Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuthamini “Zawadi Zikiwa Wanadamu”
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Juni 1
    • “Mwape Ufikirio Ambao Ni Zaidi Kuliko Ule wa Kawaida”

      14, 15. (a) Kulingana na 1 Wathesalonike 5:12, 13, ni kwa nini wazee hustahili ufikirio wetu? (b) Kwa nini inaweza kusemwa kwamba wazee ‘wanafanya kazi kwa bidii miongoni mwetu’?

      14 Pia, tunaweza kuwathamini “zawadi zikiwa wanadamu” kwa kuwapa ufikirio. Akiliandikia kutaniko huko Thesalonike, Paulo aliwashauri washiriki wake hivi: “Mwe na staha kwa wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu na kuwasimamia nyinyi katika Bwana na kuwaonya nyinyi kwa upole; na mwape ufikirio ambao ni zaidi kuliko ule wa kawaida katika upendo kwa sababu ya kazi yao.” (1 Wathesalonike 5:12, 13) ‘Kufanya kazi kwa bidii’—je, hilo halifafanui wazee ambao hujitolea wenyewe bila ubinafsi kwa niaba yetu? Fikiria kidogo ule mzigo mzito ambao ndugu hawa wapendwa huubeba.

  • Kuthamini “Zawadi Zikiwa Wanadamu”
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Juni 1
    • 16. Eleza jinsi tuwezavyo kuwapa wazee ufikirio.

      16 Tunaweza kuwaonyeshaje ufikirio? Mithali ya Biblia yasema hivi: “Neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini!” (Mithali 15:23; 25:11) Hivyo, maneno yenye uthamini wa kweli na yenye kutia moyo yaweza kuwaonyesha kuwa hatuipuuzi kazi yao ya bidii. Pia, tunapaswa kusawazika kuhusiana na yale tunayowatazamia watimize. Kwa upande mwingine, tunapaswa kujisikia huru kuwaendea ili kupata msaada. Huenda kukawa nyakati ambapo ‘moyo wetu unaumia ndani yetu’ nasi tunahitaji kitia-moyo, mwongozo, au mashauri ya Kimaandiko ya wale ambao wana “sifa ya kustahili kufundisha” Neno la Mungu. (Zaburi 55:4; 1 Timotheo 3:2) Wakati huohuo, tunahitaji kukumbuka kwamba mzee hawezi kutupa wakati mwingi mno, kwa kuwa hawezi kupuuza mahitaji ya familia yake mwenyewe au ya wengine kutanikoni. Tukiwa na “hisia-mwenzi” kwa hawa ndugu wanaofanya kazi kwa bidii, hatungependa kudai mengi mno kutoka kwao. (1 Petro 3:8) Badala yake, acheni tuthamini wakati na uangalifu wowote ule ambao kwa kufaa wanaweza kutupa.—Wafilipi 4:5.

      17, 18. Wake wengi ambao waume zao ni wazee hujidhabihu kwa njia zipi, nasi tunaweza kuonyeshaje kuwa hatuwapuuzi dada hawa waaminifu?

      17 Vipi kuhusu wake wa wazee? Je, wao pia hawastahili ufikirio wetu? Kwani, hawa wanashiriki waume zao na kutaniko. Mara nyingi hali hiyo huhitaji wajidhabihu. Mara kwa mara, wazee hulazimika kutumia saa za jioni wakitunza mambo ya kutaniko ilhali wangekuwa wakitumia wakati huo pamoja na familia zao. Katika makutaniko mengi, wanawake Wakristo waaminifu wanajidhabihu kwa hiari ili waume zao waweze kutunza kondoo za Yehova.—Linganisha 2 Wakorintho 12:15.

      18 Tunaweza kuonyeshaje kwamba hatuwapuuzi hawa dada Wakristo waaminifu? Kwa hakika tunaweza kufanya hivyo kwa kutodai mengi mno kutoka kwa waume zao. Na vilevile tusisahau pia uwezo wa maneno sahili ya shukrani. Mithali 16:24 yasema hivi: “Maneno yapendezayo ni kama sega la asali; ni tamu nafsini, na afya mifupani.” Fikiria jambo hili lililoonwa. Baada ya mkutano wa Kikristo, wenzi wawili wa ndoa walimwendea mzee na kumwomba waongee naye kuhusu mwana wao tineja. Mzee huyo alipokuwa akiongea na wenzi hao, mke wake alingojea kwa subira. Baadaye, mama huyo akamwendea mke wa mzee na kusema: “Ningependa kukushukuru kwa ajili ya wakati ambao mume wako alitumia ili kusaidia familia yangu.” Maneno hayo ya shukrani, yaliyo sahili na matamu kwa kweli yaliugusa moyo wa mke huyo wa mzee.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki