Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ujitiisho Katika Ndoa Humaanisha Nini?
    Mnara wa Mlinzi—1991 | Desemba 15
    • Si Mdhalimu

      Mume apaswa kutumiaje mamlaka yake? Kwa kufuata mfano mwema wa Mwana wa Mungu. Biblia husema hivi: “Mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa [kundi, NW]; naye ni mwokozi wa mwili. Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa [kundi, NW], akajitoa kwa ajili yake.” (Waefeso 5:23, 25) Utumizi wa ukichwa wa Yesu Kristo ulikuwa baraka kwa kundi. Yeye hakuwa mdhalimu. Hakufanya wanafunzi wake wahisi wamezuiwa au kuonewa. Badala ya hivyo, alipata staha ya wote kwa kuwatendea kwa upendo na huruma. Ni mfano mwema kama nini wa kufuatwa na waume katika kuwatendea wake zao!

      Lakini, kuna waume ambao hawafuati mfano huo mwema. Wao hutumia ukichwa wao wenye kupewa na Mungu kwa ubinafsi, badala ya kuutumia kwa faida ya wake zao. Wao hutawala wake zao kwa njia ya udhalimu, wakidai ujitiisho ulio kamili na mara nyingi kutowaruhusu wajifanyie maamuzi yoyote. Kwa wazi, wake za waume kama hao huishi maisha yasiyo ya furaha. Na mume kama huyo huteseka pia kwa sababu anashindwa kupata staha yenye upendo ya mke wake.

      Ni kweli, Mungu hutaka mke astahi cheo ambacho mume wake hushikilia akiwa kichwa cha familia. Lakini ikiwa mume anatamani kuonea shangwe staha ya mke yenye kuhisiwa-moyoni kuelekea kwake akiwa mtu, ni lazima aistahili, na njia iliyo bora zaidi ya kufanya hivyo ni kwa kutenda kwa kujali madaraka na kusitawisha sifa njema za kimungu akiwa kichwa cha nyumba.

      Ujitiisho Ni wa Kadiri

      Mamlaka ya mume juu ya mke wake si ya kamili. Katika njia fulani ujitiisho wa mke waweza kulinganishwa na ujitiisho wa Mkristo kwa mtawala wa kilimwengu. Mungu huagiza kwamba ni lazima Mkristo “aitii mamlaka iliyo kuu.” (Warumi 13:1) Hata hivyo ni lazima ujitiisho huo usawazishwe sikuzote na yale tunayowiwa na Mungu. Yesu alisema: “Mpeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na yaliyo ya Mungu mpeni Mungu.” (Marko 12:17) Ikiwa Kaisari (serikali ya kilimwengu) anadai yaliyo ya Mungu, twakumbuka yale mtume Petro aliyosema: “Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu.”—Matendo 5:29.

  • Ujitiisho Katika Ndoa Humaanisha Nini?
    Mnara wa Mlinzi—1991 | Desemba 15
    • Mume atadumisha upendo na staha ya mke wake anapoangaza sifa za kimungu za kichwa chake, Yesu Kristo, aliyewaamuru wafuasi wake wapendane wao kwa wao. (Yohana 13:34) Hata ingawa mume ni mwenye kukosea na asiye mkamilifu, akitumia mamlaka yake kupatana na ukichwa wa Kristo wenye ubora wa juu zaidi, anafanya iwe rahisi zaidi kwa mke wake kufurahi kuwa naye akiwa kichwa chake. (1 Wakorintho 11:3) Ikiwa mke anasitawisha sifa za Kikristo za kiasi na fadhili-upendo, si vigumu kwake kujitiisha mwenyewe kwa mume wake.

  • Ujitiisho Katika Ndoa Humaanisha Nini?
    Mnara wa Mlinzi—1991 | Desemba 15
    • Mielekeo kama hiyo yapasa isitawishwe kundini. Na yapasa hasa isitawishwe kati ya mume na mke katika nyumba ya Kikristo. Mume aweza kuonyesha shauku yake nyororo na upole wake kwa kusikiliza madokezo kutoka kwa mke wake. Apaswa afikirie maoni ya mke wake kabla ya kufanya uamuzi unaoathiri familia. Wake Wakristo si vichwa vitupu. Mara nyingi wanaweza kuwapa waume zao madokezo yenye thamani, kama Sara alivyompa mume wake, Abrahamu. (Mwanzo 21:12) Kwa upande mwingine, mke Mkristo hatakuwa mwenye kudai mengi kupita kiasi kwa mume wake. Ataonyesha fadhili na unyenyekevu wake wa akili kwa kufuata mwongozo wa mume wake na kuunga mkono maamuzi yake, hata ingawa nyakati nyingine huenda yakawa tofauti na mapendeleo yake mwenyewe.

      Mume mwenye kiasi, kama vile mzee mwenye kiasi, ni mwenye kukaribika na mwenye fadhili. Mke mwenye upendo huitikia kwa kuwa mwenye huruma na mstahimilivu, akitambua jitihada za mume za kutimiza madaraka yake kujapokuwa kutokamilika na mibano ya maisha. Mielekeo kama hiyo inapositawishwa na mume na mke pia, ujitiisho katika ndoa hautakuwa tatizo. Bali, ni chanzo cha shangwe, usalama, na uradhi wenye kudumu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki