Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Roho
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
    • Kama “mawe yaliyo hai,” walikuwa wakifanyizwa kuwa hekalu la kiroho ambalo msingi wake ni Kristo, na ambalo kupitia hilo “dhabihu za kiroho” zingetolewa (1Pe 2:4-6; Ro 15:15, 16) na nyimbo za kiroho kuimbwa (Efe 5:18, 19) na ambamo Mungu angekaa kupitia roho. (1Ko 3:16; 6:19, 20; Efe 2:20-22; linganisha Hag 2:5.) Roho ya Mungu ni kani yenye kuunganisha iliyo na nguvu kubwa, na maadamu Wakristo hao waliiruhusu iwe na uhuru wa kutembea, iliwaunganisha kwa njia ya amani katika vifungo vya upendo na ujitoaji pamoja na Mungu, Mwanaye, na pamoja na mtu na mwenzake. (Efe 4:3-6; 1Yo 3:23, 24; 4:12, 13; linganisha 1Nya 12:18.) Zawadi ya roho haikuwatayarisha kwa ajili ya shughuli za aina ya kiufundi, kama ilivyofanya kwa Bezaleli na wengine ambao waliunda na kutengeneza miundo na vifaa halisi, bali iliwafanya wafae kwa ajili ya kazi za kiroho za kufundisha, kuongoza, kuchunga, na kushauri. Hekalu la kiroho ambalo wao walilifanyiza lilipaswa kupambwa kwa matunda yenye kupendeza ya roho ya Mungu, na lile tunda la “upendo, shangwe, amani, ustahimilivu, fadhili, wema, imani,” na sifa kama hizo, lilikuwa uthibitisho wa hakika kwamba roho ya Mungu ilikuwa ikitenda ndani yao na miongoni mwao pia. (Gal 5:22, 23; linganisha Lu 10:21; Ro 14:17.) Hilo ndilo lililokuwa jambo la msingi na lililo kuu lenye kutokeza utaratibu mzuri na uongozi wenye matokeo miongoni mwao. (Gal 5:24-26; 6:1; Mdo 6:1-7; linganisha Eze 36:26, 27.) Walijinyenyekeza chini ya “sheria ya ile roho,” ambayo ni kani yenye matokeo kwa ajili ya uadilifu unaofanya kazi ili kuzuia mazoea ya mwili uliorithi dhambi. (Ro 8:2; Gal 5:16-21; Yuda 19-21) Tumaini lao lilikuwa katika roho ya Mungu inayotenda kazi juu yao, wala si katika uweza wao au malezi ya kimwili.—1Ko 2:1-5; Efe 3:14-17; Flp 3:1-8.

  • Hekalu
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
    • Wakristo Watiwa Mafuta​—Ni Hekalu la Kiroho. Wakristo watiwa mafuta walio duniani wanafananishwa na vitu vingi, kutia ndani hekalu. Ufananisho huo unafaa kwa kuwa roho ya Mungu hukaa katika kutaniko la watiwa mafuta. Paulo aliwaandikia Wakristo huko Efeso “katika muungano na Kristo Yesu,” wale ambao “mlitiwa muhuri kupitia . . . kwa roho takatifu iliyoahidiwa,” akisema: “Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ndiye jiwe la msingi la pembeni. Katika muungano naye, jengo lote likiwa limeunganishwa kwa upatano, linakua ili kuwa hekalu takatifu kwa ajili ya Yehova. Katika muungano naye, ninyi pia mnajengwa pamoja muwe mahali pa Mungu pa kukaa kupitia roho.” (Efe 1:1, 13; 2:20-22) Watu hao ‘waliotiwa muhuri,’ wamejengwa juu ya Msingi wa Kristo, idadi yao inatajwa kuwa 144,000. (Ufu 7:4; 14:1) Mtume Petro anawaita ‘mawe yaliyo hai yaliyojengwa kuwa nyumba ya kiroho kwa kusudi la ukuhani mtakatifu.’​—1Pe 2:5.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki