Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kupumua “Hewa ya Ulimwengu Huu Kunaleta Kifo!
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Septemba 15
    • Kupumua “Hewa ya Ulimwengu Huu Kunaleta Kifo!

      “Ni ninyi ambao Mungu alifanya hai ingawa ninyi mlikuwa mmekufa katika makosa yenu na dhambi, ambazo katika hizo wakati mmoja mlitembea... kulingana na mtawala wa mamlaka ya hewa.”​—WAEFESO 2:1, 2, NW.

      1. Uchafuzi wa hewa umekujaje kuwa wenye kuletea wanadamu kifo?

      MPUMUO wa hewa safi! Ni wenye kuburudisha kama nini baada ya mtu kuwa katika chumba kilichojazana hewa nzito! Lakini hata katika nafasi zilizo wazi sana, uchafuzi ni tatizo kubwa leo. Sumu zinatupwa-tupwa ndani ya anga kwa kadiri ya kugutusha katika nchi nyingi. Mivukizo yenye sumu, mavumbi ya redioaktivu, (au, redio-utendaji) viini vibaya vyenye kuleta magonjwa, na virasi fulani fulani vyote vinasafiri kwa hewa. Hewa yenye kuendeleza uhai ilivyoandaliwa, kwa ukarimu sana na Muumba wetu mwenye upendo inaendelea zaidi na zaidi kuleta kifo kwa sababu ya pupa na uzembe wa wanadamu.

      2. Ni “hewa” gani iliyochafuliwa iliyo hatari kuliko hewa ile iliyochafuliwa ambayo huenda tukapumua?

      2 Hata hivyo, ingawa uchafuzi wa hewa ni hatari sana, kuna namna yenye kufisha zaidi ya “hewa” iliyochafuliwa. Hiyo si hewa iliyotiwa uchafu kutokana na aksidenti ile ya nyukilia iliyotukia Chernobyl (Urusi) wala si hewa iliyojaa ukungu-moshi wa Los Angeles, California (United States). Hapana, sisi tumo katika hatari ya kupumua “hewa” yenye kuua kuliko hiyo. Mtume Paulo aliitaja alipoambia Wakristo wenzake hivi: “Ni ninyi ambao Mungu alifanya hai ingawa ninyi mlikuwa mmekufa katika makosa yenu na dhambi, ambazo katika hizo wakati mmoja mlitembea kulingana na mfumo wa mambo wa ulimwengu huu, kulingana na mtawala wa mamlaka ya hewa, roho ile inayotenda kazi sasa katika wana wa kutokutii.”—Waefeso 2:1, 2, NW.

      3, 4. (a) Ni nani “mtawala wa mamlaka ya hewa”? (b) Kwa sababu gani ile “hewa” ya Waefeso 2:1, 2 (NW) si kao la mashetani?

      3 “Hewa” hiyo ni nini? Paulo anaonyesha kwamba ina “mamlaka” au uwezo na kuna “mtawala” juu yayo. Hakuna shaka mtawala huyo ni naini. Yeye ni Shetani Ibilisi, yule ambaye Yesu Kristo aliita “mtawala wa ulimwengu huu.” (Yohana 12:31, NW) Kwa kutambua hivyo, wanachuo fulani wa Biblia wanahisi kwamba hapo Paulo aliazima neno la Kiyahudi au la vyanzo vya kipagani akasema juu ya hewa kuwa ndilo kao la mashetani ambao Ibilisi anawaongoza. Tafsiri nyingi za Biblia zinaonyesha maoni hayo. Lakini “hewa” hiyo si kitu kile kile kimoja na “mahali pa kimbingu” ambamo “majeshi ya roho waovu” wanakaa.—Waefeso 6:11, 12, NW.

      4 Wakati Paulo alipoandikia Wakristo katika Efeso, Shetani na mashetani walikuwa wangali mbinguni, ingawa walikuwa nje ya upendeleo wa Mungu. Walikuwa hawajatupwa chini kwenye ujirani wa dunia. (Ufunuo 12:7-10) Zaidi ya hilo, hewa inahusiana zaidi na wanadamu kuliko viumbe wa kiroho. Kulingana na hivyo, jamii ya kibinadamu ingehisi matokeo wakati bakuli lile la mwisho la hasira ya Mungu lingemiminwa juu ya “ile hewa.”—Ufunuo 16:17-21, NW.

      5. Ni nini ile “hewa” inayozungumzwa hapa, na ina tokeo gani juu ya watu?

      5 Kwa sababu hiyo, inaonekana kwamba Paulo anatumia hewa halisi, au anga, kufananisha roho ya ujumla, au mwelekeo mkuu wa ubinafsi na kutokutii, inayoonyeshwa na watu waliotengwa mbali na urafiki wa Mungu. Roho hiyo ni kitu kile kimoja na “roho ile inayotenda kazi sasa katika wana wa kutokutii” na “roho ya ulimwengu. (Waefeso 2:2:1 Wakorintho 2:12, NW) Sawa na vile hewa. ..halisi ilivyo kila mahali, ikiwa tayari kupumuliwa, hivyo ndivyo “roho ya ulimwengu” ilivyopo sikuzote. Kutoka utoto mchanga mpaka kaburini, roho hiyo inawaenea watu, inakuwa na mavutano juu yao, inafanyiza njia yao ya kufikiri na kutenda wanapotafuta kutimiza tamaa, matumaini, na kutaka makuu kwao.

      6. (a) Nguvu za “hewa” ya ulimwengu huu zinazidishwaje, nayo inatumiaje “mamlaka”? (b) Kupumua “hewa” hiyo kunavutaje mtu aige mwendo wa uasi wa Ibilisi?

      6 Roho hiyo ya udhambi na uasi ina nguvu nyingi katika jamii isiyokamilika ya kibinadamu. “Hewa” hiyo inapopumuliwa, nguvu zayo za kuua zinaongezewa na mikazo rika na hamu yenye kuongezeka daima ya kutaka kufurahisha nyege. Hivyo, hewa hiyo ina “mamlaka” kubwa juu ya watu. (Linganisha Warumi 6:12-14.) Ibilisi ndiye mwanzishi wa maovu yote. (Yohana 8:44) Kwa hiyo, yeye anavuta wanadamu waige mwendo wake mwenyewe wa uasi na kwa njia hiyo anaipulizia, kufanyiza, na kuiongoza roho au “hewa” hiyo ya kijumuiya. Akiwa ndiye “mtawala” juu ya uwezo au “mamlaka” hiyo mbovu, Shetani anaitumia kuongoza kufikiri kwa watu. Mambo yaliyo katika hewa hiyo yanafanyizwa ili kuendeleza watu wakiwa na shughuli nyingi sana za kutosheleza tamaa za kimwili na kufuatia mapendezi ya kilimwengu hivi kwamba hawana wakati au elekeo la kupata kujua Mungu na kujiweka chini ya uongozi wa roho takatifu yake, ‘roho ile itiayo uzima.’ (Yohana 6:63) Kwa usemi wa kiroho, wao ni wafu.

      7. (a) Ni kwa njia gani Wakristo walikuwa “watoto wa ghadhabu” wakati mmoja? (b) Tulipokwisha kuwa Wakristo, ni mgeuzo gani uliotukia?

      7 Wakristo pia walikuwa chini ya “mamlaka,” au uongozi, wa “hewa” hii iliyochafuliwa kabla ya kujifunza ukweli wa Neno la Mungu na kuanza kujipatanisha na viwango vyake vya uadilifu. “Ndivyo, kati yao wakati mmoja sote tulijiendesha kwa kupatana na tamaa za mwili wetu, tukifanya mambo yanayotakwa na mwili na mawazo, nasi kwa asili tulikuwa watoto wa ghadhabu hata kama walivyo wengine.” Lakini baada ya kuwa Wakristo, tuliacha kuipumua “hewa” yenye kuleta kifo ya ulimwengu huu. ‘Tuliuvua utu wa kale unaofanana na mwenendo wetu wa zamani tukauvaa utu mpya ulioumbwa kulingana na mapenzi ya Mungu katika uadilifu wa kweli na ushikamanifu.’—Waefeso 2:3; 4:22-24, NW.

      8. Hali yetu leo inafananaje na ile ya taifa la Israeli jangwani?

      8 Sasa hatari ni kwamba baada ya kuponyoka kutoka anga iliyochafuliwa ya ulimwengu huu huenda tukashawishwa kurudi humo. Tumekwisha kuingia kwa kina kirefu katika “wakati wa mwisho” na tupo penye ukingo kabisa wa ulimwengu mpya. (Danieli 12:4) Kwa uhakika, hatutaki kushindwa kwa sababu ya kutumbukia katika mitego ile ile walimotumbukia Waisraeli. Baada ya wao kukombolewa kimwujiza kutoka Misri na walikuwa wamewasili kwenye mpaka wa Nchi ya Ahadi, maelfu “waliangamizwa jangwani.” Kwa sababu gani? Kwa sababu walikuja kuwa waabudu sanamu, wengine wakafanya uasherati, na bado wengine wakamtia Yehova kwenye jaribu kwa kunung’unika na kulalamika kwao. Paulo anaonyesha jambo moja lenye nguvu akisema: “Sasa mambo hayo yaliendelea kuwapata kuwa mifano, nayo iliandikwa kuwa onyo kwa sisi ambao juu yetu miisho ya mifumo ya mambo imewasili.”—1 Wakorintho 10:1-11, NW.

      9. (a) Tunaweza kuwaje katika ulimwengu na bado tusiwe sehemu yao? (b) Ni lazima tuwe nini ili tuepuke kufyonzwa kurudishwa ndani ya ile anga yenye kuleta kifo ya ulimwengu?

      9 Kwa habari ya wanafunzi wake, Yesu alisali hivi: “Wao si sehemu ya ulimwengu, sawa na vile mimi nisivyo sehemu ya ulimwengu. Mimi nakuomba, usiwaondoe katika ulimwengu, bali uwalinde kwa sababu ya yule mwovu.” (Yohana 17:14, 15, NW) Yehova atatupa sisi kinga salama, lakini yeye haweki “ukingo” kutuzunguka, wala hatuwekei kimuujiza ngao ya kutuzuia na “hewa” ya ulimwengu huu. (Ayubu 1:9, 10) Kwa hiyo, tatizo lile linalotukabili ni kuwa katika ulimwengu wa Shetani bado tusiwe sehemu yao, kuzungukwa na “hewa” yao iliyochafuliwa bado tusiipumue. Wakati sisi tunaposoma vichapo vya habari za kilimwengu, tunapotazama televisheni, au tunapoenda mahali-mahali pa vitumbuizo, inaelekea tutakuwa tunaletwa nje kwenye “hewa” ya ulimwengu. Ingawa haiepukiki kuwa na mkaribiano wa kadiri fulani pamoja na walimwengu—kazini, shuleni, na kwingeneko—ni lazima sisi tuwe macho tusije tukafyonzwa kwa kurudishwa ndani ya anga yenye kuleta kifo ya ulimwengu huu.—1 Wakorintho 15:33, 34.

      10, 11. (a) Kuwa kwetu katika paradiso ya kiroho ya Yehova kungeweza kulinganishwaje na kukaa katika eneo linalosemwa “hakuna kuvuta sigareti”? (b) Ni hatua gani zinazopaswa kuchukuliwa ikiwa mipumuo ya “hewa” ya ulimwengu huu inagunduliwa?

      10 Tunaweza kulinganisha hali yetu na kuketi katika mkahawa wenye maeneo yaliyoandikwa “kuvuta sigareti” na “hakuna kuvuta sigareti.” Kwa kuwa sisi ni Wakristo katika paradiso ya kiroho ya Yehova, kwa kufaa tumo katika sehemu ile ya “hakuna kuvuta sigareti” mbali na roho ya ulimwengu huu. Kwa hakika, sisi kwa makusudi hatungeketi katika sehemu ile ya “kuvuta sigareti.” Huo ungekuwa upumbavu. Lakini ni jambo gani linalotukia mara nyingi wakati sisi tunapokuwa katika sehemu ile ya “hakuna kuvuta sigareti” ya mkahawa? Hewa ile chafu-chafu iliyojazwa moshi inapeperushwa mahali tulipo, nasi tunapata mipumuo yayo! Wakati jambo hilo linapotukia, je! tunaikuta hewa hiyo iliyochafuliwa kuwa yenye kushawishi? Au, badala ya hivyo hatuondoki ilipo kwa haraka tuwezavyo?

      11 Lakini unafanya nini wakati mipumuo ya “hewa” ya ulimwengu huu inapokuja mahali ulipo?.Je! unachukua hatua bila kukawia uondoke kwenye mavutano hayo machafu? Ukikaa hapo na kuyapumua, uwe na uhakika kwamba kufikiri kwako kutaathiriwa. Kwa kadiri unavyozidi kupumua “hewa” hiyo, ndivyo unavyozidi kujenga nguvu za kuivumilia. Zaidi ya hilo, baada ya muda mnuko ule hauwi tena wa kukuchukiza bali unakuwa wa kuvutia. wa kulevya, na wenye kutamanika kwa mwili. Huenda ukazidisha sana tamaa fulani ya siri ambayo umekuwa ukipigana nayo kuizuia.

      12. Ni jambo gani linalotakwa ili kuepuka kuathiriwa na pande zile za “hewa” ya ulimwengu huu ambazo hazigunduliwe kwa urahisi?

      12 Vichafuzi fulani vyenye kuleta kifo vya “hewa” ya ulimwengu huu havigunduliwi kwa urahisi, kama vile vichafuaji vya hewa halisi kaboni monoksaidi visivyo na harufu na ladha. Basi, hatari ni kwamba, huenda tusiigundue ile ‘mivukizo yenye kufisha’ mpaka inapokuwa imetulemea. Hivyo, tunahitaji kuwa chonjo kwamba tusiongozwe ndani ya mtego wa kifo na mielekeo ya uendekevu ya ulimwengu huu au kutokutii kwao viwango vya Mungu vya uadalifu. Paulo aliwatia moyo Wakristo wenzake “mwendelee kushauriana kwa bidii mtu na mwenzake kila siku . . . kwa kuogopa ye yote kati yenu asije kufanywa mgumu na uwezo ule wenye kudanganya wa dhambi.”—Waebrania 3:13; Warumi 12:2, NW

      Ni Mambo Gani Yanayojumlika Pamoja Kuwa “Hewa” ya Ulimwengu Huu?

      13. (a) Ni nini namna moja ya “hewa” ya ulimwengu huu tunayopaswa kujikinga dhidi yayo? (b) Inaonekanaje kwamba “hewa” hiyo imeathiri wengine wa watu wa Yehova?

      13 Ni mielekeo gani inayopatikana kwa wingi ambayo huenda sisi tukaanza kufuata, hata kabla hatujatambua hivyo, kwa sababu ya mavutano yenye nguvu ya “hewa” ya ulimwengu huu? Mmoja ni ule mwinamio wa kucheza na mambo yasiyo ya adili. Mawazo ya ulimwengu huu juu ya ngono na tabia za kiadili yanatuzunguka kila mahali. Wengi wanasema: ‘Ni sawa tu kufanya uasherati, kuzaa watoto nje ya kifungo cha ndoa, na kuzoea ugoni-jinsia-moja. Sisi tunafanya tu jambo lililo la kawaida, la asili.’ Je! “hewa” hii, au roho ya ulimwengu, imeathiri watu wa Yehova? Jambo la kusikitisha ni kwamba wakati wa mwaka wa utumishi wa 1986, ilikuwa lazima watu 37,426 watengwe na ushirika wa kundi la Kikristo, hesabu kubwa zaidi kati yao ikiwa ni kwa sababu ya kuzoea ukosefu wa adili katika ngono. Na hiyo haitii ndani hesabu iliyo kubwa hata zaidi ya waliokaripiwa kwa ukosefu wa adili lakini wasitengwe na ushirika kwa sababu wao walitubu kwa moyo mweupe.—Mithali 28:13.

      14. Kwa sababu gani Wakristo fulani wanakengeuka kiadili, nao wanakataa shauri gani la Kimaandiko?

      14 Inatukia nini katika kisa cha wale wanaojiacha washindwe na ukosefu wa adili katika ngono? Wakati mambo ya uhakika yanajulikana, mara nyingi inakutwa kwamba wao wamerudia kuipumua “hewa” ile yenye kuleta kifo ya ulimwengu huu. Wao wameacha mielekeo ya kilimwengu iwafanye washushe viwango vyao. Kwa mfano, huenda wao wakaanza kutazama sinema ambazo miaka mingi mapema wao wangaliziondokea. Ubaya unaozidi huo ni kwamba, huenda wao wakatazama katika vifaa vya kinyumbani vya vidio sinema ambazo kwa wazi hazimfai Mkristo. Kucheza-cheza hivyo pamoja na mambo ya ukosefu wa adili kunalipinga moja kwa moja agizo hili la Kimaandiko: “Acheni uasherati na ukosefu wa usafi wa kila namna au kuwa na pupa hata yasitajwe miongoni mwa ninyi, sawasawa na vile iwafaavyo watu watakatifu; wala mwenendo wenye aibu wala maongezi ya upumbavu wala mzaha wa mambo machafu.”—Waefeso 5:3, 4, NW.

      15. Ni jinsi gani kishawishi cha kucheza-cheza na ukosefu wa adili katika ngono kingeweza kuanza hivi hivi tu?

      15 Ni kweli kwamba huenda wewe ukakataa kwa haraka mnuizo wo wote wa waziwazi wa kufanya uasherati. Lakini wewe umetendaje wakati mtu fulani kazini au shuleni anapojaribu kukufanyia utani wa kimapenzi, akijaribu kukuzoea-zoea kupita kiasi kimwili, au akikualika mwende nje kufanya matembezi? Mipumuo ya “hewa” ya ulimwengu huu inakuwa imepeperuka kuja ulipo wewe. Je! wewe unajiruhusu ufurahie fikira hizo unazoelekezewa, kutia moyo jambo hilo? Kulingana na ripoti zilizopokewa kutoka kwa wazee, mara nyingi kufanya makosa kunaanza kwa njia hizo za hivi hivi tu. Huenda mwanamume mlimwengu akaambia mwanamke Mkristo hivi: “Lo, leo una sura nzuri kama nini!” Huenda ikafurahisha kusikia hivyo, hasa ikiwa mwanamke yule anahisi kidogo akiwa mpweke. Jambo zito zaidi ya hilo, wengine hawakutenda kwa hekima walipofanyiwa majaribio ya kuguswa-guswa isivyofaa. Wao wamejifanya ni kana kwamba wanakataa lakini kwa njia ya moyo nusu-nusu sana hata mlimwengu yule akatiwa moyo kuendelea na jambo alilokuwa akifanya. Namna gani kama matongozi yale ya ukosefu wa adili kuelekea mwanamke Mkristo yangeendelea, kama mipulizo yenye nguvu ya hewa iliyochafuliwa yenye kuelekezwa kwake? Inampasa yeye amwambia mtu huyo kwa imara kwamba yeye hataki na hatakubali fikira anazomwelekezea. Mwanamke yule akiendelea kuipumua “hewa” hiyo, upingaji wake utaelekea kubomoka-bomoka. Angeweza kuongozwa aingie katika ukosefu wa adili, ikiwa si katika ndoa isiyo ya hekima.—Linganisha Mithali 5:3-14; 1 Wakorintho 7:39.

      16. Ni jambo gani linilotakwa ili kuwa “manukato ya Kristo”?

      16 Basi, uwe mwenye haraka kuikataa “hewa” isiyo ya adili, yenye kuleta kifo, ya ulimwengu huu. Badala ya kujiacha ufuate harufu yayo yenye kuvuta na kuleta suto juu ya jina na tengenezo la Yehova, na uwe harufu ya kupendeza Mungu kwa mwelekeo na mwenendo wako wa kumtii yeye. Paulo alieleza jambo hilo hivi: “Kwa maana sisi tu manukato ya Kristo, mbele za Mungu, katika wao wanaookolewa, na katika wao wanaopotea; katika hawa wa pili harufu ya mauti iletayo mauti; katika hawa wa kwanza harufu ya uzima iletayo uzima.” (2 Wakorintho 2:15, 16) Si kitu hata kama wengi watakunja pua zao kwa kuudharau mwendo huo wa Kikristo. (1 Petro 4:1-5) Acha ulimwengu uendelee kufuata njia yao, ukivuna matunda yao mabaya kwa namna ya nyumba zilizovunjika-vunjika, uzazi wa watoto haramu, magonjwa yenye kuambukizwa kingono, kama vile UKIMWI, na ole mwingine usiohesabika wa maono ya kimoyo na kimwili. Wewe hutaepushwa na maumivu mengi tu bali utapata pia upendeleo wa Mungu. Zaidi ya hilo, angalau watu fulani watavutwa na mwenendo wako mwema na ujumbe wa Ufalme unaohubiri, kwa njia hiyo wavutwe na ile “harufu ya uzima iletayo uzima.”

      “Hewa” ya Mitindo ya Kilimwengu

      17. Mitindo ya kuvalia na kujipamba huenda ikafunuaje kwamba mtu amevutwa na roho ya ulimwengu huu?

      17 Upande mwingine wa “hewa” ya ulimwengu huu unahusu mitindo ya kuvalia na kujipamba. Watu wengi katika ulimwengu wanavaa ili wajifanye kuwa wenye kuvutia kingono. Hata vijana wasiofikia umri wa miaka 13 wanataka kujifanya waonekane wenye umri mkubwa zaidi, ili wavute fikira kwenye mambo ya ngono. Je! wewe umeambukizwa na “hewa” au mwelekeo huo ulioenea pote? Je! wewe unavalia ili usisimue, uchokoze-chokoze, uamushe isivyofaa upendezi wa wale wa jinsia tofauti? Ikiwa ndivyo, wewe unacheza na moto. Kuipumua “hewa” hiyo kutaikaba roho yako ya kiasi, tamaa yako ya kuwa safi kiadili. (Mika 6:8) Wale wenye roho ya kilimwengu watavutwa kwako. Kutokana na vitendo vyako, wao wataupata ujumbe wa kwamba wewe uko tayari kujiunga nao katika ukosefu wa adili. Lakini mbona uanza kuelekea upande huo kwa kuacha “hewa” kama hiyo ikushawishi kufanya lililo baya machoni pa Mungu?

      18. Kukumbuka sikuzote kwamba sisi tunawakilisha Yehova kutatusaidiaje katika kuchagua mitindo ya mavazi na kujipamba?

      18 Ili tuwe wenye kiasi, si lazima tuvalie au tujipambe ovyo-ovyo tu au kwa njia isiyovutia. Fikiria njia ile ambayo walio wengi sana wa Mashahidi wa Yehova wanavalia na kujipamba. Wao wanaiepuka mitindo ya kupita kiasi ya ulimwengu huu lakini wanajitokeza mbele ya watu kwa njia ya kuvutia, wakizingatia kwamba wao ni wahudumu wanaomwakilisha Mwenye Enzi Kuu wa ulimwengu wote mzima, Yehova. Acha ulimwengu wa kale uwe mchambuzi juu ya mitindo yenye kiasi ya wahudumu hao. Wao hawathubutu kuiacha mielekeo ya ulimwengu huu iwafanye washushe viwango vyao vya Kikristo. “Kwa hiyo, nasema hivi na kushuhudia katika Bwana,” akaandika mtume Paulo, “kwamba ninyi msienende tena kama yaendavyo mataifa pia katika mambo yasiyo na faida ya akili zao . . . Kwa kuwa walikuwa wamekuja kupita hisi ya kiadili yote wao walijitoa wenyewe upande ule mwingine kwenye mwenendo mlegevu wafanye ukosefu wa usafi wa kila namna.” (Waefeso 4:17-20, NW) Mkristo aliye mkomavu atavalia kwa kiasi, asitembee sawasawa na yanavyofanya mataifa.—1 Timotheo 2:9, 10.

      19. Baada ya kufikiria pande mbili kubwa za “hewa” ya ulimwengu huu, tayari ni jambo gani linaloonekana juu ya hatari ya kuivuta?

      19 Kufikia hapo, tumefikiria pande mbili tu za ile “hewa” ya ulimwengu huu. Lakini tayari tumekwisha kuona kwamba “hewa” hiyo ni yenye madhara sana kwa afya ya kiroho. Katika makala inayofuata, tutasonga tuzungumzie sehemu nyingine za “hewa” hiyo yenye kufisha ambayo Ibilisi na mfumo wake anaendelea kupulizia Wakristo, akitumaini kwamba wao watajiacha washindwe nayo. Ni jambo la maana kama nini tuepuke “hewa” kama hiyo kwa maana kuvuta roho ya ulimwengu huu ni kama kupumua mivuke ya kifo!

  • Endelea Kujiweka Chini ya Uongozi wa ‘Ile Roho Itiayo Uzima’
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Septemba 15
    • Endelea Kujiweka Chini ya Uongozi wa ‘Ile Roho Itiayo Uzima’

      “Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu.”​—YOHANA 6:63.

      1. (a) Yehova anasaidiaje watu wake wapinge mavutano ya “hewa” ya ulimwengu huu? (b) Kusitawisha tunda la roho ya Mungu kutatusaidiaje tuwe na mwinamio wa kiakili unaofaa?

      ROHO takatifu ya Yehova Mungu inahitajiwa kwa umuhimu ikiwa sisi tutayapinga mavutano ya “hewa” ya ulimwengu huu, au mielekeo yao. (Waefeso 2:1, 2, NW) Tunaihitaji Biblia pia, ambayo ina fikira za Mungu zilizoandikwa chini ya mwongozo wa roho takatifu. Na tunahitaji kuwa na mwelekeo wa unyenyekevu wa Kikristo, unaotokezwa kwa kusitawisha matunda ya roho ya Mungu—“upendo, furaha, amani, ustahimilivu, fadhili, wema, imani, upole, kujiweza.” Mtume Paulo alihimiza hivi: “Endeleeni kutembea kwa roho na ninyi hamtatimiza tamaa ya kimwili hata kidogo. Kwa maana mwili unapinga roho katika tamaa yao, nayo roho inapinga mwili; kwa maana hivyo viwili vinapingana, hata mambo yale mngependa kuyafanya hamyafanyi.”—Wagalatia 5:16, 17, 22, 23, NW.

      2. Mambo yanayotokezwa na roho ya Mungu yanatofautianaje na matokeo ya kuchagua kuifuata “roho ya ulimwengu”?

      2 Paulo aliandika hivi pia: “Tulipokea, si roho ya ulimwengu, bali roho inayotoka kwa Mungu, ili tupate kujua mambo ambayo kwa fadhili tumepewa na Mungu.” (1 Wakorintho 2:12, NW) “Hewa,” au mwelekeo wa kiakili, wa ulimwengu huu unaua, lakini kile ambacho Mungu anatoa kupitia roho takatifu kinawaletea uzima wa milele wale wanaokikubali. Yesu alisema: “Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; maneno hayo niliyowaambia ni roho, tena ni uzima.” (Yohana 6:63) Kwa kuwa mwili haufai kitu, sisi tunahitaji msaada wa kimungu ili kushinda dhambi na kuipinga roho ya ulimwengu.

      3, 4. (a) Pupa ni nini, na ‘mtawala wa hewa’ anachochea-chocheaje tamaa ya mwili ya kutaka vitu vya kimwili? (b) Ni jinsi gani mtu mwenye pupa ni mwabudu sanamu?

      3 Katika makala iliyotangulia, tulizungumzia pande mbili hatari za “hewa” ya ulimwengu huu—kucheza-cheza na mambo yasiyo ya adili na mitindo isiyofaa ya mavazi na mapambo. Lakini kuna pande nyingine nyingi. Kwa mfano, anga ya ulimwengu huu imejawa na pupa, na tamaa nyingi sana ya ubinafsi ya kutaka mazidio au vitu vya kimwili. ‘Mtawala wa hewa’ amehakikisha kwamba maenezi ya porojo za ulimwengu huu na utangazaji wao yanakufanya wewe uhisi hujatimiza mambo yako ikiwa huna wingi wa mali za kimwili. Upande huu wa “hewa” ya ulimwengu unaweza kukulewesha kwa wazo la kwamba haya ndiyo mambo makubwa maishani. Je! wewe umeambukizwa na “hewa” hiyo ya ufuatiaji vitu vya kimwili?

      4 Biblia inasema: “Hakuna mwasherati au mtu mchafu au mtu mwenye pupa—maana yake kuwa mwabudu sanamu—aliye na urithi wo wote katika ufalme wa Kristo na wa Mungu.” (Waefeso 5:5, NW) Angalia hapa kwamba kwa kweli mtu mwenye pupa ni mwabudu-sanamu. Huenda ukafikiri ‘Kwa uhakika, mimi sitafikia umbali huo, kuwa mwabudu sanamu.’ Lakini ibada ya sanamu ni nini? Je! si kuweka kitu kingine cho chote katika mahali pa Yehova na ibada yake, kukipa kitu hicho fikira badala ya kumpa Mungu na utumishi wake? Huenda ikatia ndani ibada halisi ya pesa na uwezo na mavutano zilizo nayo. Ukitanguliza kupata motokaa mpya, kaseti rekoda au vidyo, au kitu kingine cho chote cha kimwili mbele ya kuongeza nafasi zako katika utumishi wa Yehova, je! huo si ushuhuda wa kwamba “hewa” ya ulimwengu huu inakuathiri wewe? Je! hapo vitu vya kimwili haviwi kama sanamu za ibada kwako?

      5. Ni kwa njia gani “hewa” ya ulimwengu huu imejawa na tamaa ya ubinafsi ya kutaka mali?

      5 Ikiwa wewe unatafuta elimu ya juu zaidi au kazi yenye pesa nyingi, je! unafanya hivyo ili uwe tajiri na upate mazidio ya vitu vya kimwili kuliko vile unavyovihitaji? Je! upendezi wako unaamshwa na njama za kutajirika upesi? Kutaka kuhusika katika hizo? “Hewa” ya ulimwengu huu imejawa na tamaa ya ubinafsi ya kutaka utajiri na kupunja kwa habari ya ulipaji kodi unaopasishwa na serikali. Katika hali hiyo ya anga mchezo wa kamari na utendaji mwingine unaofanana na huo unasitawi sana. Usishawishwe. Wale wanaoepuka mavutano ya “hewa” ya ulimwengu huu uliolemewa na pupa wanakuta kwamba furaha ya kweli inatokana na kuridhika na mahitaji yaliyo ya lazima na kuweka masilahi ya Ufalme kwanza.—Mathayo 6:25-34; 1 Yohana 2:15-17.

      Utumizi Unaofaa wa Ulimi

      6. Ni tokeo gani ambalo tabia za usemi za ulimwengu huu zinaweza kuwa nalo juu yetu sisi Wakristo?

      6 Namna gani juu ya tabia za usemi zetu? Misemo michafu, maneno ya hasira, kusema uwongo—“hewa” ya ulimwengu huu imechafuliwa kweli kweli na usemi mchafu-mchafu kama huo. Na bado, nyakati nyingine hata usemi wa watu wachache wanaoshirikiana na kundi la Kikristo unakuwa na ushenzi, hata utovu wa adabu. Mwanafunzi Yakobo anatuambia hivi kwa mkazo mwingi: “Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo. Je! chemchemi katika jicho moja hutoa maji matamu na maji machungu?” (Yakobo 3:10, 11) Je! wewe umeokota kadiri fulani ya mborongoborongo au maneno ya vichochoroni ya ulimwengu huu? Je! wewe una mafungu mawili ya misamiati, moja la kutumia miongoni mwa Wakristo, lile jingine la kutumia mahali penginepo? Paulo aliandika: “Neno lo lote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa wenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia.” (Waefeso 4:29) Ni jambo la maana kama nini kutumia usemi unaofaa ulio safi wakati wote!

      7. Ni nini linalotiwa ndani ya ‘kuondolea mbali uwongo na kusema ukweli’?

      7 Tunahitaji pia kuwa waangalifu kwamba sikuzote tunasema ukweli. Kwa kweli, kusema mambo kwa vipengee au kueleza wengine mambo yaliyopotoshwa kwa makusudi ili kuepuka daraka la kulaumiwa ni sawa na kusema uwongo. Kwa hiyo hakikisha kwamba unatii shauri la Paulo: “Kwa kuwa mmeondolea mbali uwongo, semeni ukweli kila mmoja wenu na jirani yake, kwa sababu sisi kila mtu ni kiungo cha mwenzake.”—Waefeso 4:25; Mithali 3:32, NW.

      8. (a) Walimwengu wengi wanatendaje hasira yao inapoamshwa? (b) Hasiri yetu ikiamshwa, ni jambo gani ambalo imetupasa sisi kufanya?

      8 Kufungulia hasira bila kizuizi ni sehemu nyingine ya roho ya ulimwengu huu. Walimwengu wengi wanapoteza kujiweza kwa urahisi. Wanafoka kwa hasira, ndipo wanapojitolea udhuru kwa kusema walikuwa ‘wakibwaga moyo tu.’ Lakini hivyo sivyo Paulo alivyoshauri, kwa maana yeye aliandika: “Uchungu wote na ghadhabu na hasiri na kelele na matukano yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya.” (Waefeso 4:31) Lakini namna gani ikiwa hasira inajazana ijapokuwa sisi tumekuza kujiweza na matunda mengine ya roho ya Mungu. “Mwe na hasira, ila msitende dhambi,” akaandika Paulo. “Jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; wala msimpe Ibilisi nafasi.” (Waefeso 4:26, 27) Hivyo, hasira yetu ikichochewa, inatupasa tumalize jambo lile kwa haraka, kabla ya siku kuisha. Ama sivyo, uchungu na mfundo unaanza kutia mizizi katika moyo, na yanakuwa mambo magumu kung’oa. Usijiruhusu mwenyewe uvute “hewa” yenye hasira, ya kulipa kisasi ya ulimwengu huu!—Zaburi 37:8.

      9. Ni nini baadhi ya mielekeo ya waajiriwa-kazi inayopatikana kwa wingi, na kwa sababu gani inatupasa tuchunguze tabia za kazi zetu?

      9 Namna gani juu ya tabia za kazi zako? Kukaa-kaa tu bila kufanya kazi na kuiba vitu kutoka kwa mwajiri-kazi ni mambo yanayofanywa kwa wingi leo. Je! wewe umefyonza kadiri fulani ya “hewa” hiyo? Je! wewe umepakwa ule mwelekeo wa kwamba ‘kila mtu hufanya jambo hilo’? Usisahau kwamba jinsi sisi tunavyofanya kazi yetu tukiwa Wakristo inaleta sifa ya namna fulani juu ya Yehova na ibada yake ya kweli. Je! wewe ungetaka mtu fulani aukatae ukweli unaosemwa na mmoja wa Mashahidi wa Yehova mlangoni pake kwa sababu ya jinsi wewe unavyotenda kazini? “Mwibaji asiibe tena,” akasema Paulo, “bali afadhali afanye juhudi. . . apate kuwa na kitu cha kumgawia mhitaji.”—Waefeso 4:28.

      10. Katika kufanya kazi ya kimwili, tunaweza kuonyeshaje kwamba sisi hatuathiriwi na “hewa” ya ubinafsi ya ulimwengu huu?

      10 Ingawa uhusiano wa bwana-mkubwa na mtumwa wake uliokuwako katika karne ya kwanza haupatikani sana leo, waajiriwa-kazi Wakristo wanaweza kujifunza kutokana na mambo ambayo Paulo aliwaandikia watumwa Wakristo katika Waefeso 6:5-8. Hapo wafanya kazi waliambiwa ‘watii wale ambao walifanyia kazi, si kama wajipendekezao kwa wanadamu tu, bali, kama watumwa wa Kristo.’ Kwa hiyo, haimpasi kamwe Mkristo kutunga mbinu za kuepuka kufanya siku kamili ya kazi au kufanya uandalizi wa bidhaa au utumishi alioahidi. Tukifanya mambo ‘kama kumtumikia Yehova,’ tutakuwa na mwelekeo unaofaa na hatutaathiriwa na “hewa” ya ubinafsi na uvivu ya ulimwengu huu.

      Chakula, Kinywaji, na Vitumbuizo

      11. Mwelekeo wa kilimwengu juu ya chakula na kinywaji uliathirije wengine wa watu wa Yehova katika nyakati za Biblia?

      11 Je! utumizi usio wa kiasi wa chakula na kinywaji wa ulimwengu umekuathiri wewe? Mwelekeo wao ni ‘tule, tunywe, na kufanya furaha, kwa maana kesho huenda tukafa.’ (1 Wakorintho 15:32) Na roho hiyo imeathiri watu fulani kati ya watumishi wa Mungu, hata tangu nyakati za kale. Kumbuka pindi ile katika jangwa ambapo Waisraeli “waliketi, wale na kunywa. Ndipo wakainuka ili wawe na wakati mzuri.” (Kutoka 32:6, NW) “Wakati mzuri” huo uliongoza kwenye mwenendo mlegevu usiozuiwa na kwenye ibada ya sanamu, hivi kwamba hasira ya Mungu iliwaka dhidi yao. Acheni sisi tusifuate kamwe mwendo huo.​—1 Petro 4:3-6.

      12. Ikiwa tabia zetu za kula na kunywa zinahitaji kuelekezewa fikira fulani, inatupasa sisi tufanye nini?

      12 Yehova ametupa sisi namna nyingi sana za vyakula na vinywaji vyenye ladha nzuri, vya kupendeza, na vyenye kujenga mwili, lakini yeye anatutaka tutumie vitu hivyo kwa kiasi. Ulafi na ulevi ni mambo yanayokatazwa katika Biblia. (Mithali 23:20, 21) Kwa hiyo, uwe mnyofu na ujiulize mwenyewe hivi: Je! pana nafasi ya kufanyia maendeleo katika tabia zangu za kula na kunywa? Ikiwa unahitaji kujizoeza kujiweza kwa kadiri kubwa zaidi, tambua jambo hilo na kujitahidi kupatana na sala zako za kuomba roho ya Mungu ikusaidie ushinde tatizo hilo. “Msiwe mkilewa divai, ambamo mna upotovu, bali endeleeni kujazwa roho,” akasema Paulo. (Waefeso 5:18, NW) Ndiyo, ujazwe roho ya Mungu, na usijiache uifuate roho isiyozuiwa ya ulimwengu huu! “Kwamba mnakula au mnakunywa au mnafanya jambo jinginelo lote, fanyeni mambo yote kwa utukufu wa Mungu.” (1 Wakorintho 10:31, NW) Hata hivyo, ikiwa wewe una matatizo yasiyoisha kuhusiana na mambo hayo, tafuta msaada wa wanaume wakomavu kiroho katika kundi.—Wagalatia 6:1; Yakobo 5:14, 15.

      13. (a) Ni jinsi gani kuna ushuhuda wa kwamba Ibilisi ametia ufisadi katika vingi vya vitumbuizo vinavyopatikana leo? (b) Tunaweza kuepukaje mwelekeo wa ulimwengu huu juu ya vitumbuizo?

      13 Ulimwengu huu umeingiwa sana na uzoevu wa michezo, muziki, namna mbalimbali za vitumbuizo. Isipokuwa yanavunja kanuni za Kimaandiko, kufurahia mambo kama hayo si kubaya kwa lazima. Lakini tatizo ni kwamba Shetani, “yule mtawala aliye gavana wa hewa,” ametia ufisadi katika vingi vya vitumbuizo vinavyopatikana leo. (Waefeso 2:2, The Jerusalem Bible) Mara nyingi, ukosefu wa adili unatiliwa nguvu, jeuri inaachiliwa kama si kitu, na mafanikio yanayopatikana kupitia kudanganya, kupunja, na hata kuua yanaonyeshwa. Tunapotazama vitumbuizo kama hivyo, tunapumua mielekeo hiyo na kuiingiza kwa kina kirefu katika mfumo wa mwili wetu, na sumu zayo zitatudhuru bila shaka. Zaidi ya hilo, hata wakati namna fulani za vitumbuizo haikataliki Kimaandiko, kuna hatari ya kuvizoelea, hivi kwamba wakati mdogo ndio unaobaki kwa mambo ya kiroho. Kwa sababu hiyo, tunahitaji kuwa wachaguzi. Tumia wakati fulani kufurahia kwa kiasi starehe fulani yenye afya na manufaa, lakini epuka kuiga mambo ya ulimwengu yanayopita kadiri. Kama “hewa” ya ulimwengu huu inanukia vizuri au inawasha pua, bado imechafuliwa na ni ya kufisha!—Mithali 11:19.

      Kiburi cha Kabila—Upepo Mwovu

      14. Kwa habari ya matatizo ya kijamii, sisi tungeweza kuathiriwaje na “hewa” ya ulimwengu huu?

      14 Upande wa “hewa” ya ulimwengu huu ambao kidogo ni kama hauonekani wazi sana ni kiburi cha kabila na utaifa. Watu fulani wanalitilia nguvu wazo lenye makosa kwamba makabila fulani ni bora na mengine ni duni. Utukuzo wa taifa unatia watu moyo waione nchi yao ya kienyeji kuwa bora kuliko nyinginezo. Kwa kweli, watu wengi wanataabika bure na kunyimwa haki za msingi za kibinadamu na mahitaji ya lazima kwa sababu ya ubinafsi na ubaguzi wa wengine. Kwa sababu hiyo kunatokea mfundo wa moyoni, hata jeuri. Wengi wanainuka katika uasi, wakichukua sheria mikononi mwao, wakiwa na uhakika wa kutatua matatizo ya kijamii kwa njia yao wenyewe. Sisi, pia, huenda tukanaswa katika mawazo hayo. Tunapoona matendo yasiyo ya haki yakifanywa au tunapopatwa nayo halafu kuwasikia wale wanaochochea kuwe na badiliko la kijamii, tungeweza kuingizwa mavutano hayo ikiwa sisi si waangalifu. Tungeweza kuanza kuacha msimamo wetu wa kutokuwamo na kujiunga na upande huo au ule. (Yohana 15:19) Jambo zito hata zaidi, huenda sisi tukahisi tukishawishwa kujiunga katika kutia moyo wengine wagomee mipango fulani, kufanya kampeini, au kujiingiza katika jeuri ili kulazimisha mabadiliko.

