Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Unaweza Kuamua Wakati Wako Ujao Utakuwaje?
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Januari 15
    • Mtume Paulo aliandika hivi: “[Mungu] ametubariki kwa kila aina ya baraka ya kiroho katika mahali pa kimbingu katika muungano na Kristo, kama vile alivyotuchagua katika muungano naye kabla ya kuwekwa msingi wa ulimwengu . . . Kwa maana alituagiza kimbele ili tufanywe kuwa wana kwake kupitia Yesu Kristo.” (Waefeso 1:3-5) Ni nini ambacho Mungu ameagiza kimbele, na kuchaguliwa “kabla ya kuwekwa msingi wa ulimwengu” kunamaanisha nini?

  • Je, Unaweza Kuamua Wakati Wako Ujao Utakuwaje?
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Januari 15
    • Mtume Paulo alikuwa akifikiria ulimwengu gani aliposema: ‘Mungu alituchagua katika muungano naye kabla ya kuwekwa msingi wa ulimwengu’? Ulimwengu ambao Paulo anataja hapa si ulimwengu ambao Mungu alianzisha alipowaumba Adamu na Hawa. Ulimwengu huo ulikuwa ‘mwema sana’—bila dhambi au upotovu wowote. (Mwanzo 1:31) Haukuhitaji “kuachiliwa huru” kutoka katika dhambi.—Waefeso 1:7.

      Ulimwengu ambao Paulo alimaanisha ni ule ambao ulianza baada ya Adamu na Hawa kuasi huko Edeni—ulimwengu ulio tofauti sana na ule uliokusudiwa na Mungu hapo mwanzoni. Ni ulimwengu ambao ulianza na watoto wa Adamu na Hawa. Ulimwengu huo ulifanyizwa na watu waliotengwa na Mungu na watumwa wa dhambi na uharibifu. Ni ulimwengu wa watu ambao wangeweza kukombolewa, tofauti na Adamu na Hawa waliotenda dhambi kimakusudi.—Waroma 5:12; 8:18-21.

      Yehova Mungu aliweza kushughulikia mara moja hali iliyotokana na uasi huo huko Edeni. Mara tu uhitaji ulipotokea, aliagiza kimbele shirika la kipekee—Ufalme wa Kimasihi mikononi mwa Yesu Kristo—ambao ungewakomboa wanadamu kutoka katika dhambi ya Adamu. (Mathayo 6:10) Mungu alifanya hivyo “kabla ya kuwekwa msingi wa ulimwengu” wa wanadamu wanaoweza kukombolewa, yaani, kabla ya Adamu na Hawa walioasi kuzaa watoto.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki