Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoweza Kufa
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
    • KUTOWEZA KUFA

      Neno la Kigiriki a·tha·na·siʹa limeundwa kwa kiambishi a kinachokanusha muundo wa neno linalotafsiriwa “kifo” (thaʹna·tos). Hivyo, maana ya msingi ni ‘kutoweza kufa,’ na inarejelea ubora wa uhai ambao unafurahiwa, kutokuwa na mwisho kwa uhai huo na kutoharibika kwake. (1Ko 15:53, 54; 1Ti 6:16) Neno la Kigiriki a·phthar·siʹa, linalomaanisha “kutoweza kuharibika,” linarejelea uhai usioweza kudhoofika au kuharibika, ule unaodumu milele.​—Ro 2:7; 1Ko 15:42, 50, 53; Efe 6:24; 2Ti 1:10.

  • Kutoweza Kufa
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
    • Watawala Wenzi Kupewa Kutoweza Kufa. Wakristo watiwa-mafuta waliochaguliwa ili kutawala pamoja na Kristo mbinguni (1Pe 1:3, 4), wameahidiwa kushiriki pamoja na Kristo katika mfano wa ufufuo wake. (Ro 6:5) Hivyo, kama katika kisa cha Yesu aliye Bwana na Kichwa chao, wale waliotiwa mafuta katika kutaniko la Kikristo wanapokufa wakiwa waaminifu wanafufuliwa wakiwa viumbe wa kiroho wasioweza kufa, ili ‘huu unaoweza kufa uvae kutoweza kufa.’ (1Ko 15:50-54) Kama Yesu, kutoweza kufa katika kisa chao hakumaanishi tu uhai wa milele, au uhuru kutokana na kifo. Kunamaanisha kwamba wao pia wanapewa “nguvu za uzima usioweza kuharibika” wakiwa watawala wenzi pamoja na Kristo na hilo linaonekana katika maneno ya mtume Paulo kuhusiana na hali ya kutoweza kuharibika na kutoweza kufa wanayopokea. (1Ko 15:42-49) “Kifo cha pili hakina mamlaka” juu yao.​—Ufu 20:6; ona KUTOWEZA KUHARIBIKA.

      Ni jambo la pekee sana kwa warithi wa Ufalme kupewa kutoweza kufa, kwa kuzingatia ukweli huu kwamba hata malaika wa Mungu, licha ya kwamba wana miili ya kiroho na si ya nyama, wanatajwa kuwa wanaweza kufa. Uhakika wa kwamba malaika wanaweza kufa unaonekana katika hukumu ya kifo ambayo amepewa mwana wa kiroho aliyekuja kuwa Mpinzani wa Mungu, au Shetani, na pia hukumu dhidi ya malaika wengine waliofuata mwenendo wa kishetani na “hawakubaki mahali pao pa kwanza bali waliacha makao yao yanayowafaa.” (Yud 6; Mt 25:41; Ufu 20:10, 14) Kwa hiyo, kupewa “uzima usioweza kuharibika” (Ebr 7:16) au “uzima usio na kikomo” kwa Wakristo ambao wamepata pendeleo la kutawala na Mwana wa Mungu katika Ufalme wa mbinguni kunaonyesha kwa njia ya pekee uhakika ambao Mungu anao kuwaelekea.​—Ona MBINGU (Njia ya kuingia katika maisha\uhai ya mbinguni); UHAI.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki