-
Kitabu Cha Biblia Namba 49—Waefeso“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
8. Ni katika mambo gani barua ya Paulo kwa Waefeso iliandikwa kwa wakati ufaao kabisa?
8 Sasa, akiwa gerezani, Paulo afikiria matatizo yenye kukabiliwa na kundi la Efeso, lenye kuzungukwa na waabudu wapagani likiwa katika uvuli wa lile hekalu lenye kutia hofu nyingi la Artemi. Bila shaka Wakristo hawa wapakwa mafuta walihitaji kile kielezi anachowapa sasa Paulo, kinachoonyesha kwamba wao wafanyiza “hekalu takatifu,” ambamo Yehova hukaa kupitia roho yake. (Efe. 2:21) “Siri takatifu” yenye kufunuliwa kwa Waefeso, kuhusu usimamizi wa Mungu (njia yake ya kusimamia mambo yake ya nyumba) ambao kwao angerudisha umoja na amani kupitia Yesu Kristo, bila shaka iliwachochea na kuwafariji sana. (1:9, 10, NW) Paulo akazia muungano wa Myahudi na Asiye Myahudi katika Kristo. Yeye awahimiza kwenye umoja, kwenye muungamano. Hivyo, sisi twaweza sasa kuthamini kusudi, thamani, na kichocheo cha kitabu hiki.
-
-
Kitabu Cha Biblia Namba 49—Waefeso“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
9. Mungu amefanyaje upendo wake uwe mwingi sana, na sala ya Paulo ni nini?
9 Kusudi la Mungu la kuleta umoja kwa njia ya Kristo (1:1–2:22). Paulo mtume apeleka salamu. Mungu abarikiwe kwa sababu ya fadhili zake zisizostahilika zenye utukufu. Jambo hili lahusu vile Yeye aliwachagua wao wawe katika muungano pamoja na Yesu Kristo, ambaye kwa njia yake wao wapata kufunguliwa kwa ukombozi kupitia damu yake. Zaidi ya hilo, Mungu amefanya upendo wake uwe mwingi kuwaelekea kwa kujulisha siri takatifu ya penzi lake. Kwa maana yeye amekusudia usimamizi, ili “kukusanya tena vitu vyote pamoja katika Kristo,” katika muungano na yule ambaye wao pia walipewa mgawo wawe warithi pamoja naye. (1:10, NW) Wao wametiwa muhuri kwa roho takatifu ili hicho kiwe kionyeshi cha mapema kwamba watakuwa hivyo. Sala ya Paulo ni kwamba watasadikishwa kwa uthabiti juu ya tumaini ambalo wameitiwa na watambue kwamba, Mungu atatumia kuwaelekea wao, nguvu ile ile aliyotumia katika kufufua Kristo na kumweka awe juu sana ya kila serikali na mamlaka na kumfanya awe Kichwa cha vitu vyote kuhusiana na kundi, ndiyo pia ataitumia kuwaelekea wao.
-
-
Kitabu Cha Biblia Namba 49—Waefeso“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
19. Ni tumaini na kitia-moyo gani ambacho Waefeso yaendelea kutoa kwa siku hii?
19 Kwa habari ya “ile siri takatifu,” pia Paulo alinena juu ya “usimamizi . . . [wa] kuvikusanya tena vitu vyote pamoja katika Kristo, vitu vilivyomo mbinguni [wale waliochaguliwa kuwa katika Ufalme wa kimbingu] na vitu vilivyomo duniani [wale ambao wangeishi duniani katika makao ya Ufalme huo].” (NW) Kwa njia hiyo kusudi tukufu la Mungu la kurudisha amani na umoja latangulizwa. Kwa habari hiyo Paulo alisali kwa ajili ya Waefeso, ambao macho ya mioyo yao yalikuwa yameelimishwa, kwamba waweze kulishika kikamili tumaini ambalo Mungu alikuwa amewaitia na kuona “utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu.” Lazima maneno hayo yawe yaliwatia moyo sana katika tumaini lao. Na barua hiyo iliyopuliziwa na Mungu waliyoandikiwa Waefeso yaendelea kujenga kundi mpaka siku hii, ili ‘tupate kutimilika kwa utimilifu wote wa Mungu.’—1:9-11, 18; 3:19.
-