Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wafilipi 4:6, 7—“Msihangaike Kuhusiana na Jambo Lolote”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
    • “Msihangaike kuhusiana na jambo lolote, bali katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani, mjulisheni Mungu maombi yenu; na amani ya Mungu inayozidi uelewaji wote itailinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili kupitia Kristo Yesu.”—Wafilipi 4:6, 7, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

      “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.”​—Wafilipi 4:6, 7, Union Version.

  • Wafilipi 4:6, 7—“Msihangaike Kuhusiana na Jambo Lolote”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
    • Mungu anajibu sala hizo kwa kuwapa waabudu wake amani. “Amani ya Mungu” ni utulivu ambao unatokana na urafiki wa karibu pamoja na Mungu. (Waroma 15:13; Wafilipi 4:9) Amani hiyo ‘inazidi uelewaji wote’ kwa sababu inatoka kwa Mungu na inaweza kutusaidia kuliko tunavyoweza kufikiri.

      Mstari huo wa Biblia unasema kwamba amani ya Mungu inaweza kulinda mioyo yetu. Neno la Kigiriki lililotafsiriwa “itailinda” ni neno lililotumika katika jeshi kufafanua kile ambacho kikosi cha jeshi kingefanya ili kulinda jiji lililozungukwa na kuta ndefu. Vivyo hivyo, amani ya Mungu hulinda hisia na akili ya mtu. Humsaidia kutolemewa na matatizo.

      Amani ambayo Mungu anatupatia inatulinda “kupitia Kristo Yesu,” kwa sababu kupitia Yesu tunaweza kuwa na uhusiano na Mungu. Yesu alitoa uhai wake ukiwa dhabihu kwa ajili ya dhambi zetu. Tunaweza kufurahia baraka za Mungu tukiwa na imani katika Yesu. (Waebrania 11:6) Tunaweza pia kusali kwa Mungu kupitia Yesu. Yesu alisema hivi: “Hakuna mtu anayekuja kwa Baba bila kupitia kwangu.”​—Yohana 14:6; 16:23.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki