-
Ni Nini Kitakachokusaidia Uendelee Kujifunza Biblia?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
4. Hakikisha kwamba kujifunza Biblia ni jambo muhimu kwako
Nyakati fulani huenda ukahisi una shughuli nyingi sana hivi kwamba huna wakati wa kujifunza Biblia. Ni nini kinachoweza kukusaidia? Soma Wafilipi 1:10, kisha mzungumzie maswali haya:
Unafikiri ni mambo gani yaliyo “muhimu zaidi” maishani?
Unaweza kufanya nini ili kujifunza Biblia kuwe jambo muhimu kwako?
Ukiweka mchanga kwenye ndoo kisha ujaribu kuongeza mawe, mawe hayatakuwa na nafasi ya kutosha
Ukiweka mawe kwanza kwenye ndoo utakuwa na nafasi ya kuongeza mchanga. Vivyo hivyo, ukitanguliza “mambo muhimu zaidi” maishani, utafaulu kuyatimiza na pia utakuwa na muda wa kufanya mambo mengine
Kujifunza Biblia hutimiza uhitaji wetu wa kiroho, yaani, uhitaji wetu wa kumjua na kumwabudu Mungu. Soma Mathayo 5:3, kisha mzungumzie swali hili:
Tutanufaikaje ikiwa tutaona kujifunza Biblia kuwa jambo muhimu maishani mwetu?
-
-
Chagua Burudani Inayomfurahisha YehovaFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
4. Tumia muda wako kwa hekima
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.
Ingawa ndugu katika video hiyo hakuwa akitazama jambo lisilofaa, tatizo lilikuwa wapi?
Soma Wafilipi 1:10, kisha mzungumzie swali hili:
Mstari huu unaweza kutusaidiaje kuamua muda tutakaotumia katika burudani?
-