-
Ujuzi wa Kimbele, Agizo la KimbeleUfahamu wa Kina wa Maandiko
-
-
Maoni ya ile imani ya kuwa imeandikwa kimbele. Maoni ya kwamba matumizi ya Mungu ya ujuzi wa kimbele hayana kipimo na kwamba yeye huagiza kimbele mwendo na hatima ya kila mtu mmoja-mmoja ndiyo ile imani ya kuwa imeandikwa kimbele. Wanaoitetea husema kwamba kwa vile yeye ni Mungu na ni mkamilifu mambo hayo yanamtaka awe mjua-yote, si kwa habari ya wakati uliopita na wakati uliopo bali pia kuhusiana na wakati ujao. Kulingana na dhana hiyo, akikosa kujua kimbele mambo yote kutia na lililo dogo zaidi jambo hilo lingekuwa ni uthibitisho wa kutokamilika. Mifano kama vile kisa cha wana-mapacha wa Isaka, Esau na Yakobo, hutumiwa kuwa uthibitisho wa kwamba Mungu huagiza kimbele juu ya viumbe kabla havijazaliwa. (Ro 9:10-13); na maandiko kama vile Waefeso 1:4, 5 hutajwa kuwa uthibitisho wa kwamba Mungu alijua kimbele na kuagiza kimbele ni nini utakaokuwa wakati ujao wa viumbe vyake vyote hata kabla ya mwanzo wa uumbaji.
-
-
Ujuzi wa Kimbele, Agizo la KimbeleUfahamu wa Kina wa Maandiko
-
-
Kwa wakati wake Yehova Mungu alimpa mgawo Mwana wake mzaliwa wa kwanza atimize fungu la “uzao” lililotabiriwa na kuwa Masihi. Hakuna jambo la kuonyesha kwamba Mwana huyo alikuwa ‘ameandikiwa kimbele’ fungu hilo hata kabla ya yeye kuumbwa au kabla ya uasi kutokea katika Edeni. Vilevile uteuzi wake na Mungu uliofanywa hatimaye awe na daraka la kutimiza unabii mbalimbali haukufanywa bila ya kuwapo na msingi kimbele. Bila shaka, kile kipindi cha ushirikiano wa kindani kati ya Baba na Mwanaye kabla hajatumwa duniani kilimfanya Yehova ‘amjue’ Mwanaye kwa kadiri ambayo yeye angeweza kuwa na uhakika Mwanaye angetimiza kwa uaminifu ahadi na mifano ya kinabii.—Linganisha Ro 15:5; Flp 2:5-8; Mt 11:27; Yoh 10:14, 15; ona YESU KRISTO (Aliyejaribiwa na Kukamilishwa).
Kuagizwa kimbele kwa “walioitwa na waliochaguliwa.” Kumebaki yale maandishi yanayoshughulika na Wakristo “walioitwa,” au “waliochaguliwa.” (Yuda 1; Mt 24:24) Wanasimuliwa kuwa “waliochaguliwa kulingana na ujuzi wa kimbele wa Mungu Baba” (1Pe 1:1, 2), ‘waliochaguliwa kabla ya kuwekwa msingi wa ulimwengu,’ ‘walioagizwa kimbele ili kufanywa kuwa wana wa Mungu’ (Efe 1:3-5, 11), ‘waliochaguliwa tangu mwanzo kwa ajili ya wokovu na kuitwa kwa lengo hili’ (2Th 2:13, 14). Kuelewa maandiko haya kunategemea kama yanarejezea kuagizwa kimbele kwa watu fulani au kama yanasimulia kuagizwa kimbele kwa jamii ya watu, yaani, kutaniko la Kikristo, ule “mwili mmoja” (1Ko 10:17) wa wale watakaokuwa warithi-washirika pamoja na Kristo Yesu katika Ufalme wake wa kimbingu.—Efe 1:22, 23; 2:19-22; Ebr 3:1, 5, 6.
Ikiwa maneno hayo yanatumika kwa watu fulani kuwa wameagizwa kimbele wapate wokovu wa milele, basi inamaanisha kwamba watu hao mmoja-mmoja hawangeweza kamwe kukosa kuwa waaminifu au kushindwa kutimiza wito wao, kwa maana ujuzi wa kimbele wa Mungu kuwahusu haungeweza kukosea na agizo lake la kimbele kuhusiana na wao kufikia kusudi fulani halingeweza kamwe kushindwa au kuzuiwa. Hata hivyo mitume hao hao waliopuliziwa kuandika maneno hayo yaliyotangulia walionyesha kwamba baadhi ya ‘walionunuliwa’ na ‘kutakaswa’ na damu ya fidia ya dhabihu ya Kristo na ambao walikuwa “wameonja zawadi ya bure ya kimbingu” na ‘kuwa washiriki wa roho takatifu na nguvu za mfumo wa mambo unaokuja’ wangekengeuka wapite hatua ya kuweza kutubu na wajiletee uharibifu. (2Pe 2:1, 2, 20-22; Ebr 6:4-6; 10:26-29) Kwa muungano mitume waliwasihi wale waliowaandikia: “Fanyeni hata zaidi yote mnayoweza ili kufanya mwito na kuchaguliwa kwenu kuwe hakika kwa ajili yenu wenyewe; kwa maana mkiendelea kufanya mambo hayo hamtashindwa hata kidogo”; pia, “Endeleeni kuufanyia kazi wokovu wenu
wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.” (2Pe 1:10, 11; Flp 2:12-16) Paulo, “aliyeitwa kuwa mtume wa Yesu Kristo” (1Ko 1:1), kwa wazi hakujichukua binafsi kuwa ameandikiwa kimbele wokovu wa milele, kwa kuwa anazungumzia jitihada zake nyingi za kupania kufikia “ule mradi kwa ajili ya tuzo la mwito wa Mungu wa kwenda juu” (Flp 3:8-15) na hangaiko lake yeye mwenyewe asije ‘akakataliwa kwa njia fulani.’—1Ko 9:27.
-