Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ubatizo​—Lengo Muhimu!
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 3. Mtu anapaswa kuchukua hatua gani kabla ya kubatizwa?

      Kabla ya kubatizwa, unapaswa kujifunza kumhusu Yehova na kujenga imani yenye nguvu kwake. (Soma Waebrania 11:6.) Kadiri ujuzi na imani yako inavyozidi kuongezeka, ndivyo utakavyompenda Yehova zaidi. Bila shaka, utatamani kuwaambia wengine kumhusu na kuishi kulingana na viwango vyake. (2 Timotheo 4:2; 1 Yohana 5:3) Mtu anapoanza kuishi “kwa kumstahili Yehova ili kumpendeza kikamili,” inawezekana kwamba ataamua kujiweka wakfu kwa Mungu na kubatizwa.​—Wakolosai 1:9, 10.a

  • Ubatizo​—Lengo Muhimu!
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • a Ikiwa mwanzoni mtu alibatizwa katika dini nyingine, anahitaji kubatizwa tena. Kwa nini? Kwa sababu dini hiyo haikufundisha ukweli ulio katika Biblia.​—Ona Matendo 19:1-5 na Somo la 13.

  • Je, Uko Tayari Kubatizwa?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 1. Unahitaji kuwa na ujuzi mwingi kadiri gani kabla ya kubatizwa?

      Ili ubatizwe, unahitaji kuwa na “ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Timotheo 2:4) Hilo halimaanishi kwamba kabla ya kubatizwa unapaswa kujua majibu ya maswali yote ya Biblia ambayo huenda watu wakakuuliza. Hata Wakristo ambao walibatizwa miaka mingi iliyopita bado wanaendelea kujifunza. (Wakolosai 1:9, 10) Lakini unahitaji kuelewa mafundisho ya msingi ya Biblia. Wazee wa kutaniko watakusaidia kujua ikiwa una ujuzi wa kutosha.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki