Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Ndoa?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
      • Majukumu ya wote wawili. Waume na wake wanapaswa kutendeana kwa upendo na heshima. (Waefeso 5:33) Kila mmoja anapaswa kushughulikia mahitaji ya ngono ya mwenzake kwa njia yenye upendo na kuepuka aina zote za ukosefu wa uaminifu. (1 Wakorintho 7:3; Waebrania 13:4) Ikiwa wana watoto, mume na mke wana jukumu la kusaidiana kuwalea.—Methali 6:20.

        Mama akimsaidia binti yake kufanya kazi za shule huku baba akikatakata mboga karibu nao.

        Biblia haisemi kihususa jinsi wenzi wa ndoa wanavyopaswa kugawana majukumu yanayohusu kazi ya kimwili na kazi za nyumbani. Wanapaswa kuamua pamoja ni nini kitakachofaa familia yao.

  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Ndoa?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
      • Jukumu la mke. Biblia inasema kwamba “mke anapaswa kumheshimu sana mume wake.” (Waefeso 5:33) Mke anapoheshimu jukumu ambalo Mungu amemkabidhi mume wake, Mungu anafurahi.

        Mume na mke wakizungumzia mambo yanayohusu pesa pamoja.

        Jukumu la mke ni kuwa msaidizi wa mume wake, kumsaidia kufanya maamuzi mazuri, na kuunga mkono ukichwa wake. (Mwanzo 2:18) Biblia inamsifu mke anayetimiza jukumu lake muhimu katika ndoa.—Methali 31:10.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki