-
‘Waite Wazee wa Kundi’Mnara wa Mlinzi—1993 | Mei 15
-
-
18, 19. Wazee Wakristo wana daraka gani kuhusiana na Wagalatia 6:2, 5?
18 Ni lazima wazee Wakristo wachukue daraka lao kuelekea kundi la Mungu. Ni lazima wawe wenye kuunga mkono. Kwa mfano, Paulo alisema hivi: “Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe. Mchukuliane mizigo [yenye kulemea, NW] na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo.” Mtume aliandika hivi pia: “Kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe.”—Wagalatia 6:1, 2, 5.
19 Tunaweza kuchukulianaje mizigo yenye kulemea na hata hivyo kulichukua furushi letu wenyewe? Tofauti katika maana ya yale maneno ya Kigiriki ambayo yametafsiriwa “mizigo yenye kulemea” na “furushi” ndiyo hutoa jibu. Mkristo akipatwa na ugumu wa kiroho unaomlemea sana, wazee na waamini wenzake wengine wangemsaidia, hivyo wakimsaidia kuchukua “mizigo” yake yenye kulemea. Hata hivyo, mtu huyo mwenyewe anatazamiwa kuchukua “furushi” lake mwenyewe la daraka kwa Mungu.a Wazee huchukua kwa furaha “mizigo yenye kulemea” ya ndugu zao kupitia kitia-moyo, shauri la Kimaandiko, na sala. Hata hivyo, wazee hawaondoi “furushi” letu la kibinafsi la daraka la kiroho.—Warumi 15:1.
-
-
‘Waite Wazee wa Kundi’Mnara wa Mlinzi—1993 | Mei 15
-
-
a A Linguistic Key to the Greek New Testament, cha Fritz Rienecker, chafasili phor·tiʹon kuwa “mzigo ambao mtu hutazamiwa kuchukua” na chaongeza hivi: “Lilitumiwa likiwa neno la kijeshi la kifurushi cha mtu au vifaa vya askari-jeshi.”
-