-
Amani na Usalama wa Kweli Ni Karibu!Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
-
-
3 Unabii wa Biblia wenye kupendeza ulieleza kwamba wakati ungefika ambapo viongozi wa ulimwengu wangetangaza “amani na usalama!”a Kwa kweli, wakati Umoja wa Mataifa ulipotangaza 1986 kuwa “Mwaka wa Kimataifa wa Amani” uliuliza matengenezo kila mahali yafanye jitihada ya pekee kuanzia mwaka huo na kuendelea yaendeleze mradi wa “amani, usalama wa kimataifa na ushirikiano.”1
4. Ili mpango wo wote wa amani na usalama ukunufaishe wewe, ni matatizo gani ambayo lazima utatue?
4 Lakini je! hiyo ingekuwa “amani na usalama” wa kweli? Je! ungefika ndani ya ujirani wako na ndani ya nyumba yako na kuondoa matatizo yanayokupata wewe binafsi? Je! ungetatua tatizo la kuongezeka kwa uhalifu na uzoelevu wa dawa za kulevya, gharama zenye kupanda za chakula, kutozwa sana kodi, uchafuzi unaoenea, na kudhoofika daima kwa vifungo vya jamaa? Maadamu zo zote za hali hizi zinaendelea, zinaelekea kuharibu amani na usalama wako binafsi.
5, 6. Kwa msingi wa mambo ambayo umejionea mwenyewe maishani, je! wewe unaamini kwamba wanadamu watayatatua matatizo hayo?
5 Kweli, wanadamu wanatumaini kwamba wao wanaweza kuyaondoa magumu hayo. Wanasema kwamba, wakiwa huru na gharama zinazowalemea za vita, wanaweza kutumia mali ile yote, uchunguzi, na wafanyi kazi kuyatatua matatizo haya.
6 Je! kweli wewe waamini hayo? Je! kuna ushuhuda wo wote ulio hakika unaoonyesha kwamba wanadamu wanaweza kuleta matatuzi yenye kudumu? Historia inaonyesha nini? Kwa kweli, mambo ambayo wewe umejionea mwenyewe maishani yanakuambia nini?
-
-
Amani na Usalama wa Kweli Ni Karibu!Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
-
-
10 Kwa kupendeza, unabii wa Biblia kuhusu “amani na usalama” uliotangulia kuzungumzwa unatia ndani sehemu hizi: “Wakati wo wote wanaposema: ‘Amani na usalama!’ ndipo uharibifu wa ghafula utakapokuwa juu yao papo kwa hapo.” (1 Wathesalonike 5:3, NW) Kwa hiyo ni wazi kwamba amani yo yote wanayotangaza viongozi wa kibinadamu itakuwa ya muda mfupi sana. Kwa kuwa unabii unaonyesha kwamba mara tu baadaye tawala zote za kibinadamu zitavunjwa-vunjwa na kuondolewa zisiwepo, na mahali pazo patachukuliwa na serikali moja duniani pote—Ufalme wa Mungu.
-