Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi Ambavyo Kutaniko Limepangwa
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • Yehova ni Mungu mwenye utaratibu. (1 Wakorintho 14:33) Hivyo, tunatazamia watu wake wawe na utaratibu. Kutaniko la Kikristo limepangwa jinsi gani? Tunawezaje kuunga mkono utaratibu huo?

      1. Kichwa cha kutaniko ni nani?

      ‘Kristo ndiye kichwa cha kutaniko.’ (Waefeso 5:23) Akiwa mbinguni, anaongoza kazi ya watu wa Yehova ulimwenguni pote. Yesu alimweka rasmi “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” yaani, kikundi kidogo cha wazee wakomavu ambao pia wanaitwa Baraza Linaloongoza. (Soma Mathayo 24:45-47.) Kama mitume na wazee katika karne ya kwanza huko Yerusalemu, Baraza Linaloongoza hutoa mwongozo kwa makutaniko yote ulimwenguni. (Matendo 15:2) Hata hivyo, wanaume hao si viongozi wa tengenezo letu. Wanafuata mwongozo wa Yehova na Neno lake na kujitiisha chini ya ukichwa wa Yesu.

      2. Wazee wana jukumu gani?

      Wazee ni Wakristo wakomavu wanaofundisha kwa kutumia Maandiko na kuwachunga watu wa Yehova kwa kuwasaidia na kuwatia moyo. Hawalipwi mshahara kwa kazi wanayofanya. Badala yake, wanatumikia “kwa hiari mbele za Mungu; si kwa kupenda pato lisilo la haki, bali kwa hamu.” (1 Petro 5:1, 2) Wazee husaidiwa na watumishi wa huduma ambao baadaye wanaweza kustahili kuwa wazee.

      Baraza Linaloongoza huweka rasmi baadhi ya wazee wawe waangalizi wa mzunguko. Waangalizi hao hutembelea makutaniko mbalimbali ili kutoa mwongozo na kuwatia moyo akina ndugu na dada. Wao huweka rasmi wazee na watumishi wa huduma, ambao wanapaswa kutimiza viwango vilivyoonyeshwa katika Maandiko.​—1 Timotheo 3:1-10, 12; Tito 1:5-9.

      3. Kila Shahidi wa Yehova ana jukumu gani?

      Wote katika kutaniko ‘hulisifu jina la Yehova’ kwa kushiriki katika mikutano na kazi ya kuhubiri kulingana na hali zao.​​—Soma Zaburi 148:12, 13.

      CHIMBA ZAIDI

      Jifunze Yesu ni kiongozi wa aina gani, jinsi wazee wanavyojitahidi kuiga mfano wake, na jinsi tunavyoweza kumtii Yesu na kushirikiana na wazee wa kutaniko.

      4. Yesu ni kiongozi mwenye fadhili na mwenye kuburudisha

      Yesu anatupatia mwaliko wenye kupendeza. Soma Mathayo 11:28-30, kisha mzungumzie swali hili:

      • Yesu ni kiongozi wa aina gani na anataka tuhisije kuhusu uongozi wake?

      Wazee wanaigaje mfano wa Yesu? Onyesha VIDEO.

      VIDEO: Wazee Wachukua Hatua Baada ya Tetemeko Huko Nepal (4:56)

      Biblia inafundisha waziwazi jinsi wazee wanavyopaswa kufanya kazi yao.

      Soma Isaya 32:2 na 1 Petro 5:1-3, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Unahisije unapojua kwamba wazee wanajitahidi kuwaburudisha wengine kwa kumwiga Yesu?

      • Wazee wanamwiga Yesu katika njia gani nyingine?

      5. Wazee hufundisha kwa kuweka mfano

      Yesu anataka wazee wawe na maoni gani kuhusu jukumu lao? Onyesha VIDEO.

      VIDEO: Wazee Ongozeni! (7:39)

      Yesu aliwawekea mfano wale wanaoongoza kutanikoni. Soma Mathayo 23:8-12, kisha mzungumzie swali hili:

      • Unapochunguza kile ambacho Biblia inasema kuhusu jinsi wazee wanavyopaswa kutenda, umeona tofauti gani na viongozi wa dini nyingine?