      15. Ni mwendo gani ambao Biblia inapendekeza wakati sisi tunapohisi tukiwa na mwinamio wa ‘kujilipiza wenyewe kisasi’?

      15 Roho ya kundi inaweza kuathiriwa na hisia za kikabila au za utukuzo wa taifa. (Linganisha Matendo 6:1-7.) Lakini sisi tutakuwa na roho inayofaa tukitii shauri hili: “Ikiwa inawezekana, kwa kadiri ambavyo inawategemea ninyi, iweni wenye kuamanika pamoja na watu wote. Msijilipize wenyewe kisasi, wapendwa, bali iwachieni ghadhabu nafasi ya kupita; kwa maana imeandikwa: ‘Kisasi ni changu; mimi nitarudisha malipo, asema Yehova.’” (Warumi 12:18, 19, NW) Kwa kuwa makabila yote yalitokana na wale watu wawili wa kwanza na Mungu hana upendeleo, hakuna nafasi ya kiburi cha kabila au utaifa katika kundi la Kikristo.—Matendo 10:34, 35; 17:26; Warumi 10:12; Waefeso 4:1-3.

      Endelea Kupumua “Hewa” Itiayo Uzima

      16. Ni jambo gani litakalosaidia kuzuia tusiambukizwe na roho ya ulimwengu huu?

      16 Tumezungumzia sehemu zile kubwa-kubwa zinazoleta kifo za “hewa” au roho ya ulimwengu huu. Hiyo inatuzunguka na kutokeza mkazo mwingi sana hivi kwamba tukiruhusu uwazi fulani utokee katika hali ya kiroho kwa haraka iingie katika uwazi huo na kuujaza. Mafanikio katika kuipinga yanategemea s,ana kadiri ambayo sisi tunapenda mambo yaliyo ya utakato, safi, na ya uadilifu. na kadiri ambayo tunachukia mambo yasiyo ya utakato, yasiyo safi na yenye uovu. Sisi hutaendelea kuipumua “hewa” inayofaa ikiwa tutaendelea kusitawisha mwelekeo wa kiakili unaofaa kwa kuitikia mwongozo wa roho takatifu ya Yehova.—Warumi 12:9; 2 Timotheo 1:7; Wagalatia 6:7, 8.

      17. Ni jambo gani linalopasa kufanywa bila kukawia tukigundua kadiri fulani ya “hewa” ya ulimwengu huu ikielekea mahali tulipo?

      17 Kwa vyo vyote, usiache yo yote ya “hewa” chafu-chafu ya ulimwengu ianze kuwa na unukio wa kukufurahisha wewe. Mtawala wa “hewa” hiyo analijua jambo lile hasa linalohitajiwa ili kuzivuta hisi na kuanzisha tamaa nyingi ambayo mara nyingi inaongoza kwenye dhambi. (Yakobo 1:14, 15) Endelea kukaa katika sehemu ile inayoonyesha “hakuna kuvuta sigareti,” paradiso ya kiroho ya Yehova. Unapogundua mpumuo mmoja wa “hewa” ya ulimwengu huu ukija mahali ulipo uepuke. Geukia kando na mahali ulipo sawasawa na vile ungeepuka sumu yenye kuleta kifo. “Endeleeni kulinda kwa uangalifu sana kwamba jinsi mnavyotembea si kama wasio na hekima bali kama watu walio na hekima, kununua kabisa wakati unaofaa kwa ajili yenu wenyewe. Kwa sababu siku ni zenye uovu. Kwa sababu hiyo acheni kuwa wajinga, bali endeleeni kufahamu yaliyo mapenzi ya Yehova.”—Waefeso 5:15-17. NW.

      18. Ni roho gani watakayokuwa nayo wale watakaopendelewa kuishi katika dunia iliyosafishwa?

      18 Ni mapenzi ya Mungu kwamba sisi tumtumikia yeye tukiwa washika-ukamilifu. Kufanya hivyo kutamaanisha uzima katika mfumo mpya wake, ambao sasa uko karibu sana. Tutakapovuta mpumuo mmoja wa “hewa” ya wakati huo, utakuwa wenye kuburudisha kama nini! Hakutakuwa na vichafuaji vyenye kuleta kifo, ni hewa ya utakato tu yenye kuendeleza uhai. Hivyo ndivyo itakavyokuwa juu ya hewa ile halisi na, jambo la maana zaidi, ndivyo itakavyokuwa roho ya wale waliopendelewa kuishi katika dunia iliyosafishwa. Wao watakuwa wana mwelekeo wa utii, unyenyekevu na wa kuitikia mambo. “Hewa” ya ulimwengu huu wa kale, yenye kujawa na mavutano ya uasi, ya ufisadi na ya kutokutii Mungu itakuwa imetokomea.—Ufunuo 21:5-8.

      19. Ni nani watakaookoka waingie mfumo mpya ya Yehova?

      19 Kwa uhakika, sisi hatutaki kuwa miongoni mwa wale wanaoipumua “hewa” ya mfumo huu wakati ambapo Yehova atakapoondolea mbali uchafuzi na hata wachafuzi wayo kwenye Har–Magedoni. Wakati ulimwengu wa kale utakapokuwa umetokomea na ‘mtawala wa hewa’ awe ametiwa katika lile shimo refu sana, lo, kutakuwako kitulizo kama nini! Kila mtu anayependa Yehova na anayeendelea kutenda yaliyo safi, ya ustahifu, na ya uadilifu atakuwa pale. Yehova anawataka wao wawe pale na atawasaidia kwa roho yake. Yeye atawapa uzima wa milele katika mfumo mpya ulio safi, wenye afya. Sisi na tusilikose pendeleo hilo kwa sababu ya kuvuta “hewa” yenye kuleta kifo ya mfumo huu wa kale!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki