Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Desemba
    • Ni katika maana gani mtume Paulo “alinyakuliwa mpaka kwenye mbingu ya tatu” na “kuingia katika paradiso”?—2 Kor. 12:2-4.

      Mtu huyo alikuwa nani? Paulo alipoliandikia kutaniko la Korintho, alikazia kwamba Mungu alikuwa akimtumia yeye kama mtume. (2 Kor. 11:5, 23) Kisha alitaja kuhusu ‘maono na ufunuo wa Bwana.’ Katika muktadha huo Paulo hakutaja ndugu wengine. Hivyo, tunaweza kufikia mkataa kwamba alikuwa akijirejelea yeye mwenyewe kuwa ndiye mwanamume aliyepokea maono na ufunuo.—2 Kor. 12:1, 5.

      Hivyo Paulo ndiye aliyenyakuliwa “mpaka kwenye mbingu ya tatu” na “kuingia katika paradiso.” (2 Kor. 12:2-4) Alitumia neno “ufunuo,” ambalo linadokeza kufunuliwa kwa mambo ambayo yatatukia wakati ujao.

      “Mbingu ya tatu” ambayo Paulo aliona ni nini?

      Katika Biblia, neno “mbingu” linaweza kurejelea mbingu halisi. (Mwa. 11:4; 27:28; Mt. 6:26) Lakini neno “mbingu” hutumiwa pia katika maana nyingine. Nyakati nyingine linarejelea utawala wa wanadamu. (Dan. 4:20-22) Au linaweza kurejelea utawala wa Mungu, akitumia Ufalme wake.—Ufu. 21:1.

      Paulo aliona “mbingu ya tatu.” Alimaanisha nini? Pindi fulani, katika Biblia jambo fulani hutajwa mara tatu ili kutilia mkazo, kuonyesha msisitizo, au kuongeza uzito wa jambo hilo. (Isa. 6:3; Eze. 21:27; Ufu. 4:8) Inaonekana kwamba Paulo alipozungumza kuhusu “mbingu ya tatu,” alikuwa akikazia utawala wenye ubora wa hali ya juu na uliokwezwa sana, yaani, Ufalme wa Kimasihi, Yesu Kristo akiwa mfalme pamoja na watawala wenzake 144,000. (Tazama Insight on the Scriptures, Buku la 1, uku. 1059, 1062.) Kama mtume Petro alivyoandika, tunatarajia “mbingu mpya” kulingana na ahadi ya Mungu.—2 Pet. 3:13.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Desemba
    • Inaonekana kwamba “mbingu ya tatu” inayotajwa kwenye andiko la 2 Wakorintho 12:2 ni Ufalme wa Kimasihi, Yesu Kristo akiwa mfalme pamoja na watawala wenzake 144,000, yaani, “mbingu mpya.”​—2 Pet. 3:13.

      Inatajwa kuwa “mbingu ya tatu” kwa sababu Ufalme huo ni utawala wenye ubora wa hali ya juu na uliokwezwa sana.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki