Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha—Sehemu ya 1
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • Hakuna ndoa iliyo kamilifu. Kwa hiyo, mume na mke wanapaswa kushirikiana ili kushinda matatizo. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

      VIDEO: Jinsi ya Kuimarisha Kifungo cha Ndoa (5:44)

      • Katika video hiyo, ni mambo gani yanayoonyesha kwamba uhusiano kati ya mume na mke ulianza kudhoofika?

      • Walifanya nini ili kuimarisha ndoa yao?

      Soma 1 Wakorintho 10:24 na Wakolosai 3:13. Baada ya kusoma kila andiko, zungumzieni swali hili:

      • Kufuata ushauri huo kunawezaje kuimarisha ndoa?

      Biblia inasema kwamba tunapaswa kuheshimiana. Kumheshimu mtu kunatia ndani kumtendea kwa njia ya fadhili na staha. Soma Waroma 12:10, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Je, mume au mke anapaswa kutarajia kwamba mwenzi wake ndiye anayepaswa kuwa wa kwanza kuonyesha heshima? Kwa nini?

  • Dumisha Umoja Katika Kutaniko
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 3. Utafanya nini hali ya kutoelewana ikitokea kati yako na Mkristo mwenzako?

      Ingawa tuna umoja, sisi si wakamilifu. Wakati fulani, tunaweza kuwavunja moyo waabudu wenzetu au kuwaumiza hisia. Kwa hiyo, Neno la Mungu linatuhimiza hivi: “Endeleeni . . . kusameheana,” kisha linaongeza hivi: “Kama vile Yehova alivyowasamehe kwa hiari, nanyi lazima mfanye vivyo hivyo.” (Soma Wakolosai 3:13.) Sisi humkosea Yehova mara nyingi sana, hata hivyo bado anatusamehe. Basi anataka tuwasamehe ndugu zetu. Ukigundua kwamba umemkosea mtu fulani, chukua hatua ya kwanza ili kusuluhisha tatizo hilo.​​—Soma Mathayo 5:​23, 24.b

  • Dumisha Umoja Katika Kutaniko
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 5. Samehe kwa hiari na ufanye amani

      Yehova hutusamehe kwa hiari ingawa yeye hahitaji kamwe sisi tumsamehe. Soma Zaburi 86:5, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Yehova husamehe kwa njia kubwa jinsi gani?

      • Kwa nini unathamini msamaha wake?

      • Ni hali gani zinazoweza kusababisha kutoelewana kati yetu na watu wengine?

      Tunawezaje kumwiga Yehova na kuendelea kushirikiana na ndugu na dada zetu kwa umoja? Soma Methali 19:11, kisha mzungumzie swali hili:

      • Mtu anapofanya jambo linalokuudhi au kukukasirisha, unaweza kufanya nini ili kusuluhisha hali hiyo?

      Wakati fulani sisi huwakosea wengine. Unapaswa kufanya nini hilo linapotokea? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

      VIDEO: Kufanya Amani Huleta Baraka (6:01)

      • Katika video hiyo, dada huyo alichukua hatua gani ili kufanya amani?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki