-
“Ninyi na Mwe na Amani”Mnara wa Mlinzi—1988 | Februari 15
-
-
4. Ni jinsi gani watu wa Yehova wanadumisha amani ya akili na moyo katika hizi nyakati za hatari?
4 Sisi tunaishi katika wakati wa mwisho, katika “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.” (2 Timotheo 3:1, NW) Wale wapanda-farasi waliotabiriwa katika Ufunuo wanaendesha farasi zao kwa kupita katika dunia—kama vile ambavyo wewe unaweza kuona kutokana na vita, mapungufu ya chakula, na kifo ambacho kinatokana na magonjwa. (Ufunuo 6:3-8) Watu wa Yehova wanaathiriwa pia na hali zinazowazunguka. Kwa hiyo ni jinsi gani wewe unaweza kudumisha amani ya kimungu, ya akili na ya moyo? Kwa kuendelea kuwa karibu na kile Chanzo kikubwa cha faraja na amani. Kama vile ambavyo makala iliyotangulia ilionyesha, jambo hilo linataka sala na dua ya mara nyingi. Kwa njia hiyo ‘ile amani ya Mungu ambayo inapita mno fikira yote italinda moyo wako na nguvu zako za kiakili kwa njia ya Kristo Yesu.’—Wafilipi 4:6, 7, NW.
5. Kwa sababu gani Paulo alikuwa na uhakika kwamba “ile amani ya Mungu” ingeweza kulinda mioyo yetu?
5 Mtume Paulo, ambaye aliandika maneno hayo, alikuwa yeye mwenyewe amevumilia hatari na magumu. Yeye alikuwa ametiwa gerezani na kupigwa na Wayahudi na Waroma. Yeye alipigwa kwa mawe na akaachwa akidhaniwa kuwa mfu. Kusafiri katika siku hizo kulikuwa jukumu kubwa; Paulo alivunjikiwa na meli nyakati tatu, na mara nyingi yeye alikuwa katika hatari kutokana na wakora wa njia kuu. Yeye alitumia mausiku mengi yasiyo na usingizi na mara nyingi akataabishwa na baridi, njaa, na kiu. Zaidi ya yote hayo, kila siku yeye alihisi “sumbuko kwa ajili ya makundi yale yote.” (2 Wakorintho 11:24-28, NW) Kwa hiyo Paulo alijua kutokana na majionea yake mengi jinsi ilivyo ya maana “ile amani ya Mungu” ambayo inaweza kulinda mioyo yetu.
6. Kwa sababu gani ni jambo muhimu kusimamisha kwa uthabiti na kudumisha kifungo chenye uchangamfu na usiri pamoja na Muumba wetu?
6 “Ile amani ya Mungu” inaweza kuelezwa kuwa hisia ya ushwari na utulivu, ikionyesha uhusiano mwema pamoja na Mungu. Jambo hilo ni la maana sana kwa Wakristo, hasa wakati ambapo wao wanaelekeana na mnyanyaso au dhiki. Kwa sababu gani? Sisi sote ni watu wasio wakamilifu; kwa sababu hiyo, wakati tunaposumbuliwa-sumbuliwa na matatizo, mkazo, upinzani, au aina mbalimbali za vipingamizi, sisi tungeweza kwa urahisi kujawa na woga. Hiyo ingeweza kutuongoza tukose kuendeleza ukamilifu wetu. Jambo hilo lingeleta shtaka lenye aibu juu ya jina la Mungu, lingetuletea hasara ya kutokuwa na upendeleo wa Yehova, na lingeweza kutuongoza tupoteze uhai wa milele. Kwa hiyo ni jambo muhimu kama nini tujitahidi kupata “ile amani ya Mungu” ambayo itatusaidia tuelekeane na miito ya ushindani kwa mafanikio. Kwa uhakika amani hiyo ni moja ya zile ‘zawadi njema na matuzo makamilifu’ ambayo baba yetu wa kimbingu amefanya yapatikane.—Yakobo 1:17, NW.
7, 8. (a) “Ile amani ya Mungu” inategemea nini, na ni jinsi gani hiyo ‘inapita mno fikira yote’? (b) Kielelezo cha amani hiyo kilionyeshwa jinsi gani katika kisa cha ndugu mmoja Mwafrika?
7 Huenda wewe ukawa umeona kwamba watu fulani wanapita katika maisha wakiwa watulivu na wenye uhakika. Mara nyingi hiyo ni kwa sababu ya uweza ambao wamezaliwa nao, mavutano ya kijamaa, utajiri, elimu, au mambo mengine kama hayo. “Ile amani ya Mungu” ni tofauti sana na jambo hilo. Hiyo haitegemei kuwa na hali zinazofaa, wala haitokani na uweza au njia ya kibinadamu ya kufikiri. Inatokana na Mungu na ‘inapita mno fikira yote.’ Fasiri ya J. B. Phillips ya Wafilipi 4:7 ni kwamba “ile amani ya Mungu... inapita kwa mbali ufahamu wa kibinadamu.” Watu wa kilimwengu wanastaajabia mara nyingi njia ambayo Wakristo wanaelekeana na matatizo mazito, madhara ya kimwili, au hata kifo.
8 Kielelezo kimoja cha ki-siku-hizi juu ya jambo hilo ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova ambaye alikuwa akiongoza mkutano wa Kikristo katika nchi moja ya Kiafrika ambamo Mashahidi walishtakiwa juu ya kuwa wavamizi-haramu, hasa kwa sababu ya uchochezi wa Wakatoliki wa huko. Kwa ghafula, polisi wa kivita wenye bunduki-visu walitokea. Wao waliambia wanawake na watoto waende nyumbani lakini wakaanza kuwapiga wanaume. Shahidi huyo anakumbuka hivi: “Mimi sina maneno ya kusimulia namna sisi tulitendwa. Koporo-polisi mwenye kutusimamia alitangaza waziwazi kwamba sisi tungepigwa mpaka tufe. Mimi nilipokea mapigo makubwa sana kwa rungu ya mti hata baadaye nikatapika damu kwa siku 90. Lakini hangaikio langu lilikuwa uhai wa waandamani wangu. Katika sala nilimwomba Yehova atunze uhai wa hao, kondoo zake,” na wote walibaki hai. Hicho ni kielelezo kizuri kama nini cha kuendelea kuwa mtulivu katika janga baya sana na cha kufikiria wengine kwa upendo! Ndiyo, baba yetu wa kimbingu mwenye upendo anajibu matakwa yanayoombwa na watumishi wake waaminifu, akiwapa wao amani yake. Mmoja wa wale askari wenye kushangaa sana katika kisa hicho alisema kwamba Mungu wa Mashahidi “ndiye wa kweli bila shaka.”
9. Kuisoma Biblia na kutafakari juu yayo kunaweza kuwa na tokeo gani?
9 Katika nyakati hizi zenye magumu, Wakristo wengi wana matatizo ambayo yanawafanya wahisi wamevurugika fikira na kuvunjika moyo. Njia nzuri ya kudumisha amani ya akili ni kusoma Biblia na kutafakari juu yayo. Hiyo inaweza kumjaza mtu imara na hali ya kupiga moyo konde ili asonge mbele na kusimama kwa uthabiti. “Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu.”—Waebrania 4:12.
10. Ni jinsi gani kuweza kukumbuka maandiko kungeweza kuwa baraka?
10 Hata hivyo, namna gani ikiwa janga linatufikilia sisi wakati ambapo Biblia haipatikani? Mathalani, huenda Mkristo akakamatwa kwa ghafula na kusukumwa ndani ya jela bila Biblia. Katika kisa hicho, ingekuwa baraka halisi kuweza kukumbuka maandiko kama vile Wafilipi 4:6, 7; Mithali 3:5, 6; 1 Petro 5:6, 7; na Zaburi 23. Je! wewe hungethamini kwa kina kirefu kuweza kukumbuka na kufikiri sana juu ya vifungu kama hivyo? Katika kile kikao cha gereza kilicho na mambo makali, ingekuwa kama kwamba Yehova mwenyewe anakuambia wewe mambo. Neno la Mungu linaweza kuponya akili zilizoumizwa, kuimarisha kama ngome mioyo yenye kuzimia, na kuweka amani mahali pa mtaabiko-taabiko wa kiakili. (Ona Zaburi 119:165.) Ndiyo, ni jambo la maana kukaza sana maandiko katika akili zetu sasa maadamu sisi tuna fursa ya kufanya hivyo.
11. Ni jinsi gani ndugu mmoja katika Uholanzi alidhihirisha uhitaji wa chakula cha kiroho?
11 Arthur Winkler alikuwa mmoja ambaye alithamini Biblia kwa kina kirefu, hasa wakati Uholanzi ilipokuwa ikikaliwa na Wanazi, wakati Mashahidi walipolazimika kuendesha utendaji wao wa Kikristo chini-chini. Polisi wa siri walikuwa wamekuwa wakiwinda Ndugu Winkler. Wao walipomteka mwishowe, wao walijaribu kumwachisha msimamo wake lakini wakashindwa. Ndipo walipompiga mpaka akakosa fahamu. Meno yake yakiwa yamegongwa yakatoka, utaya wake wa chini ukiwa umetegushwa, na mwili wake kutandikwa bila huruma, yeye alitiwa ndani ya chumba cha jela chenye giza. Lakini mlinzi wake alikuwa mwenye huruma na urafiki. Ndugu Winkler alitafuta mwongozo wa Yehova katika sala. Pia alihisi kwa kina kirefu uhitaji wa chakula cha kiroho na akaomba mlinzi huyo msaada. Baadaye, mlango wa chumba kile cha jela ulifunguliwa, na Biblia ikatupwa ndani. “Ilikuwa furaha kama nini,” akakumbuka Ndugu Winkler, “kufurahia kila siku yale maneno yenye kufurahisha ya ukweli. . . Mimi nilijihisi nikipata imara zaidi kiroho.”a
Amani ya Kimungu Itakulinda Wewe Salama
12. Kwa sababu gani kuna uhitaji wa pekee kwetu sisi kulinda mioyo yetu na nguvu za kiakili? ‘
12 Yehova anaahidi kwamba amani yake “italinda mioyo yenu na nguvu zenu za kiakili.’ (Wafilipi 4:7, NW) Hilo ni jambo muhimu sana! Moyo ndicho kiti cha msukumo wa vitendo na cha hisi za moyoni. Katika hizi siku za mwisho, mioyo yetu inaweza kwa urahisi kudhoofishwa na woga au sumbuko, au kutushawishi sisi tufanye kosa. Kiolezo cha ujumla cha maisha kinaendelea kuzorota kwa haraka sana. Ni lazima sisi tuwe macho kujilinda daima. Zaidi ya kuhitaji mioyo imara, ni lazima sisi tutiwe imara pia katika ‘nguvu zetu za kiakili’ na kuelekezwa na Mungu kupitia Neno lake na kundi lake.
13. Ni manufaa gani ambazo zinakuja kwa kufanya nguvu zetu za kiakili ziwe zimelindwa?
13 Kulingana na W. E. Vine, neno la Kigiriki no’e-ma (lililofasiriwa ‘nguvu za kiakili’) linatoa wazo la “kusudi” au “ubuni wa akili.” (An Expository Dictionary of New Testament Words) Hivyo, amani ya Mungu inaweza kuimarisha kusudi letu la Kikristo na kutulinda sisi dhidi ya elekeo lo lote la kudhoofisha au kubadili akili zetu bila sababu njema. Hivyo mvunjiko-moyo au matatizo hayangetuachisha lengo letu kwa urahisi. Mathalani, ikiwa sisi tumekusudia kutumikia Yehova katika nafasi fulani ya pekee, kama vile kwa kuwa mhudumu painia wa wakati wote au kuhama ili kutumikia mahali ambako wahudumu wanahitajiwa sana, “ile amani ya Mungu” itakuwa msaada mkubwa kwetu sisi katika kuendelea kufuatia mradi huo. (Linganisha Luka 1:3; Matendo 15:36; 19:21; Warumi 15:22-24, 28; 1 Wathesalonike 2:1, 18.) Ili kuzidi kuimarisha nguvu zako za kiakili, toa wakati unaozidi kipimo kile cha kawaida uwe wa kujifunza Neno la Mungu na wa ushirika wa Kikristo. Kwa kufanya hivyo unakuwa ukilisha akili na moyo wako fikira safi, zenye kujenga. Je! wewe unaweza kutoa wakati wa kutosha ujihusishe mwenyewe ndani ya “semi” zilizovuviwa na Mungu? Je! wewe unapaswa kuzipa hizo fikira zaidi?
14. Ni shauri gani lililovuviwa na Mungu ambalo inatupasa sisi tulitii kwa uangalifu, na kwa sababu gani?
14 Unaweza kuona kwamba vyote viwili, moyo na akili, au nguvu za kiakili, vinahusika katika kujipatia na kunufaika kutokana na “ile amani ya Mungu.” Jambo hilo linaonyeshwa wazi katika lile shauri la kimungu: “Mwana wangu, tega sikio la uangalifu kwa maneno yangu. Inamisha sikio lako kuelekea semi zangu. Hizo zisiende mbali kutoka kwenye macho yako. Weka hizo katikati ya moyo wako. Kwa maana hizo ni uhai kwa wale ambao wanazipata na afya kwa mnofu wao wote. Zaidi ya kinginecho chote ambacho ni cha kulindwa, linda salama moyo wako wewe, kwa maana vyanzo vya uhai ni kutoka katika huo.”—Mithali 4:20-23, NW.
15. Yesu anatimiza sehemu gani katika kuwa kwetu na “ile amani ya Mungu”?
15 “Ile amani ya Mungu” ambayo inatokana na kifungo chenye uchangamfu na usiri pamoja na Yehova inalinda mioyo yetu na nguvu za kiakili “kwa njia ya Kristo Yesu.” (Wafilipi 4:7, NW) Ni fungu gani la kikazi ambalo Yesu anatimiza katika jambo hilo? Paulo anaeleza hivi: “Ninyi na mwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na yule Bwana Yesu Kristo. Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu sisi kwamba yeye aweze kutukomboa sisi kutoka mfumo mwovu wa mambo uliopo kulingana na mapenzi ya Mungu na Baba yetu.” (Wagalatia 1:3, 4, NW) Ndiyo, kwa upendo Yesu alitoa uhai wake ili sisi tuweze kukombolewa. (Mathayo 20:28) Kwa hiyo ni “kwa njia ya Kristo Yesu” kwamba sisi tunaweza kukubalika kwa Yehova tukiwa watumishi wake waliojitoa wakfu na kuwa katika msimamo wa kufurahia amani hiyo ya kimungu ambayo inaweza kutulinda sisi salama.
-
-
“Ninyi na Mwe na Amani”Mnara wa Mlinzi—1988 | Februari 15
-
-
20. Inampasa mtu ye yote ambaye anatenda kosa kubwa afanye nini?
20 Ikiwa wo wote wanakuwa wenye hatia ya kosa kubwa lakini wanalifunikiza, wao kwa uwazi watapoteza kibali cha Yehova “na ile amani ya Mungu” ambayo walikuwa nayo. Pia watapoteza amani ya akili yao wenyewe. (Linganisha 2 Samweli 24:10; Mathayo 6:22, 23.) Basi, wewe unaweza kuona ni kwa sababu gani lazima Mkristo ye yote ambaye ameanguka ndani ya dhambi aungame kwa Yehova na kwa wazee wenye upendo, ambao wanaweza kuendeleza ponyo la kiroho. (Isaya 1:18,19; 32:1, 2; Yakobo 5:14,15) Wakati mtu ambaye amepoteza usawaziko wa kiroho katika kile kijia chenye utelezi wa dhambi anapotafuta msaada kutoka kwa ndugu wakomavu, yeye hataendelea kuwa na dhamiri yenye mfadhaiko au kuwa bila amani ya kimungu.
21. Ni kisababishi gani cha shukrani za kina kirefu kwa Yehova ambacho sisi tunacho leo, na inatupasa sisi tuwe na hali gani ya kupiga moyo konde?
21 Ni pendeleo kama nini kuwa mmoja wa Mashahidi waliojitoa wakfu wa Yehova leo! Pande zote zinazotuzunguka sisi, ulimwengu huu wa kishetani unavunjika-vunjika na unakuwa vurugu-vurugu. Karibuni huo utapitilia mbali. Watu wengi ‘wanazimia kwa sababu ya woga na kwa kutazamia mambo yanayokuja juu ya dunia inayokaliwa.’ Lakini sisi tunaweza kuinua vichwa vyetu kwa sababu tunajua kwamba ‘ukombozi wetu unakaribia.’ (Luka 21:25-28, NW) Kuonyesha jinsi tulivyo wenye shukrani kwa Yehova kwa ajili ya ‘amani yake ambayo inapita mno fikira yote,’ acheni sisi tufanye yote yote ambayo tunaweza ili tutumikie kwa uaminifu “yule Mungu ambaye anatoa amani.”—Warumi 15:33; 1 Wakorintho 15:58, NW.
-