-
Kitabu Cha Biblia Namba 48—Wagalatia“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
12. (a) Sasa ni lazima Wagalatia watembee kulingana na nini? (b) Paulo afanya utofautiano gani wa maana?
12 Kutahiriwa au kutotahiriwa si kitu, aeleza Paulo, bali jambo la maana ni imani yenye kufanya kazi kupitia upendo. Sheria nzima yatimizwa katika usemi huu: “Umpende jirani yako kama nafsi yako.” Endeleeni kutembea kwa roho, kwa maana ‘mkiongozwa na roho, hampo chini ya sheria.’ Kwa habari ya kazi za mwili, Paulo atangulia kuonya “kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.” Kwa kuonyesha utofautiano mkubwa, aeleza juu ya matunda ya roho, ambayo hayana sheria juu yayo, na aongezea hivi: ‘Tukiishi kwa roho, na tuenende kwa roho’ na kuondolea mbali majivuno na husuda.—5:14, 18, 21, 25.
-
-
Kitabu Cha Biblia Namba 48—Wagalatia“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
15. Barua hiyo ilikuwaje yenye mafaa kwa makundi ya Galatia, nayo yatoa uongozi gani kwa Wakristo leo?
15 Barua hii ilikuwa yenye mafaa kwa makundi katika Galatia ili kuthibitisha waziwazi uhuru wao katika Kristo na kuondosha sifa ya wakengeushaji wa habari njema. Ilionyesha wazi ni kwa imani kwamba mtu hujulishwa rasmi kuwa mwadilifu na kwamba kutahiriwa si kwa lazima tena ili mtu apate wokovu. (2:16; 3:8; 5:6) Kwa kuweka kando tofauti hizo za kimwili, ilitumika kuunganisha Wayahudi na wasio Wayahudi katika lile kundi moja. Uhuru kutokana na Sheria haukupasa kutumika kuwa kichocheaji tamaa za mwili, kwa maana kanuni hii ingali ilihusu: “Umpende jirani yako kama nafsi yako.” Yaendelea kutumika ikiwa kielekezi kwa Wakristo leo.—5:14.
-