiri iwezekanavyo katika wakati wake mfupi duniani. Kama vile tumeona, wazo lake halikuwa lazima kuishi maisha yenye dhambi bali, badala yake, kuonea shangwe wakati wa sasa, kwa kuwa hakuna uhai baada ya kifo.
Hivyo, Epikurasi alipinga utendaji kosa kisiri ili kuepukana na hofu ya kugunduliwa, tisho hakika kwa furaha ya sasa. Alitia moyo kuwa na kiasi ili kuepukana na matokeo ya kujitia kupita kiasi, kizuizi kingine cha furaha ya sasa. Pia alitia moyo kuwa na mahusiano mazuri na wengine kwa sababu kufanya kwao hivyohivyo kungeleta manufaa. Bila shaka, kuepuka utendaji kosa kisiri, kuzoea kiasi, na kukuza urafiki ni vitendo vyenye kustahili pongezi. Hivyo ni kwa nini falsafa ya Epikurasi ilikuwa hatari kwa Mkristo? Kwa sababu shauri lake lilitegemea mtazamo wake huu usio na imani: “Acheni tule na tunywe, kwa maana kesho tutapaswa kufa.”—1 Wakorintho 15:32.
Ni kweli, Biblia huonyesha watu jinsi ya kuishi kwa furaha sasa. Hata hivyo, yashauri hivi: “Jitunzeni wenyewe katika upendo wa Mungu, huku mkingojea rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo kwa tazamio la uhai udumuo milele.” (Yuda 21) Ndiyo, Biblia hukazia zaidi ule wakati ujao wa milele, si wa sasa ambao unapita upesi sana. Upendezi mkubwa wa Mkristo ni kumtumikia Mungu, naye hupata kwamba amwekapo Mungu kwanza, yeye ni mwenye furaha na kutosheka. Kwa njia hiyohiyo, badala ya kujishughulisha sana na mapendezi yake kibinafsi, Yesu alitumia nishati zake bila ubinafsi akitumikia Yehova na kusaidia watu. Aliwafundisha wanafunzi wake kutendea wengine mema, bila kutumaini kutendewa hivyohivyo, lakini watende hivyo kwa sababu ya kuwapenda kikweli. Kwa wazi, vichocheo vya msingi vya Uepikurea na Ukristo ni tofauti kabisa.—Marko 12:28-31; Luka 6:32-36; Wagalatia 5:14; Wafilipi 2:2-4.
-
-
Jihadhari na “Waepikurea”Mnara wa Mlinzi—1997 | Novemba 1
-
-
Ijapokuwa Uepikurea ulitoweka karne ya nne W.K., leo kuna wale ambao hukubali maoni hayohayo ya ishi kwa ajili ya sasa. Watu hao hawana imani au wana imani kidogo katika ahadi ya Mungu ya uhai wa milele. Lakini, baadhi yao wana viwango vya juu vya mwenendo kwa kulinganishwa.
Huenda Mkristo akashawishiwa kufanyiza uhusiano wa karibu na watu wa namna hiyo, labda akisababu kwamba sifa zao nzuri hustahilisha urafiki. Hata hivyo, ingawa hatujifikirii kuwa bora zaidi, lazima tukumbuke kwamba “mashirika mabaya” yote—kutia na wale ambao uvutano wao ni wenye hila zaidi—“huharibu mazoea yenye mafaa.”
Falsafa ya ishi kwa ajili ya sasa pia hutokea katika semina fulani za kibiashara, vitabu vya kuboresha hali yako mwenyewe, riwaya, sinema, programu za televisheni, na muziki. Ingawa hayaendelezi mwenendo wenye dhambi moja kwa moja, je, maoni hayo yasiyo na imani yangeweza kutuathiri katika njia zenye hila? Kwa kielelezo, je tungeweza kuwa tukijishughulisha sana na hali ya kujiridhisha wenyewe hivi kwamba twasahau suala la enzi kuu ya Yehova? Je, tungeweza kukengeushwa ‘tufanye machache katika utumishi,’ badala ya “[ku]wa na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana”? Au tungeweza kuongozwa vibaya kutilia shaka uhaki na manufaa za viwango vya Yehova? Twahitaji kujihadhari dhidi ya kuathiriwa na ukosefu wa adili wa moja kwa moja, jeuri, na uwasiliani-roho na vilevile dhidi ya wale ambao wameathiriwa na maoni ya kilimwengu!—1 Wakorintho 15:58; Wakolosai 2:8.
-