-
“Mungu wa Faraja Yote”Mnara wa Mlinzi—2008 | Septemba 1
-
-
MAMBO mengi maishani kama vile, kuteseka, kuvunjika moyo, au upweke, yanaweza kumfanya mtu ahuzunike au hata atamauke. Nyakati kama hizo unaweza kujiuliza, ‘Nitapata wapi msaada?’ Maneno ya mtume Paulo yanayopatikana kwenye 2 Wakorintho 1:3, 4 yanaonyesha chanzo cha faraja isiyokoma, yaani, Yehova Mungu.
Katika mstari wa 3, Mungu anaitwa “Baba ya rehema nyororo.” Maneno hayo yanamaanisha nini? Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “rehema nyororo” linaweza kuwa na wazo la kuhisi huruma kwa ajili ya kuteseka kwa wengine.a Kitabu kimoja cha marejeo ya Biblia kinasema kwamba neno hilo linaweza kutafsiriwa “anahisi sikitiko” au “anajali sana.” “Rehema nyororo” za Mungu zinamchochea kutenda. Kujua sifa hiyo ya utu wa Mungu kunatufanya tutake kumkaribia, sivyo?
Pia, Paulo anamrejelea Yehova kama “Mungu wa faraja yote.” Hapo Paulo anatumia neno linalosemekana kutia ndani “wazo la kumliwaza mtu aliye na matatizo au huzuni na la kumsaidia au kumtia moyo.” Kitabu fulani kuhusu Biblia (The Interpreter’s Bible) kinaeleza hivi: “Tunamfariji mtu anayeteseka tunapompa ujasiri wa kuvumilia maumivu yake.”
Huenda ukauliza, ‘Mungu anatufariji jinsi gani na kutupa ujasiri wa kuvumilia maumivu?’ Anafanya hivyo hasa kupitia Neno lake, Biblia, na kupitia zawadi ya sala. Paulo anatuambia kwamba kwa upendo Mungu anatupa Neno Lake ili “kupitia faraja kutokana na Maandiko tuwe na tumaini.” Isitoshe, kupitia sala za kutoka moyoni, tunaweza kuwa na “amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote.”—Waroma 15:4; Wafilipi 4:7.
-
-
“Mungu wa Faraja Yote”Mnara wa Mlinzi—2008 | Septemba 1
-
-
a Mungu anaitwa “Baba [au, chanzo] ya rehema nyororo” kwa sababu huruma inatoka kwake na ni sehemu ya utu wake.
-