      A. Picha: Mzee akikazia fikira hali yake ya kiroho na ya familia yake. 1. Anasali kabla ya kujifunza Biblia. 2. Anamfundisha binti yake Biblia akisaidiana na mke wake. B. Mzee yuleyule na mke wake wakimtembelea dada mgonjwa wa kutaniko lao aliyelazwa hospitalini. C. Mzee yuleyule akimhubiria mtu nyumbani kwake. D. Picha: 1. Mzee yuleyule anatoa hotuba kwenye mkutano wa kutaniko. 2. Anasafisha sakafu ya Jumba la Ufalme.
      1. Wazee hujitahidi kuimarisha hali yao ya kiroho na ya familia zao

      2. Wazee wanawajali wote katika kutaniko

      3. Wazee wanahubiri kwa ukawaida

      4. Wazee ni walimu. Pia, wanasaidia kufanya usafi na kazi nyingine

      6. Jinsi tunavyoweza kushirikiana na wazee

      Biblia inatuonyesha umuhimu wa kushirikiana na wazee. Soma Waebrania 13:17, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Biblia inatutia moyo tutii na kujinyenyekeza chini ya wale wanaoongoza, je, ushauri huo unafaa? Kwa nini?

      Soma Luka 16:10, kisha mzungumzie swali hili:

      • Kwa nini ni muhimu kushirikiana na wazee hata katika mambo yanayoonekana kuwa madogo?

      WATU FULANI HUSEMA: “Si lazima ushirikiane na kikundi fulani cha dini.”

      • Unafikiri kuna manufaa gani ya kumwabudu Mungu kwa kushirikiana na kutaniko?

      MUHTASARI

      Yesu ndiye kichwa cha kutaniko. Tunafurahia kushirikiana na wazee wanaotumikia chini ya Yesu kwa sababu wanatuburudisha na kutufundisha kupitia mfano wao mzuri.

      Ungejibuje?

      • Kichwa cha kutaniko ni nani?

      • Wazee wanasaidiaje kutaniko?

      • Kila mwabudu wa Yehova ana jukumu gani?

      Lengo

      CHUNGUZA ZAIDI

      Ona uthibitisho unaoonyesha jinsi Baraza Linaloongoza na wazee katika kutaniko wanavyowahangaikia Wakristo leo.

      Kuwaimarisha Akina Ndugu Wakati wa Marufuku (4:22)

      Jifunze kuhusu kazi ambayo waangalizi wa mzunguko wanafanya.

      Maisha ya Mwangalizi wa Mzunguko Vijijini (4:51)

      Soma kuhusu jukumu la wanawake katika kutaniko.

      “Je, Mashahidi wa Yehova Wanawaruhusu Wanawake Kufundisha?” (Mnara wa Mlinzi, Septemba 1, 2012)

      Chunguza jinsi wazee wanavyojitahidi kuwatia moyo waamini wenzao.

      “Wazee Wakristo Ni ‘Wafanyakazi Wenzi kwa Shangwe Yetu’” (Mnara wa Mlinzi, Januari 15, 2013)

  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha—Sehemu ya 1
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 1. Biblia inatoa ushauri gani kwa waume?

      Yehova amempa mume jukumu la kuwa kichwa cha familia. (Soma Waefeso 5:23.) Yehova anatarajia mume afanye maamuzi yatakayoinufaisha familia. Biblia inawashauri hivi waume: “Endeleeni kuwapenda wake zenu.” (Waefeso 5:25) Hilo linamaanisha nini? Mume mwenye upendo humtendea mke wake kwa fadhili wanapokuwa nyumbani na pia hadharani. Anahakikisha kwamba mke wake yuko salama na anafanya yote anayoweza ili kumtimizia mahitaji yake ya kimwili na ya kihisia. (1 Timotheo 5:8) Jambo muhimu zaidi, anamsaidia mke wake kusitawisha urafiki wa karibu na Yehova. (Mathayo 4:4) Kwa mfano, anaweza kusali na kusoma Biblia pamoja na mke wake. Mume anapomtendea mke wake kwa upendo na kumjali, anadumisha urafiki mzuri na Yehova.​—Soma 1 Petro 3:7.

  • Jukumu la “Mtumwa Mwaminifu na Mwenye Busara”
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • Yesu ndiye Kichwa cha kutaniko la Kikristo. (Waefeso 5:23) Leo, Yesu akiwa mbinguni anaongoza wafuasi wake duniani kupitia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” (Soma Mathayo 24:45.) Kwa kuwa aliwekwa rasmi na Yesu, “mtumwa” huyo ana mamlaka kwa kadiri fulani, lakini bado anaendelea kuwa mtumwa wa Kristo na kuwatumikia ndugu za Kristo. Mtumwa huyo ni nani? Naye anatutunza jinsi gani?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki