-
Ufalme wa MunguUfahamu wa Kina wa Maandiko
-
-
“Ufalme wa Mwana wa Upendo Wake.” Siku kumi baada ya kupanda kwa Yesu kwenda mbinguni, katika Pentekoste ya 33 W.K., wanafunzi wake walikuwa na uthibitisho kwamba yeye “aliinuliwa kwenye mkono wa kuume wa Mungu” wakati Yesu alipomimina roho takatifu juu yao. (Mdo 1:8, 9; 2:1-4, 29-33) Hivyo, lile “agano jipya” likaanza kutenda kuwaelekea, nao wakawa kiini cha “taifa takatifu” jipya, Israeli wa kiroho.—Ebr 12:22-24; 1Pe 2:9, 10; Gal 6:16.
Sasa Kristo alikuwa ameketi kwenye mkono wa kuume wa Baba yake naye alikuwa ni Kichwa juu ya kutaniko hili. (Efe 5:23; Ebr 1:3; Flp 2:9-11) Maandiko yanaonyesha kwamba kuanzia Pentekoste 33 W.K. na kuendelea, ufalme wa kiroho ulisimamishwa juu ya wanafunzi wake. Akiwaandikia Wakristo wa karne ya kwanza katika Kolosai, mtume Paulo alirejelea Yesu Kristo kana kwamba tayari ana ufalme: “[Mungu] alitukomboa kutoka katika mamlaka ya giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa upendo wake.”—Kol 1:13; linganisha Mdo 17:6, 7.
Ufalme wa Kristo kuanzia Pentekoste ya 33 W.K. na kuendelea umekuwa ni wa kiroho, ukitawala juu ya Israeli wa kiroho, Wakristo ambao wamezaliwa kupitia roho ya Mungu ili wawe watoto wa kiroho wa Mungu. (Yoh 3:3, 5, 6) Wakati Wakristo hao waliozaliwa kwa roho watakapopokea thawabu yao ya kimbingu, hawatakuwa tena raia za kidunia wa ufalme wa kiroho wa Kristo, bali watakuwa wafalme pamoja na Kristo mbinguni.—Ufu 5:9, 10.
-
-
Ufalme wa MunguUfahamu wa Kina wa Maandiko
-
-
“Bwana wetu,” Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ndiye anayethibitisha mamlaka yake juu ya “ufalme wa ulimwengu,” akisimamisha udhihirisho mpya wa enzi yake kuu kuielekea dunia yetu. Yeye anampa mwanaye, Yesu Kristo, hisa ndogo katika Ufalme huo, hivi kwamba unaitwa “ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake.” Kiwango na mweneo wa Ufalme huo ni mkubwa zaidi ya “ufalme wa Mwana wa upendo wake,” unaotajwa kwenye Wakolosai 1:13. “Ufalme wa Mwana wa upendo wake” ulianza katika Pentekoste 33 W.K. nao umekuwa juu ya wanafunzi watiwa-mafuta wa Kristo; “ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake” unatokezwa mwishoni mwa “nyakati zilizowekwa za mataifa” nao uko juu ya jamii yote ya wanadamu duniani.—Lu 21:24.
-