Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Ngono?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 4. Unaweza kupinga vishawishi

      Ni nini kinachoweza kufanya iwe vigumu kupinga kishawishi cha kufanya uasherati? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

      VIDEO: Shinda Vishawishi kwa Kusoma Biblia (3:02)

      • Ndugu katika video hiyo alifanya nini alipotambua kwamba mawazo na matendo yake yangefanya akose kuwa mwaminifu kwa mke wake?

      Wakati mwingine, hata Wakristo waaminifu hupambana ili kudumisha mawazo safi. Unawezaje kuacha kufikiria mawazo machafu? Soma Wafilipi 4:8, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Tunapaswa kufikiria mambo gani?

      • Kusoma Biblia na kuwa na shughuli nyingi katika utumishi wa Yehova, kunawezaje kutusaidia kupinga vishawishi vya kutenda dhambi?

  • Unawezaje Kumfurahisha Yehova Kupitia Mazungumzo Yako?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 3. Ni nini ambacho kitatusaidia kuzungumza kwa njia itakayowajenga wengine?

      Mara nyingi mambo tunayosema yanafunua kile kilicho moyoni mwetu au jambo ambalo tunafikiria. (Luka 6:​45) Basi, tunapaswa kujizoeza kufikiria mambo yenye kujenga, yaani, mambo yaliyo ya uadilifu, yaliyo safi kiadili, yanayopendeka, na yanayostahili sifa. (Wafilipi 4:8) Ili tukazie fikira mambo hayo, tunapaswa kuchagua burudani na marafiki wetu kwa hekima. (Methali 13:20) Pia, tunahitaji kufikiria kwa makini mambo tutakayosema kabla ya kuzungumza. Fikiria jinsi maneno yako yatakavyowaathiri wengine. Biblia inasema hivi: “Maneno yanayosemwa bila kufikiri huchoma kama upanga, lakini ulimi wa mwenye hekima huponya.”​—Methali 12:18.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki