-
Biblia Inasema Nini Kuhusu Ndoa?Maswali ya Biblia Yajibiwa
-
-
Majukumu ya wote wawili. Waume na wake wanapaswa kutendeana kwa upendo na heshima. (Waefeso 5:33) Kila mmoja anapaswa kushughulikia mahitaji ya ngono ya mwenzake kwa njia yenye upendo na kuepuka aina zote za ukosefu wa uaminifu. (1 Wakorintho 7:3; Waebrania 13:4) Ikiwa wana watoto, mume na mke wana jukumu la kusaidiana kuwalea.—Methali 6:20.
Biblia haisemi kihususa jinsi wenzi wa ndoa wanavyopaswa kugawana majukumu yanayohusu kazi ya kimwili na kazi za nyumbani. Wanapaswa kuamua pamoja ni nini kitakachofaa familia yao.
-
-
Biblia Inasema Nini Kuhusu Ndoa?Maswali ya Biblia Yajibiwa
-
-
Jukumu la mke. Biblia inasema kwamba “mke anapaswa kumheshimu sana mume wake.” (Waefeso 5:33) Mke anapoheshimu jukumu ambalo Mungu amemkabidhi mume wake, Mungu anafurahi.
Jukumu la mke ni kuwa msaidizi wa mume wake, kumsaidia kufanya maamuzi mazuri, na kuunga mkono ukichwa wake. (Mwanzo 2:18) Biblia inamsifu mke anayetimiza jukumu lake muhimu katika ndoa.—Methali 31:10.
-